< San Lucas 16 >
1 Y otra vez dijo a los discípulos: Había un hombre de gran riqueza que tenía un administrador; y se le dijo que este siervo estaba desperdiciando sus bienes.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Palikuwa na tajiri mmoja na msimamizi wake. Ilisemekana kwamba huyo msimamizi alikuwa anatumia vibaya mali ya tajiri yake.
2 Y envió a buscarlo, y dijo: ¿Qué es esto que se dice de ti? dame una cuenta de todo lo que has hecho, porque ya no serás el administrador de mi propiedad.
Hivyo huyo tajiri akamwita na kumuuliza, ‘Ni mambo gani haya ninayoyasikia kukuhusu? Toa taarifa ya usimamizi wako, kwa sababu huwezi kuendelea kuwa msimamizi.’
3 Y el administrador se dijo a sí mismo: ¿Qué he de hacer ahora que mi señor me quita mi puesto? No tengo la fuerza suficiente para trabajar en el campo, y me avergonzaría si pidiera dinero a la gente en las calles.
“Yule msimamizi akawaza moyoni mwake, ‘Nitafanya nini sasa? Bwana wangu ananiondoa katika kazi yangu. Sina nguvu za kulima, nami ninaona aibu kuombaomba.
4 He tomado una decisión sobre qué hacer, para que cuando me saquen de mi posición me lleven a sus casas.
Najua nitakalofanya ili nikiachishwa kazi yangu hapa, watu wanikaribishe nyumbani kwao.’
5 Y enviando por cada uno que estaba en deuda con su señor, dijo al primero: ¿Cuál es el monto de su deuda con mi señor?
“Kwa hiyo akawaita wadeni wote wa bwana wake, mmoja mmoja. Akamuuliza wa kwanza, ‘Deni lako kwa bwana wangu ni kiasi gani?’
6 Y él dijo: Cien medidas de aceite. Y él dijo: Toma tu cuenta de inmediato y pon cincuenta.
“Akajibu, ‘Galoni 800za mafuta ya mizeituni.’ “Msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati ya deni lako, ibadilishe upesi, uandike galoni 400.’
7 Entonces dijo a otro: ¿Cuál es el monto de tu deuda? Y él dijo: Cien medidas de grano. Y él le dijo: Toma tu cuenta y baja a ochenta.
“Kisha akamuuliza wa pili, ‘Wewe deni lako ni kiasi gani?’ “Akajibu, ‘Vipimo 1,000vya ngano.’ “Yule msimamizi akamwambia, ‘Chukua hati yako, andika vipimo 800!’
8 Y su señor alabó al mal administrador, porque él había sido sabio; porque los hijos de este mundo son más sabios en los negocios del mundo pecador que los hijos de la luz. (aiōn )
“Yule bwana akamsifu yule msimamizi dhalimu kwa jinsi alivyotumia ujanja. Kwa maana watu wa dunia hii wana ujanja zaidi wanapojishughulisha na mambo ya dunia kuliko watu wa nuru. (aiōn )
9 Y les digo: hagan amigos por la riqueza de este mundo pecador, para ganarse amigos para que cuando la riquezas se acaben y llegue a su fin, sean llevados a los eternos lugares de descanso. (aiōnios )
Nawaambia, tumieni mali ya kidunia kujipatia marafiki, ili itakapokwisha, mkaribishwe katika makao ya milele. (aiōnios )
10 El que es fiel en lo poco, es fiel en lo mucho; el que no es honrado en lo poco. no es honrado en lo mucho.
“Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, pia ni mwaminifu hata katika mambo makubwa, naye mtu ambaye si mwaminifu katika mambo madogo pia si mwaminifu katika mambo makubwa.
11 Si, entonces, no has sido fiel en las riquezas de este mundo pecador, ¿quién les confiará la verdadera riqueza?
Ikiwa hamkuwa waaminifu katika mali ya kidunia, ni nani atakayewaaminia mali ya kweli?
12 Y si no has sido fiel en el cuidado de la propiedad de otras personas, ¿quién les dará lo que les pertenece?
Nanyi kama hamkuwa waaminifu na mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?
13 Ninguno puede ser siervo de dos señores; porque él tendrá odio por uno y amor por el otro; o se quedará con el uno y no tendrá respeto por el otro. No pueden ser siervos de Dios y de la riqueza.
“Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.”
14 Y los fariseos, que tenían un gran amor al dinero, al oír estas cosas, se burlaban de él.
Mafarisayo, waliokuwa wapenda fedha, waliyasikia hayo yote na wakamcheka kwa dharau.
15 Y él dijo: Ustedes tienen cuidado de parecer buenos a los ojos de los hombres, pero Dios conoce sus corazones; y las cosas que son importantes en opinión de los hombres, son aborrecidas a los ojos de Dios.
Yesu akawaambia, “Ninyi mnajionyesha kuwa wenye haki mbele za wanadamu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana vile vitu ambavyo wanadamu wanavithamini sana, kwa Mungu ni machukizo.
16 La ley y los profetas fueron hasta Juan; pero luego vino la predicación del reino de Dios, y todos se esfuerzan para entrar en el.
“Sheria na Manabii vilihubiriwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa, na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu.
17 Pero el cielo y la tierra llegarán a su fin antes de que la letra más pequeña de la ley deje de cumplirse.
Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria.
18 Todo aquel que se divorcia de su mujer y toma a otra, adultera; y el que está casado con una mujer cuyo marido la ha abandonado, adúltera.
“Mtu yeyote amwachaye mkewe na kumwoa mwanamke mwingine anazini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa anazini.
19 Y había cierto hombre de gran riqueza, que estaba vestido con ropas de púrpura y delicado lino, y estaba resplandeciente y alegre todos los días.
“Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa kila siku.
20 Y un pobre hombre, llamado Lázaro, estaba tendido a la puerta, lleno de heridas,
Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.
21 Deseando los trozos de comida que salían de la mesa del hombre rico; y hasta los perros vinieron y pusieron sus lenguas sobre sus heridas.
Huyo Lazaro alitamani kujishibisha kwa makombo yaliyoanguka kutoka mezani kwa yule tajiri. Hata mbwa walikuwa wakija na kuramba vidonda vyake.
22 Y con el tiempo el pobre hombre llegó a su fin, y los ángeles lo llevaron al seno de Abraham. Y el hombre rico llegó a su fin y fue sepultado.
“Wakati ukafika yule maskini akafa, nao malaika wakamchukua akae pamoja na Abrahamu. Yule tajiri naye akafa na akazikwa.
23 Y en el infierno, estando en gran dolor, alzando sus ojos vio a Abraham, muy lejos, y Lázaro sobre su seno. (Hadēs )
Kule kuzimu alipokuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Abrahamu kwa mbali, naye Lazaro alikuwa karibu yake. (Hadēs )
24 Y él dio un grito y dijo: Padre Abraham, ten misericordia de mí y envía a Lázaro, para que él ponga la punta de su dedo en agua y la ponga sobre mi lengua, porque yo estoy ardiendo cruelmente en esta llama.
Hivyo yule tajiri akamwita, ‘Baba Abrahamu, nihurumie na umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake ndani ya maji aupoze ulimi wangu, kwa sababu nina maumivu makuu kwenye moto huu.’
25 Pero Abraham dijo: Ten en cuenta, hijo mío, que cuando vivías, tenías tus bienes, mientras que Lázaro tenía sus males; pero ahora, él es consolado y tú tienes dolor.
“Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
26 Y además, hay una división profunda entre nosotros y usted, para que aquellos que puedan ir de aquí a usted no puedan hacerlo, y nadie puede venir de usted hacia nosotros.
Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
27 Y él dijo: Padre, es mi petición que lo envíes a la casa de mi padre;
“Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
28 Porque tengo cinco hermanos; y que les dé cuenta de estas cosas, para que no lleguen a este lugar de dolor.
maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
29 Pero Abraham dijo: Ellos tienen a Moisés y los profetas; que escuchen lo que dicen.
“Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
30 Y él dijo: No, padre Abraham, pero si alguien fuera a ellos de entre los muertos, cambiarían sus corazones.
“Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
31 Y le dijo: Si no quieren prestar atención a Moisés y a los profetas, no creerán aunque alguno vuelva de entre los muertos.
“Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’”