< Levítico 16 >

1 Y él Señor dijo a Moisés, después de la muerte de los dos hijos de Aarón, cuando tomaron fuego extraño delante del Señor y la muerte los alcanzó;
Yahwe alizungumza na Musa - hii ni baada vifo vya wana wawili wa Haruni, walipomkaribia Yahwe na ndipo wakafa.
2 El Señor le dijo a Moisés: Dile a Aarón, tu hermano, que no puede venir en todo momento al lugar santo dentro del velo, delante del propiciatorio, por temor a que la muerte lo alcance; porque seré visto en la nube en la cubierta del cofre.
Yahwe alimwambia Musa, “Ongea na Haruni kaka yako na umwambie hapana kuja tu wakati wowote katika patakatifu pa patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kifuniko cha upatanisho kilicho juu ya sanduku. Akifanya hivyo, anakufa, kwasababu naonekana katika wingu juu ya kifuniko cha upatanisho.
3 Dejemos que Aarón venga al lugar santo de esta manera: con un buey para el sacrificio por el pecado y un carnero para el sacrificio.
Hivi ndivyo jinsi Haruni lazima aje katika patakatifu pa patakatifu. Yeye lazima aingie pamoja na ndama kama sadaka ya dhambi, na kondoo dume kama sadaka ya dhambi.
4 Deja que se ponga el saco de lino sagrado, el pantalón de lino sobre su cuerpo, él cinto de lino ceñido y la mitra de lino sobre la cabeza porque esto es ropa santa, y antes de ponerlos sobre su cuerpo, debe ser lavado con agua.
Ni lazima avae kanzu ya kitatani, na lazima avae ndani yake nguo ya kitani, na lazima avae mshipi wa kitani na kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu. Lazima aoge mwili wake katika maji na avae mavazi haya.
5 Y que tome de los hijos de Israel dos chivos para el sacrificio por el pecado y un carnero para el holocausto.
Lazima achukue kwenye umati wa watu wa Israeli mbuzi wawili waume kama sadaka ya dhambi na kondoo dume moja ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa.
6 Y Aarón debe dar el buey de la ofrenda por el pecado para sí mismo, para que él y su casa se liberen del pecado.
Ndipo Haruni lazima alete ng'ombe kama sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake.
7 Y él tiene que tomar las dos cabras y ponerlas delante del Señor en la puerta de la tienda de la reunión.
Ndipo lazima achukue mbuzi wawili na kuwaweka mbele ya Yahwe katika mlango wa kuingilia kwenye hema ya mkutano.
8 Y Aarón echará suertes sobre los dos machos cabríos, una suerte para el Señor y una suerte para él macho cabrío expiatorio.
Ndipo Haruni lazima apige kura kwaajili ya mbuzi hao wawili, kura moja kwaajili ya Yahwe, na kura nyingine kwaajili ya msingiziwa.
9 Y el macho cabrío que está marcada para el Señor, deja que Aarón haga una ofrenda por el pecado.
Ndipo Haruni lazima awasilishe mbuzi ambaye kura imeangukia kwa Yahwe, na kumtoa mbuzi huyo kama sadaka ya dhambi.
10 Pero el macho cabrío expiatorio debe colocarse vivo delante del Señor, para quitar el pecado, para que pueda ser enviada con todas las maldad de ellos a las tierras del desierto.
Lakini mbuzi ambaye kura ya usingiziwa imemwangukia lazima aletwe kwa Yahwe akiwa hai, kufanya upatanisho kwa kumwachia aende porini kama, mbuzimsingiziwa.
11 Y Aarón debe dar el becerro de la ofrenda por el pecado para sí mismo y quitar el pecado de sí mismo y de su casa, y matar el becerro de la ofrenda por el pecado que es para sí mismo.
Pia Haruni lazima alete ng'ombe kwaajili ya sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwaajili yake mwenyewe, lazima afanye upatanisho kwaajili yake mwenyewe na familia yake, hivyo lazima yeye amuue huyo ng'ombe kama sadaka ya dhambi kwaajili yake mwenyewe.
12 Y él tomará un vaso lleno de brasas que se quema del altar delante del Señor y en su mano un poco de incienso, y lo llevará dentro del velo;
Haruni lazima achukue chetezo iliyojaa mkaa wa moto kutoka kwenye madhabahu mbele ya Yahwe, na mikono imejaa ubani mzuri, na kuleta vitu hivi ndani ya pazia.
13 Y tomará el incienso sobre el fuego delante del Señor para que el cofre se cubra con una nube del humo del perfume, que está sobre él testimonio para que la muerte no lo alcance.
Hapo lazima aweke ubani juu ya moto mbele za Yahwe ili kwamba wingu kutoka kwenye ubani liweze kufunika kifuniko cha agano la imani ya upatanisho. Yeye afanye hivyo ili kwamba asife.
14 Y tomará algo de la sangre del buey, sacudiendo sus gotas de su dedo encima del propiciatorio en el lado este, y delante del propiciatorio, siete veces.
Ndipo lazima achukue kiasi cha damu ya ng'ombe na kuinyunyiza kwa kidole chake mbele ya kifuniko cha upatanisho. Lazima anyunyize kiasi cha damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko cha upatanisho.
15 Entonces, degollara al macho cabrío de la ofrenda por el pecado, y lleva su sangre al interior del velo y haz con él lo que hizo con la sangre del buey, sacudiendo gotas encima y delante del cofre del pacto.
Ndipo lazima aue mbuzi kwaajili ya sadaka ya dhambi ambayo ni kwaajili ya watu na kuileta damu yake ndani kwenye pazi. Hapo lazima aifanyie damu kama alivyofanya kwenye damu ya fahali: lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho.
16 Y libere el lugar santo de todo lo que sea inmundo entre los hijos de Israel y de su maldad en todos sus pecados; y que haga lo mismo con la Tienda de reunión, que tiene su lugar entre un pueblo impuro.
Yeye lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli, na kwa sababu ya uasi na dhambi zao zote. Yeye pia lazima afanye haya kwaajili ya hema ya mkutano, ambapo Yahwe anaishi kati yao, katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.
17 Y ningún hombre puede estar en la Tienda de reunión desde el momento en que Aarón entra para quitar el pecado en el lugar santo hasta que salga, habiéndose hecho a sí mismo, a su casa y a todo el pueblo de Israel libres del pecado.
Hakuna mtu anayetakiwa kuwepo katika hema ya mkutano wakati Haruni anaingia kufanya upatanisho katika mahali patakatifu pa patakatifu, na mpaka atoke nje na amemaliza kufanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya familia yake, na kwaajili umati wa Israeli.
18 Y saldrá al altar que está delante del Señor y lo liberará del pecado; y él debe tomar algo de la sangre del buey y la sangre del chivo y ponerla en los cuernos del altar y rodearla;
Yeye lazima aende nje kwenye madhabahu hapo mbele za Yahwe na kufanya upatanisho kwaajili ya hiyo, na lazima achukue kiasi cha damu ya mbuzi na kuiweka juu ya pembe za madhabahu yote kuzunguka.
19 Sacudir las gotas de sangre de su dedo en él siete veces para santificarlo y limpiarlo de todo lo que sea inmundo entre los hijos de Israel.
Anatakiwa anyunyize kiasi cha damu juu yake kwa kidole chake mara saba kuitakasa na kuitenga maalumu kwa Yahwe, mbali kutoka matendo ya unajisi wa watu wa Israeli.
20 Y cuando haya hecho lo que sea necesario para hacer que el lugar santo y la Tienda de reunión y el altar estén libres de pecado, ponga al chivo viviente delante del Señor;
Atakapo maliza kupatanisha kwaajili ya mahali patakatifu sana, hema la mkutano, na madhabahu, lazima amlete mbuzi aliyehai.
21 Y Aarón, poniendo sus dos manos sobre la cabeza del chivo viviente, hará una declaración pública sobre él de todas las malas acciones de los hijos de Israel y de todas sus malas acciones, en todos sus pecados; y los pondrá sobre la cabeza del chivo y lo enviará lejos, al cuidado de un hombre que lo estará esperando allí, lo llevará y soltará en él desierto.
Haruni lazima aweke mikono yake yote juu ya kichwa cha mbuzi huyu aliyehai na akiri juu yake maovu yote ya watu wa Israeli, uasi wao wote, dhambi zao zote. Ndipo lazima aweke dhambi hizo juu ya kichwa cha mbuzi na amwachie katika uangalizi wa mtu aliyetari kumwongoza mbuzi huyo porini.
22 Y él chivo llevará sobre sí, todos sus pecados a una tierra separada de los hombres, y él enviará al chivo al desierto.
Mbuzi lazima abebe juu yake mwenyewe uovu wote kwenda mahali pakiwa. Kule msituni, huyo mtu amwache mbuzi aende huru.
23 Entonces, Aarón entrará en la Tienda de la reunión y se quitará la ropa de lino que se puso cuando entró en el lugar santo, y la dejara allí;
Ndipo Haruni anapaswa kwenda tena humo kwenye hema ya mkutano na kuvua mavazi ya kitani ambayo amayavaa kabla hajaenda mahali patakatifu sana, na anatakiwa kuyaacha mavazi hayo pale.
24 Y después se bañará su cuerpo en agua en un lugar santo, debe ponerse su ropa y salir y dar su ofrenda quemada y la ofrenda quemada de la gente, para quitar su pecado y el pecado de la gente.
Anapaswa aoshe mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na avae nguo zake za kawaida; pia lazima atoke nje kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya kuteketezwa kwaajili ya wale watu, na kwa njia hii anafanya upatanisho kwaajili yake mwenyewe na kwaajili ya watu.
25 Y la grasa de la ofrenda por el pecado será quemada por él en el altar.
Lazima yeye achome mafuta ya sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
26 Y el hombre que soltó el chivo; como chivo expiatorio debe lavarse la ropa y bañar su cuerpo en agua para luego regresar al campamento de la tienda.
Huyu mtu anayemwacha mbuzi msingiziwa aende huru anafua nguo zake na kuosha mwili wake katika maji; baada ya hayo, anaweza kurudi tena kambini.
27 Y el becerro de la ofrenda por el pecado y él chivo de la ofrenda por el pecado, cuya sangre fue tomada para hacer que el lugar santo esté libre del pecado, deben ser sacados fuera del campamento de la Tienda, sus pieles, la carne y sus desperdicios serán quemados con fuego.
Yule fahali kwaajili ya sadaka ya dhambi na mbuzi kwaajili ya sadaka za dhambi, ambaye damu yake ililetwa kufanya upatanisho katika mahali patakatifu, lazima ipelekwe nje ya kambi. kule lazima wachome, ngozi zao, nyama yao na kinyesi chao.
28 Y el hombre por el cual son quemados es lavado, su ropa y su cuerpo bañado en agua, para luego regresar al campamento de la tienda.
Huyu anayechoma sehemu hizo lazima afue nguo zake na aoge mwili wake katika maji; baada ya hapo, anaweza kurudi tena kwenye kambi.
29 Y sea para ustedes una orden para siempre: en el séptimo mes, en el décimo día, deben mantenerse a sí mismos sin placer y no hacer ningún tipo de trabajo, los que son israelitas de nacimiento y los de otras tierras. quienes viven entre ustedes.
Hii itakuwa sharti kwaajili yenu kwamba katika mwezi wa saba, kwenye siku ya kumi ya mwezi, mtanyenyekea wenyewe na msifanye kazi, iwe mwenyeji wa kuzaliwa au mgeni anayeishi kati yenu.
30 Porque en este día tu pecado será quitado y serás limpio: serás libre de todos tus pecados ante el Señor.
Hii ni kwasababu katika siku hii ya upatanisho utafanywa kwaajili yenu, kuwatakasa ninyi kutoka dhambi zenu zote ili mwe safi mbele za Yahwe.
31 Es un sábado especial para ustedes, y ustedes deben humillarse; Es una orden para siempre.
Hii ni maalumu kwa Sabato ya kupumzika kwaajili yenu, na lazima mnyenyekee wenyewe na msifanye kazi. Hili litakuwa sharti kati yenu.
32 Y el hombre sobre cuya cabeza se ha puesto el aceite santo, y que ha sido señalado como sacerdote en lugar de su padre, hará lo que sea necesario para quitar el pecado, y se pondrá la ropa de lino. incluso las ropas santas.
Kuhani mkuu, ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu kuwa kuhani mkuu katika nafasi ya baba yake, lazima afanye upatanisho huu na kuvaa mavazi ya kitani, hayo ni mavazi matakatifu.
33 Y hará la purificación del lugar santo y la Tienda de reunión y el altar del pecado; Él quitará el pecado de los sacerdotes y de todo el pueblo.
Lazima afanye upatanisho kwaajili ya mahali patakatifu sana; lazima afanye upatanisho kwaajili ya hema ya mkutano na madhabahu, na lazima afanye upatanisho kwaajili ya makuhani na kwaajili ya kusanyiko la watu.
34 Y sea para siempre una orden para ustedes, para que el pecado de los hijos de Israel se pueda quitar una vez al año. Se hizo lo que el Señor le mandó a Moisés.
Hii daima itakuwa sharti kwaajili yako, kufanya upatanisho kwaajili ya watu wa Israeli kwasababu ya dhambi zao zote, mara moja kwa kila mwaka.” Na ilikuwa ikifanika kama Yahwe alivyomwamuru Musa.

< Levítico 16 >