< Levítico 11 >

1 Y él Señor dijo a Moisés y a Aarón:
Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
2 Di a los hijos de Israel: Estos son los seres vivos que pueden tener para comer entre todas las bestias de la tierra.
“Sungumzeni na watu wa Israeli muwaambie, 'Hivi ndivyo viumbe vyenye uhai ambavyo mwaweza kula miongoni mwa wanyama walioko juu ya nchi.
3 Pueden tener como alimento a cualquier bestia que tenga pezuña partida, y rumiante cuya comida vuelva a su boca para ser aplastada nuevamente.
Mnaweza kula mnyama yeyote aliye na kwato zenye kugawanyika na ambaye pia hucheua.
4 Pero, al mismo tiempo, de esas bestias, no pueden tomar el camello por comida, porque su comida regresa pero no tiene pezuña partida; es sucio para ustedes.
Hata hivyo, kuna baadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika, nanyi msiwale hao, wanyama kama ngamia, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika. Kwa hiyo ngamia ni najisi kwenu.
5 Y el tejón de roca, por la misma razón, es impuro para ustedes.
Pimbi pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyo pia ni najisi kwenu.
6 Y la liebre, porque no tiene pezuña, es impura para ustedes.
Na sungura pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyu naye ni najisi kwenu.
7 Y el cerdo te es inmundo, porque aunque la pezuña de su pie está partido, pero no es rumiante.
Na nguruwe pia: ingawaje yeye anazo kwato zilizogawanyika lakini hacheui, kwa hiyo yeye ni najisi kwenu.
8 Su carne no puede ser usada como alimento, y sus cuerpos muertos ni siquiera pueden ser tocados; son impuros para ustedes.
Msile aina yoyote ya nyama yao, wala msiiguse mizoga yao. Hao ni najisi kwenu.
9 Estos pueden tener para comida de todas las cosas que viven en el agua: cualquier cosa que viva en el agua, en los mares o ríos, que tenga aletas y escamas, se puede usar como comida.
Nao wanyama waishio majini mnaoweza kuwala ni wale wote walio na mapezi na magamba, iwe waliomo baharini au mitoni.
10 Todas las demás cosas que viven y se mueven en el agua, en el mar o en los ríos, son una cosa desagradable para ustedes;
Lakini viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni, pamoja na wale waendao majini na viumbe hai waliomo majini —watakuwa chukizo kwenu.
11 No se pueden usar para comer, y sus cuerpos muertos despreciarás.
Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
12 Cualquier cosa en el agua que no tenga aletas o escamas lo tendrás por repugnante.
Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
13 Y entre las aves te serán repugnantes, y no se usarán para comer: el águila y él buitre y el zopilote;
Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
14 El gallinazo y el halcón, y las aves de ese tipo;
mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
15 Todo cuervo, y aves de ese tipo;
kila aina ya kunguru,
16 Y el avestruz y el gavilán y la gaviota, y las aves de ese tipo;
kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
17 Y la lechuza y el cormorán y la gran lechuza;
Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
18 Y la gallina de agua y el pelícano y el buitre;
bundi mweupe na mwari,
19 La cigüeña y la garza, y las aves de ese tipo, y la abubilla y el murciélago.
korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
20 Cada cosa de cuatro patas aladas que va sobre la tierra les será abominación;
Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
21 Pero de las cosas de cuatro patas aladas, las que tienen patas largas para saltar sobre la tierra pueden comer;
Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
22 Como todos los diferentes tipos de langosta, grillos, saltamontes.
Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
23 Pero todas las otras cosas aladas de cuatro patas que van sobre la tierra les serán abominación.
Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
24 Por esto serás inmundo; Cualquiera que toque sus cuerpos muertos será inmundo hasta la tarde:
Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
25 Quien quite el cadáver de uno de ellos, será lavado su ropa, y será inmundo hasta la tarde.
Na yeyote atakayeokota mojawapo wa mizoga yao ni lazima atazifua ngua zake naye atakuwa najisi hata jioni.
26 Toda bestia, con pezuña, pero que no tiene pezuña partida, ni rumia, es impura para ustedes: cualquiera que toque una de estas será impuro.
Mnyama yeyote ambaye anazo kwato ziliachana ambazo hazikugawanyika kabisa au hacheui huyo ni najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa najisi.
27 Cualquier bestia de cuatro patas que ande sobre sus garras, es impura; cualquiera que toque el cadáver de uno de estos será inmundo hasta la tarde.
Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
28 Cualquiera que saque el cadáver de uno de estos debe lavarse la ropa y ser inmundo hasta la tarde.
Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
29 Y estas cosas son inmundas para ustedes entre las cosas que se arrastran sobre la tierra; la comadreja y el ratón y el gran lagarto, y los animales de ese tipo;
Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
30 Y el geco, el cocodrilo de tierra y el lagarto y la lagartija, el camaleón.
kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
31 Todo esto les es inmundo: cualquiera que los toque cuando estén muertos será inmundo hasta la tarde.
Wanyama hawa wote ambao hutambaa, hawa ndiyo watakuwa najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa njisi hata jioni.
32 El cuerpo muerto de cualquiera de estos, cayendo sobre cualquier cosa, hará que esa cosa sea impura; si se trata de cualquier recipiente de madera, ropa, piel o bolsa, sea lo que sea, si se usa para cualquier propósito, se deberá poner en el agua y quedará impuro hasta la tarde; después de eso estará limpio.
Na iwapo mmoja wao anakufa na kuanguka juu ya chombo, chombo hicho kitakuwa najisi, ama kiwe kimetengenezwa kwa mbao, nguo, ngozi, au gunia. Kiwe chombo cha namna gani na kiwe kwa matumizi gani, ni lazima kitalowekwa katika maji nacho kitakuwa najisi hata jio. Kisha kitakuwa safi.
33 Y si uno de ellos se mete en cualquier recipiente de la tierra, todo lo que esté en el recipiente será inmundo y el recipiente tendrá que ser roto.
Kwa hiyo kila chungu ambacho mnyama najisi atakiangukia juu yake au ndani yake, chochote kilichomo kwenye chungu hicho kitakuwa najisi, na ni lazima mtakivunja chungu hicho.
34 Cualquier alimento que contenga, y cualquier cosa de la que provenga el agua, será inmunda: cualquier bebida que se tome de tal recipiente será inmunda.
Vyakula vyote ambavyo ni safi na kilichuhusiwa kuliwa, lakini kikaingiwa na maji kutoka kwenye chungu najisi kilichoanguka, nacho kitakuwa najisi.
35 Cualquier parte del cuerpo muerto de uno de estos, cayendo sobre cualquier cosa, lo dejará impuro; si es un horno o una olla, tendrá que romperse: están sucios y serán impuros para ustedes.
Na kitu chochote kinachoweza kunywewa kutoka kwenye chungu kama hicho kitakuwa najisi. Kila kitu kitakachoangukiwa juu yake na kipande cha mzoga wa mnyama najisi nacho kitakuwa najisi, ama liwe ni jiko au vyungu vya kupikia. Ni najisi na ni lazima kiwe najisi kwenu.
36 Pero al mismo tiempo, un manantial o una cisterna donde se almacena el agua para su uso estará limpio; pero cualquiera que toque sus cuerpos muertos será inmundo.
Chemchemi au kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika patabaki kuwa safi iwapo kiumbe najisi kama hicho kitaangukia humo. Lakini ikiwa yeyote anaugusa mzoga wa mnyama aliye najisi uliomo ndani ya maji, yeye atakuwa najisi.
37 Si alguna parte del cuerpo muerto de uno de estos entra en contacto con cualquier semilla para plantar, está limpia;
Iwapo sehehemu yoyote ya mzoga wa mnyama aliyenajisi inaangukia juu ya mbegu zozote zilizo kwa ajili ya kupanda. Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi.
38 Pero si se pone agua en la semilla, y cualquier parte del cuerpo muerto cae sobre ella, será impura para ustedes.
Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu, na kama sehemu ya mzoga unaangukia juu yake, nazo zitakuwa najisi kwenu.
39 Y si alguna bestia que pueda ser usada para comer llega a una muerte natural, cualquiera que toque su cadáver será inmundo hasta la tarde.
Iwapo mnyama yeyote awezaye kuliwa anakufa, naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni.
40 Y el que hace uso de cualquier parte de su cuerpo para comer debe lavar su ropa y ser inmundo hasta la tarde; y cualquiera que se saque su cuerpo debe lavarse la ropa y ser inmundo hasta la tarde.
Na yeyote alaye chochote cha mzoga huo atalazimika kufua nguo zake naye atakuwa anjisi hata jioni. Na yeyote aokotaye mzoga kama huo atafua nguo zake na kuwa najisi hata jioni.
41 Todo lo que se arrastra sobre su cuerpo en la tierra es asqueroso, y no debe usarse como alimento.
Kila mnyama atambaaye juu ya ardhi atakuwa chukizo; hatakuwa wa kuliwa.
42 Lo que se arrastran en su estómago o en cuatro pies o que tenga una gran cantidad de pies, incluso todos los que se quedan en la tierra, no se pueden usar como alimento, porque son asquerosos.
Chochote kitambaacho kwa kujivuta juu ya tumbo lake, na chochote kitembeacho kwa miguu yake yote minne, au chochote kilicho na miguu mingi—wanyama wote ambao hutambaa juu ya nchi, hawa msiwale, kwa sababu watakuwa machukizo.
43 Ustedes no deben contaminarse con cualquier cosa que se arrastre sobre la tierra; Ustedes no pueden hacerse impuros con ellos, de tal manera que no sean santos para mí.
Msijinajisi wenyewe kwa kiumbe chochote nnajisi kitaambacho; msijinasi wenyewe kwavyo, ili kwamba msije mkachafuliwa navyo.
44 Porque yo soy el Señor, su Dios; por este motivo, consagrense y sean santos, porque yo soy santo; Ustedes no deben hacerse impuros con ningún tipo de cosa que se arrastra sobre la tierra.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu. Nanyi lazima muwe watakatifu, kwa hiyo na iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu. Haiwapasi kujichafua kwa aina yoyote ya kiendacho juu ya nchi.
45 Porque yo soy el Señor, que te saqué de la tierra de Egipto para ser su Dios; por eso deben ser santos, porque yo soy santo.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh, aliyewaleta ninyi kutoka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo lazima muwe watakatifu, kwa kuwa Mimi ni mtakatifu.
46 Esta es la ley sobre las bestias y las aves y todo ser viviente que se mueve en las aguas, y todo ser viviente que se arrastra sobre la tierra:
Hii ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho majini, na ya kila kiumbe kitambaacho juu ya nchi,
47 Para distinguir Sobre lo impuro de lo limpio y entre los animales que puede usarse para comer y de lo que no.
kwa jili ya kilie kinachopaswa kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi, na kati ya vitu vilivyokufa na vilivyo hai ambavyo vyaweza kuliwa na vitu vyenye uihai visivyoweza kuliwa.”

< Levítico 11 >