< Levítico 11 >
1 Y él Señor dijo a Moisés y a Aarón:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
2 Di a los hijos de Israel: Estos son los seres vivos que pueden tener para comer entre todas las bestias de la tierra.
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
3 Pueden tener como alimento a cualquier bestia que tenga pezuña partida, y rumiante cuya comida vuelva a su boca para ser aplastada nuevamente.
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
4 Pero, al mismo tiempo, de esas bestias, no pueden tomar el camello por comida, porque su comida regresa pero no tiene pezuña partida; es sucio para ustedes.
“‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
5 Y el tejón de roca, por la misma razón, es impuro para ustedes.
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
6 Y la liebre, porque no tiene pezuña, es impura para ustedes.
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
7 Y el cerdo te es inmundo, porque aunque la pezuña de su pie está partido, pero no es rumiante.
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
8 Su carne no puede ser usada como alimento, y sus cuerpos muertos ni siquiera pueden ser tocados; son impuros para ustedes.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
9 Estos pueden tener para comida de todas las cosas que viven en el agua: cualquier cosa que viva en el agua, en los mares o ríos, que tenga aletas y escamas, se puede usar como comida.
“‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
10 Todas las demás cosas que viven y se mueven en el agua, en el mar o en los ríos, son una cosa desagradable para ustedes;
Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
11 No se pueden usar para comer, y sus cuerpos muertos despreciarás.
Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
12 Cualquier cosa en el agua que no tenga aletas o escamas lo tendrás por repugnante.
Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
13 Y entre las aves te serán repugnantes, y no se usarán para comer: el águila y él buitre y el zopilote;
“‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
14 El gallinazo y el halcón, y las aves de ese tipo;
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
15 Todo cuervo, y aves de ese tipo;
aina zote za kunguru,
16 Y el avestruz y el gavilán y la gaviota, y las aves de ese tipo;
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
17 Y la lechuza y el cormorán y la gran lechuza;
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
18 Y la gallina de agua y el pelícano y el buitre;
mumbi, mwari, nderi,
19 La cigüeña y la garza, y las aves de ese tipo, y la abubilla y el murciélago.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
20 Cada cosa de cuatro patas aladas que va sobre la tierra les será abominación;
“‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
21 Pero de las cosas de cuatro patas aladas, las que tienen patas largas para saltar sobre la tierra pueden comer;
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
22 Como todos los diferentes tipos de langosta, grillos, saltamontes.
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
23 Pero todas las otras cosas aladas de cuatro patas que van sobre la tierra les serán abominación.
Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
24 Por esto serás inmundo; Cualquiera que toque sus cuerpos muertos será inmundo hasta la tarde:
“‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
25 Quien quite el cadáver de uno de ellos, será lavado su ropa, y será inmundo hasta la tarde.
Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
26 Toda bestia, con pezuña, pero que no tiene pezuña partida, ni rumia, es impura para ustedes: cualquiera que toque una de estas será impuro.
“‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
27 Cualquier bestia de cuatro patas que ande sobre sus garras, es impura; cualquiera que toque el cadáver de uno de estos será inmundo hasta la tarde.
Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
28 Cualquiera que saque el cadáver de uno de estos debe lavarse la ropa y ser inmundo hasta la tarde.
Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
29 Y estas cosas son inmundas para ustedes entre las cosas que se arrastran sobre la tierra; la comadreja y el ratón y el gran lagarto, y los animales de ese tipo;
“‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
30 Y el geco, el cocodrilo de tierra y el lagarto y la lagartija, el camaleón.
guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
31 Todo esto les es inmundo: cualquiera que los toque cuando estén muertos será inmundo hasta la tarde.
Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
32 El cuerpo muerto de cualquiera de estos, cayendo sobre cualquier cosa, hará que esa cosa sea impura; si se trata de cualquier recipiente de madera, ropa, piel o bolsa, sea lo que sea, si se usa para cualquier propósito, se deberá poner en el agua y quedará impuro hasta la tarde; después de eso estará limpio.
Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
33 Y si uno de ellos se mete en cualquier recipiente de la tierra, todo lo que esté en el recipiente será inmundo y el recipiente tendrá que ser roto.
Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
34 Cualquier alimento que contenga, y cualquier cosa de la que provenga el agua, será inmunda: cualquier bebida que se tome de tal recipiente será inmunda.
Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
35 Cualquier parte del cuerpo muerto de uno de estos, cayendo sobre cualquier cosa, lo dejará impuro; si es un horno o una olla, tendrá que romperse: están sucios y serán impuros para ustedes.
Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
36 Pero al mismo tiempo, un manantial o una cisterna donde se almacena el agua para su uso estará limpio; pero cualquiera que toque sus cuerpos muertos será inmundo.
Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
37 Si alguna parte del cuerpo muerto de uno de estos entra en contacto con cualquier semilla para plantar, está limpia;
Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
38 Pero si se pone agua en la semilla, y cualquier parte del cuerpo muerto cae sobre ella, será impura para ustedes.
Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
39 Y si alguna bestia que pueda ser usada para comer llega a una muerte natural, cualquiera que toque su cadáver será inmundo hasta la tarde.
“‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
40 Y el que hace uso de cualquier parte de su cuerpo para comer debe lavar su ropa y ser inmundo hasta la tarde; y cualquiera que se saque su cuerpo debe lavarse la ropa y ser inmundo hasta la tarde.
Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41 Todo lo que se arrastra sobre su cuerpo en la tierra es asqueroso, y no debe usarse como alimento.
“‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
42 Lo que se arrastran en su estómago o en cuatro pies o que tenga una gran cantidad de pies, incluso todos los que se quedan en la tierra, no se pueden usar como alimento, porque son asquerosos.
Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
43 Ustedes no deben contaminarse con cualquier cosa que se arrastre sobre la tierra; Ustedes no pueden hacerse impuros con ellos, de tal manera que no sean santos para mí.
Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
44 Porque yo soy el Señor, su Dios; por este motivo, consagrense y sean santos, porque yo soy santo; Ustedes no deben hacerse impuros con ningún tipo de cosa que se arrastra sobre la tierra.
Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
45 Porque yo soy el Señor, que te saqué de la tierra de Egipto para ser su Dios; por eso deben ser santos, porque yo soy santo.
Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
46 Esta es la ley sobre las bestias y las aves y todo ser viviente que se mueve en las aguas, y todo ser viviente que se arrastra sobre la tierra:
“‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
47 Para distinguir Sobre lo impuro de lo limpio y entre los animales que puede usarse para comer y de lo que no.
Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”