< Josué 6 >

1 Ahora bien, Jericó estaba cerrada, asegurada para defenderla de los hijos de Israel; no salían ni entraban.
Basi malango ya Yeriko yalifungwa kwa uthabiti kwa ajili ya Waisraeli. Hakuna mtu yeyote aliyetoka au kuingia.
2 Y él Señor dijo a Josué: Mira, he entregado en tus manos a Jericó con su rey y todos sus hombres de guerra.
Kisha Bwana akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeitia Yeriko mikononi mwako, pamoja na mfalme wake na watu wake wa vita.
3 Ahora, dejen que todos sus hombres de guerra hagan un círculo alrededor de la ciudad, dando vueltas alrededor una vez. Hagan esto durante seis días.
Zunguka mji mara moja pamoja na watu wote wenye silaha. Fanya hivi kwa siku sita.
4 Y que siete sacerdotes vayan ante él cofre del pacto con siete cuernos de carnero en sus manos: en el séptimo día, debes ir por el pueblo siete veces, los sacerdotes tocarán sus cuernos.
Uwe na makuhani saba wakibeba mabaragumu ya pembe za kondoo dume mbele ya Sanduku. Siku ya saba, mzunguke mji mara saba, nao makuhani wakipiga baragumu hizo.
5 Y ante el sonido de una larga nota en los cuernos, que todos griten fuertemente; y la muralla de la ciudad se derrumbará, y toda la gente deberá avanzar.
Utakapowasikia wamepaliza sauti kubwa ya baragumu, watu wote wapige kelele kwa sauti kuu, kisha ukuta wa mji utaanguka na watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele.”
6 Entonces Josué, el hijo de Nun, mandó llamar a los sacerdotes y les dijo: Tomen él cofre del pacto y deja que siete sacerdotes tomen siete cuernos en sus manos y vayan delante del cofre del pacto el Señor.
Ndipo Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia, “Chukueni Sanduku la Agano la Bwana na makuhani saba wachukue baragumu za pembe za kondoo dume mbele yake.”
7 Y dijo a la gente: Vayan adelante, rodeen la ciudad y dejen que los hombres armados vayan delante del cofre del pacto del Señor.
Naye akawaagiza watu, “Songeni mbele! Mkauzunguke mji, na walinzi wenye silaha watangulie mbele ya Sanduku la Bwana.”
8 Entonces, después de que Josué hubo dicho esto a la gente, los siete sacerdotes con sus siete cuernos avanzaron delante del Señor, soplando sobre sus cuernos, y el cofre del pacto del Señor fue tras ellos.
Baada ya Yoshua kuzungumza na watu, wale makuhani saba wenye kuzibeba zile baragumu saba mbele za Bwana, wakatangulia mbele, wakipiga baragumu zao na Sanduku la Agano la Bwana likawafuata.
9 Y los hombres armados iban delante de los sacerdotes que estaban tocando los cuernos, y la retaguardia de la gente fue tras él cofre del pacto, mientras los sacerdotes continuaban tocando sus cuernos.
Walinzi waliokuwa na silaha wakaenda mbele ya hao makuhani waliopiga hizo baragumu na hao walinzi wa nyuma wakafuata Sanduku. Wakati wote huu baragumu zilikuwa zikipigwa.
10 Y a la gente Josué dio una orden, diciendo: No gritarán, ni harán sonido alguno, y no dejen salir ninguna palabra de su boca hasta el día en que yo diga: Griten fuerte; entonces den un grito fuerte.
Bali Yoshua alikuwa amewaagiza watu, “Msipige kelele ya vita, msipaze sauti zenu, wala kusema neno lolote mpaka siku ile nitakayowaambia mpige kelele. Ndipo mtapiga kelele!”
11 Hizo que el cofre del pacto del Señor diera una vuelta por el pueblo una vez; luego volvieron a las tiendas para pasar la noche.
Basi akalipeleka Sanduku la Bwana kuzungushwa huo mji, likizungushwa mara moja. Kisha watu wakarudi kambini kulala.
12 Y temprano en la mañana se levantó Josué, y los sacerdotes tomaron el cofre del pacto del Señor.
Yoshua akaamka mapema asubuhi iliyofuata nao makuhani wakalichukua Sanduku la Bwana.
13 Y los siete sacerdotes con sus siete cuernos continuaron delante del cofre del pacto del Señor, tocando sus cuernos; los hombres armados fueron delante de ellos, y los hombres de guerra fue tras el arca del Señor, tocando sus cuernos.
Wale Makuhani saba wakizibeba zile baragumu saba wakatangulia mbele ya Sanduku la Bwana wakizipiga. Watu wenye silaha wakatangulia mbele yao na walinzi wa nyuma wakalifuata Sanduku la Bwana, huku baragumu hizo zikiendelea kulia.
14 El segundo día marcharon alrededor del pueblo una vez, y luego regresaron a sus tiendas, y así lo hicieron durante seis días.
Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja na kurudi kambini. Wakafanya hivi kwa siku sita.
15 Al séptimo día se levantaron temprano, al amanecer del día, y marcharon alrededor de la ciudad de la misma manera, pero ese día la rodearon siete veces.
Siku ya saba, wakaamka asubuhi na mapema wakauzunguka mji kama walivyokuwa wakifanya, isipokuwa siku ile waliuzunguka mji mara saba.
16 Y la séptima vez, al sonido de los cuernos de los sacerdotes, Josué dijo a la gente: Ahora griten fuerte; porque el Señor les ha dado el pueblo.
Walipouzunguka mara ya saba, makuhani walipopiga baragumu kwa sauti kubwa, Yoshua akawaamuru watu akisema, “Pigeni kelele! Kwa maana Bwana amewapa mji huu!
17 Y el pueblo será sometido a la destrucción, y todo lo que en él se le dará al Señor: sólo Rahab, la mujer prostituta, y todos los que están en la casa con ella, se mantendrán a salvo, porque ella mantuvo el secreto los hombres que enviamos.
Mji huu pamoja na vyote vilivyomo ndani yake utawekwa wakfu kwa Bwana. Ila Rahabu tu, yule kahaba na wote ambao wako pamoja naye nyumbani mwake ndio watakaosalimishwa, kwa sababu aliwaficha wale wapelelezi tuliowatuma.
18 Y en cuanto a ustedes, manténganse alejados de ciudad que él Señor ha ordenado destruir, por temor a que puedan desearlos y tomen parte de ellos, y así sean causa de una maldición y grandes problemas en las tiendas de Israel.
Lakini mjiepushe na vitu vilivyowekwa wakfu, msije mkachukua chochote katika hivyo, msije mkajiletea maangamizi katika maskani ya Israeli na kuiletea taabu.
19 Pero toda la plata y el oro y los vasos de bronce y hierro son santos para el Señor: han de entrar en la tesorería del Señor.
Fedha yote na dhahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Bwana, lazima viletwe katika hazina yake.”
20 Entonces la gente dio un fuerte grito, y sonaron los cuernos; y al oír los cuernos, la gente dio un fuerte grito, y la pared se derrumbó, de modo que la gente subió a la ciudad, todos los hombres derecho hacia adelante, y tomaron la ciudad.
Wakati baragumu zilipopigwa, watu walipiga kelele, na katika sauti ya baragumu, na watu kupaza sauti, ukuta ukaanguka; hivyo kila mtu akapanda akiendelea mbele na kuuteka mji.
21 Y pusieron todo en el pueblo a la destrucción; Hombres y mujeres, jóvenes y viejos, bueyes y ovejas y asnos, mueren a filo de espada.
Wakauweka mji wakfu kwa Bwana, na kila chenye uhai ndani yake walikiangamiza kwa upanga, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee, ngʼombe, kondoo na punda.
22 Entonces Josué dijo a los dos hombres que habían sido enviados que hicieran una búsqueda por la tierra: Entra en la casa de la mujer prostituta y sácala, y a todos los que están con ella, como tú le diste tu juramento.
Yoshua akawaambia wale watu wawili waliokuwa wameipeleleza nchi, “Nendeni nyumbani kwa yule kahaba, mleteni pamoja na wote waliomo nyumbani mwake, kulingana na kiapo chenu kwake.”
23 Entonces los buscadores entraron y sacaron a Rahab, a su padre, a su madre, a sus hermanos y todo lo que tenía, y ellos sacaron a toda su familia; y los sacaron de las tiendas de Israel.
Basi wale vijana waliofanya upelelezi wakaenda kumleta Rahabu, baba yake na mama yake, na ndugu zake na watu wote waliokuwa pamoja naye. Wakaleta jamaa yake yote na kuwaweka mahali nje ya kambi ya Israeli.
24 Luego, después de quemar la ciudad y todo lo que había en ella, pusieron la plata y el oro y las vasijas de bronce y hierro en el almacén de la casa del Señor.
Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Bwana.
25 Pero Josué salvó la vida a Rahab, a la mujer prostituta, y a la familia de su padre y todo lo que ella tenía, y así se ganó un lugar de vida entre los hijos de Israel hasta el día de hoy; porque ella mantuvo a salvo a los hombres que Josué había enviado para hacer una búsqueda por la tierra.
Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo.
26 Entonces Josué dio órdenes al pueblo con un juramento, diciendo: Que el hombre sea maldecido ante el Señor que pone su mano en la reedificación de este pueblo: con la pérdida de su primer hijo pondrá la primera piedra de la misma en su lugar, y con la pérdida de su hijo menor, él levantará sus puertas.
Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za Bwana ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.”
27 Así que el Señor estaba con Josué; Y noticias de él fueron por toda la tierra.
Hivyo Bwana alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.

< Josué 6 >