< Juan 1 >

1 Desde el principio él era la Palabra, y la Palabra estaba con Dios y era Dios.
Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
2 Esta Palabra estaba desde el principio con Dios.
Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
3 Todas las cosas llegaron a existir a través de él, y sin él nada era.
Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
4 Lo que comenzó a existir en él fue la vida, y la vida fue la luz de los hombres.
Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
5 Y la luz sigue brillando en la oscuridad y no es vencida por la oscuridad.
Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
6 Hubo un hombre enviado por Dios, cuyo nombre era Juan.
Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
7 Él vino para dar testimonio, para dar testimonio acerca de la luz, para que todos los hombres tuvieran fe a través de él.
Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
8 Él mismo no era la luz: fue enviado a dar testimonio de la luz.
Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
9 La verdadera luz, que ilumina a cada hombre, estaba entrando en el mundo.
Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
10 Él estaba en el mundo, el mundo que surgió a través de él, pero el mundo no tenía conocimiento de él.
Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
11 Llegó a las cosas que eran suyas y su gente no lo recibió.
Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
12 Sin embargo, a todos los que lo recibieron, se les dio el derecho de convertirse en hijos de Dios, es decir, a los que tenían fe en su nombre:
Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
13 Cuyo nacimiento era de Dios y no de sangre, o de un impulso de la carne y el deseo del hombre.
Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
14 Y el Verbo se hizo carne y tomó un lugar entre nosotros por un tiempo; y vimos su gloria, la gloria que él Padre le dio a su único hijo, lleno de gracia y verdad.
Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
15 Juan dio testimonio acerca de él, y exclamó: Este es aquel de quien dije: “El que viene detrás de mí me ha sido puesto porque él existía antes que yo”.
Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
16 De su plenitud todos hemos recibido gracia sobre gracia.
Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
17 Porque la ley fue dada por medio de Moisés; la gracia y el verdadero modo de vida son nuestros a través de Jesucristo.
Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
18 Ningún hombre ha visto a Dios en ningún momento; el único Hijo, que está en íntima relación con el Padre, ha dejado en claro qué es Dios.
Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
19 Y este es el testimonio de Juan cuando los judíos enviaron sacerdotes y levitas de Jerusalén a él con la pregunta: ¿Quién eres tú?
Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
20 Dijo abiertamente y sin rodeos, yo no soy el Cristo.
Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
21 Y ellos le dijeron: ¿Qué, pues? ¿Eres Elías? Y él dijo: no. ¿Eres el profeta? Y su respuesta fue, no.
Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
22 Entonces ellos le dijeron: ¿Quién eres entonces? Tenemos que dar alguna respuesta a quienes nos enviaron. ¿Qué tienes que decir sobre ti?
Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
23 Él dijo: Yo soy la voz del que clama en el desierto, enderecen el camino del Señor, como dijo el profeta Isaías.
Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
24 Los que habían sido enviados venían de los fariseos.
Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
25 Y le hicieron esta pregunta, diciendo: ¿Por qué, pues, estás dando el bautismo si no eres el Cristo, o Elías, o el profeta?
“Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
26 La respuesta de Juan fue: doy el bautismo con agua; pero hay uno entre ustedes de quien no tienen conocimiento;
Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
27 Es él quien viene detrás de mí; No soy digno para desatar la correa de sus sandalias.
Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
28 Estas cosas tuvieron lugar en Betania, al otro lado del Jordán, donde Juan estaba dando el bautismo.
Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
29 Al día siguiente, Juan ve a Jesús acercarse a él y le dice: “Mira, aquí está el Cordero de Dios que quita el pecado del mundo”.
Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
30 Este es aquel de quien dije: Uno viene detrás de mí, quién es puesto sobre mí porque él existía antes que yo.
huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
31 Yo mismo no tenía conocimiento de él, pero vine bautizando con agua para que Israel lo viera abiertamente.
Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
32 Juan dio este testimonio, diciendo: Vi al Espíritu que descendía del cielo como una paloma y descansaba sobre él.
Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
33 No sabía quién era, pero el que me envió a bautizar con agua me dijo: Aquel sobre quien veas descender y descansar al Espíritu, es él quien da el bautismo con el Espíritu Santo.
Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
34 Yo mismo lo he visto y mi testimonio es que él es el Hijo de Dios.
Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
35 El día después, Juan estaba allí otra vez con dos de sus discípulos;
Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
36 Y mirando a Jesús mientras caminaba, dijo: ¡Mira, ahí está el Cordero de Dios!
walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
37 Al escuchar lo que dijo, los dos discípulos fueron tras Jesús.
Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
38 Y Jesús, volviéndose, los vio venir detrás de él y les dijo: ¿Qué estás buscando? Le dijeron a él, Rabino (que es decir, Maestro), ¿dónde estás viviendo?
Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
39 Él les dijo: Ven a ver. Entonces fueron con él y vieron dónde vivía; y estuvieron con él todo ese día: era alrededor de la décima hora del día.
Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
40 Andrés, el hermano de Simón Pedro, fue uno de los dos hombres que, al oír lo que Juan dijo, fue tras Jesús.
Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
41 Temprano en la mañana se encontró con su hermano y le dijo: ¡Hemos hecho un descubrimiento! ¡Es el Mesías! (es decir, el Cristo).
Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
42 Y lo llevó a Jesús. Mirándolo fijamente, Jesús dijo: Tú eres Simón, el hijo de Juan; su nombre será Cefas, (es decir, Pedro).
Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
43 El día después de esto, Jesús deseaba ir a Galilea. Se encontró con Felipe y le dijo: Ven y sé mi discípulo.
Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
44 Ahora la ciudad de Felipe era Betsaida, de donde vinieron Andrés y Pedro.
Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
45 Felipe se encontró con Natanael y le dijo: ¡Hemos hecho un descubrimiento! Es él de quien Moisés, en la ley y los profetas estaban escribiendo, Jesús de Nazaret, el hijo de José.
Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
46 ¡Nazaret! dijo Natanael: ¿es posible que algo bueno salga de Nazaret? Felipe le dijo: Ven a ver.
Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
47 Jesús vio a Natanael acercándose a él y le dijo: Mira, aquí hay un verdadero hijo de Israel en quien no hay nada falso.
Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
48 Natanael le dijo: ¿De dónde me conoces? En respuesta, Jesús dijo: Antes de que Felipe hablara contigo, mientras aún estabas debajo de la higuera, te vi.
Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
49 Natanael le dijo: Rabí, tú eres el Hijo de Dios, tú eres el Rey de Israel.
Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
50 En respuesta, Jesús le dijo: Tú tienes fe porque yo te dije, te vi debajo de la higuera. Verás cosas más grandiosas que estas.
Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
51 Y él le dijo: De cierto les digo que verán el cielo abierto y los ángeles de Dios que suben y bajan sobre el Hijo del Hombre.
Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”

< Juan 1 >