< Juan 7 >
1 Después de esto, Jesús fue de lugar en lugar en Galilea. No anduvo en Judea, porque los judíos buscaban la oportunidad de matarlo.
Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.
2 Pero la fiesta de los judíos, la fiesta de los tabernáculos, estaba cerca.
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 Entonces le dijeron sus hermanos: Vete de aquí a Judea, para que tus discípulos vean las obras que haces.
Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.
4 Porque nadie hace las cosas secretamente si desea que los hombres lo conozcan. Si haces estas cosas, déjate ver por todos los hombres.
Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”
5 Porque aun sus hermanos no creyeron en él.
Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.
6 Jesús les dijo: Mi tiempo está por venir, pero cualquier momento es bueno para ustedes.
Yesu akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.
7 No es posible que sean odiados por el mundo; pero soy soy odiado, porque doy testimonio de que lo que hacen es maldad.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu.
8 vayan a la fiesta: no voy ahora a la fiesta porque mi tiempo no ha llegado del todo.
Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”
9 Diciéndoles estas cosas, él todavía se quedó en Galilea.
Akiisha kusema hayo, akabaki Galilaya.
10 Pero después que sus hermanos fueron a la fiesta, él fue, no públicamente, sino en secreto.
Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alikwenda lakini kwa siri.
11 En la fiesta, los judíos lo buscaban y decían: ¿Dónde está?
Wayahudi walikuwa wakimtafuta huko kwenye Sikukuu na kuulizana, “Yuko wapi huyu mtu?”
12 Y hubo mucha discusión sobre él entre la gente. Algunos dijeron: Él es un buen hombre; pero otros dijeron: No, le está dando a la gente ideas falsas.
Kulikuwa na minongʼono iliyoenea kumhusu Yesu katika umati wa watu, wakati wengine wakisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walikuwa wakisema, “La, yeye anawadanganya watu.”
13 Pero ningún hombre dijo nada acerca de él abiertamente por temor a los judíos.
Lakini hakuna mtu yeyote aliyemsema waziwazi kumhusu kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
14 Ahora en medio de la fiesta, Jesús fue al Templo y estaba enseñando.
Ilipokaribia katikati ya Sikukuu, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
15 Entonces los judíos se sorprendieron y dijeron: ¿Cómo ha aprendido este hombre los libros? Él nunca ha estado en la escuela.
Wayahudi wakastaajabia mafundisho yake wakasema, “Mtu huyu amepataje kujua mambo haya bila kufundishwa?”
16 Jesús les dio esta respuesta: No es mi enseñanza, sino de aquel que me envió.
Ndipo Yesu akawajibu, “Mafundisho yangu si yangu mwenyewe, bali yanatoka kwake yeye aliyenituma.
17 Si algún hombre está listo para hacer el placer de Dios, él tendrá conocimiento de la enseñanza y de dónde proviene, de Dios o de mí mismo.
Mtu yeyote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa ajili yangu mwenyewe.
18 El hombre cuyas palabras provienen de sí mismo está buscando la gloria para sí mismo, pero el que está buscando la gloria del que le envió, ese hombre es verdadero y no hay mal en él.
Wale wanenao kwa ajili yao wenyewe hufanya hivyo kwa kutaka utukufu wao wenyewe. Lakini yeye atafutaye utukufu wa yule aliyemtuma ni wa kweli, wala hakuna uongo ndani yake.
19 ¿No te dio Moisés la ley? Aun así, ninguno de ustedes cumple la ley. ¿Por qué tienen el deseo de matarme?
Je, Mose hakuwapa ninyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja wenu anayeishika hiyo sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 Respondió el pueblo en respuesta: Tú tienes espíritu malo; ¿quién tiene deseo de matarte?
Ule umati wa watu ukamjibu, “Wewe una pepo mchafu! Ni nani anayetaka kukuua?”
21 Esta fue la respuesta de Jesús: he hecho un milagro en el dia de reposo y todos ustedes están sorprendidos.
Yesu akawajibu, “Nimefanya muujiza mmoja na nyote mkastaajabu.
22 Moisés te dio la circuncisión, no porque sea de Moisés, sino de los ancestros de ustedes, y aun en día de reposo le das la circuncisión a un niño.
Lakini kwa kuwa Mose aliwaamuru tohara (ingawa kwa kweli haikutoka kwa Mose bali kwa baba zenu wakuu), mnamtahiri mtoto hata siku ya Sabato.
23 Si a un niño se le da la circuncisión en el día de reposo para que la ley de Moisés no se rompa, ¿por qué estás enojado conmigo porque sane a un hombre en el día de reposo?
Ikiwa mtoto aweza kutahiriwa siku ya Sabato kusudi sheria ya Mose isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumponya mtu mwili wake wote siku ya Sabato?
24 No dejes que tus decisiones se basen en lo que ves, sino en la justicia.
Acheni kuhukumu mambo kwa jinsi mnavyoona tu, bali hukumuni kwa haki.”
25 Entonces algunos de los habitantes de Jerusalén dijeron: ¿No es éste el hombre que andan buscando para matarle?
Ndipo baadhi ya watu wa Yerusalemu wakawa wanasema, “Tazameni, huyu si yule mtu wanayetaka kumuua?
26 ¡ Y aquí él está hablando abiertamente y no le dicen nada! ¿Es posible que los gobernantes tengan conocimiento de que este es verdaderamente el Cristo?
Mbona yuko hapa anazungumza hadharani na wala hawamwambii neno lolote? Je, inawezekana viongozi wanafahamu kuwa huyu ndiye Kristo?
27 Sin embargo, es claro para nosotros de dónde viene este hombre, pero cuando venga Cristo, nadie sabrá de dónde viene.
Tunafahamu huyu mtu anakotoka, lakini Kristo atakapokuja, hakuna yeyote atakayejua atokako.”
28 Entonces, cuando estaba enseñando en el Templo, Jesús dijo a gran voz: Ustedes me conocen, y saben de dónde vengo; y no he venido de mí mismo; pero hay Uno que me ha enviado; él es verdadero y digno de confianza, pero ustedes no tienen conocimiento de él.
Ndipo Yesu, akaendelea kufundisha Hekaluni, akisema, “Ninyi mnanifahamu na kujua nitokako. Mimi sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, bali yeye aliyenituma ni wa kweli na ninyi hammjui.
29 Lo conozco, porque vengo de él y él me envió.
Mimi namjua kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye alinituma.”
30 Entonces tuvieron el deseo de arrestarlo, pero ningún hombre le puso las manos porque aún no había llegado su hora.
Ndipo wakatafuta kumkamata, lakini hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumshika kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijawadia.
31 Y el pueblo creyó en él, y dijeron: Cuando el Cristo venga, ¿hará más milagros de los que este hombre hizo?
Nao watu wengi wakamwamini, wakasema, “Je, Kristo atakapokuja, atafanya miujiza mikuu zaidi kuliko aliyoifanya mtu huyu?”
32 Esta discusión del pueblo llegó a los oídos de los fariseos; y los principales sacerdotes y los fariseos enviaron siervos para tomarlo.
Mafarisayo wakasikia watu wakinongʼona mambo kama hayo kuhusu Yesu, ndipo wao pamoja na viongozi wa makuhani wakatuma walinzi wa Hekalu waende kumkamata.
33 Entonces Jesús dijo: Yo estaré contigo un poco más y luego iré al que me envió.
Yesu akasema, “Mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo, kisha nitarudi kwake yeye aliyenituma.
34 Me buscarán, y no me encontraran; y donde yo esté, no podrán ir.
Mtanitafuta lakini hamtaniona, nami niliko ninyi hamwezi kuja.”
35 Entonces los judíos dijeron entre sí: ¿A dónde irá que no lo encontraremos? ¿irá a los judíos que viven entre los griegos y se convertirá en el maestro de los griegos?
Wayahudi wakaulizana wao kwa wao, “Huyu mtu anataka kwenda wapi ambako hatuwezi kumfuata? Je, anataka kwenda kwa Wayunani ambako baadhi ya watu wetu wametawanyikia, akawafundishe Wayunani?
36 ¿Qué es esta palabra suya, me buscarán y no me encontraran, y donde yo estoy, no podrán estar?
Yeye ana maana gani anaposema, ‘Mtanitafuta lakini hamtaniona,’ na, ‘nami niliko ninyi hamwezi kuja’?”
37 En el último día, el gran día de la fiesta, Jesús se levantó y dijo a gran voz: Si alguno necesita de beber, que venga a mí y beba.
Siku ile ya mwisho ya Sikukuu, siku ile kuu, wakati Yesu akiwa amesimama huko, akapaza sauti yake akasema, “Kama mtu yeyote anaona kiu na aje kwangu anywe.
38 El que tiene fe en mí, de su cuerpo, como han dicho las Escrituras, fluirán ríos de agua viva.
Yeyote aniaminiye mimi, kama Maandiko yasemavyo, vijito vya maji ya uzima vitatiririka ndani mwake.”
39 Esto lo dijo del Espíritu que se le daría a los que tenían fe en él: el Espíritu no se le había dado entonces, porque la gloria de Jesús aún estaba por venir.
Yesu aliposema haya alimaanisha Roho Mtakatifu ambaye wote waliomwamini wangempokea, kwani mpaka wakati huo, Roho alikuwa hajatolewa, kwa kuwa Yesu alikuwa bado hajatukuzwa.
40 Cuando estas palabras llegaron a sus oídos, algunas personas dijeron: Este es ciertamente el profeta.
Waliposikia maneno hayo, baadhi ya watu miongoni mwa ule umati wakasema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii.”
41 Otros dijeron: Este es el Cristo. Pero otros dijeron: No es así; vendrá el Cristo de Galilea?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine wakauliza, “Je, Kristo kwao ni Galilaya?
42 ¿No dicen las Escrituras que el Cristo viene de la simiente de David y de Belén, la pequeña ciudad donde estaba David?
Je, Maandiko hayasemi kwamba Kristo atakuja kutoka jamaa ya Daudi na kutoka Bethlehemu, mji alioishi Daudi?”
43 Entonces hubo una división entre la gente por causa de él.
Kwa hiyo watu wakagawanyika kwa ajili ya Yesu.
44 Y algunos de ellos tenían el deseo de arrestarlo; pero ningún hombre le puso las manos encima.
Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.
45 Entonces los guardianes volvieron a los principales sacerdotes y a los fariseos, y les dijo: ¿Por qué no lo trajeron con ustedes?
Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
46 Los guardianes respondieron: Ningún hombre dijo cosas como este hombre.
Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
47 Entonces los fariseos les dijeron: ¿Al igual que a los demás, se les han dado ideas falsas?
Mafarisayo wakajibu, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 ¿Alguno de los gobernantes creen en él o alguno de los fariseos?
Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
49 Pero esta gente que no conoce la ley está maldita.
Lakini huu umati wa watu wasiojua Sheria ya Mose, wamelaaniwa.”
50 Nicodemo, el que había venido a Jesús antes, siendo él mismo uno de ellos, les dijo:
Ndipo Nikodemo, yule aliyekuwa amemwendea Yesu siku moja usiku, ambaye alikuwa mmoja wao akauliza,
51 ¿Es un hombre juzgado por nuestra ley antes que le haya dado oído y tenga conocimiento de lo que ha hecho?
“Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”
52 Esta fue su respuesta: ¿y vienes de Galilea? investiga las escrituras y verás que ningún profeta sale de Galilea.
Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza nawe utaona kwamba hakuna nabii atokae Galilaya!” [
53 Y cada uno fue a su casa;
Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.