< Juan 13 >
1 Antes de la fiesta de la Pascua, estaba claro para Jesús que había llegado el momento de irse de este mundo al Padre. Después de haber amado aquellos que estaban en el mundo que eran suyos, su amor por ellos llegó hasta el final.
Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
2 Así que, mientras comía, el Maligno ya había puesto en el corazón de Judas Iscariote, hijo de Simón, para traicionarlo,
Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
3 Jesús, consciente de que el Padre había puesto todo en sus manos, y que él vino de Dios y se fue a Dios,
Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
4 se levantó de la mesa, se quitó la bata exterior, tomó un trapo y se lo puso en la cintura.
hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
5 Luego puso agua en un lebrillo y lavó los pies de los discípulos y los secó con el paño que llevaba en la cintura.
Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
6 Entonces vino a Simón Pedro. Pedro dijo: Señor, ¿son mis pies lavados por ti?
Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
7 Y Jesús, respondiendo, le dijo: Lo que yo hago no está claro para ti ahora, pero te será claro a su tiempo.
Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
8 Pedro dijo: Nunca dejaré que mis pies sean lavados por ti, nunca. Jesús dijo en respuesta: Si no te los lavo, no tienes parte conmigo. (aiōn )
Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn )
9 Simón Pedro le dijo: Señor, no sólo mis pies, sino mis manos y mi cabeza.
Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
10 Jesús le dijo: El que está recién bañado no tiene más que lavarse los pies y luego está limpio; y ustedes, mis discípulos, están limpios, pero no todos.
Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
11 Él sabía quién le iba a traicionar, por eso dijo: “No están limpios todos”.
Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
12 Luego, después de lavarse los pies y volver a ponerse la bata, se sentó y les dijo: ¿Saben lo que les he hecho?
Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
13 Ustedes me dan el nombre de Maestro y Señor; y tienen razón; eso es lo que soy.
Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
14 Si yo, el Señor y el Maestro, he limpiado sus pies, es correcto que se limpien los pies unos a otros.
Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
15 Les he dado un ejemplo, para que puedan hacer lo que les he hecho.
Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
16 De cierto os digo que un siervo no es mayor que su señor; y el enviado no es mayor que el que lo envió.
Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
17 Si estas cosas están claras para ustedes, felices son ustedes si las hacen.
Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
18 No estoy hablando de todos ustedes: yo se quienes son mis verdaderos discípulos, pero las cosas son como son, para que las Escrituras se hagan realidad, el que come el pan conmigo se ha vuelto contra mí.
“Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
19 De aquí en adelante, les digo esto de antemano antes de que sucedan, para que cuando surjan, puedan creer que yo soy él.
“Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
20 De cierto les digo, que el que recibe en su corazón a cualquiera a quien yo envíe, me lleva en su corazón; y el que me recibe a mí, recibe al que me envió.
Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
21 Cuando Jesús hubo dicho esto, se turbó en espíritu, y dio testimonio, diciendo: De cierto les digo que ninguno de ustedes me será fiel.
Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Entonces los ojos de los discípulos se volvieron el uno al otro, en la duda de a quién tenía en mente.
Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
23 Había en la mesa uno de sus discípulos, a quien Jesús amaba, que apoyaba la cabeza en el pecho de Jesús.
Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
24 Haciéndole una señal, Simón Pedro dijo: ¿De quién está hablando?
Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
25 Entonces, él, apoyando la cabeza en el pecho de Jesús, le dijo: Señor, ¿quién es?
Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
26 Esta fue la respuesta que dio Jesús: es a quien le daré este pedazo de pan después de haberlo puesto en el recipiente. Luego tomó el pedazo de pan, lo puso en el recipiente y se lo dio a Judas, el hijo de Simón Iscariote.
Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
27 Y cuando Judas tomó el pan, Satanás entró en él. Entonces Jesús le dijo: Haz lo que tienes que hacer rápidamente.
Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
28 Ahora no estaba claro para nadie en la mesa por qué le dijo esto.
Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
29 Algunos opinaron que debido a que Judas guardó la bolsa de dinero que Jesús le dijo, consiga las cosas que necesitamos para la fiesta; o, que debía dar algo a los pobres.
Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
30 Entonces Judas, que había tomado el pedazo de pan, salió de inmediato; y fue de noche.
Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
31 Entonces, cuando salió, Jesús dijo: Ahora es glorificado el Hijo del hombre, y Dios es glorificado en él.
Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32 Si a Dios se le da gloria en él, Dios le dará gloria en sí mismo, y le dará gloria ahora mismo.
Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
33 Mis queridos hijos, solo debo estar con ustedes un poco más de tiempo. Entonces me estarán buscando, y como les dije a los judíos, ahora les digo: adónde voy, es posible que no vengan.
“Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
34 Les doy un nuevo mandamiento: ámense unos a otros; así como he tenido amor por ustedes, también deben amarse unos a otros.
“Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
35 Por esto, será claro que ustedes son mis discípulos, si tienen amor el uno por el otro.
Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
36 Simón Pedro le dijo: Señor, ¿a dónde vas? Jesús dijo en respuesta: “A dónde voy, no pueden seguirme ahora, pero me seguirás después”.
Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
37 Pedro le dijo: ¿Por qué no iré contigo ahora? Daré mi vida por ti.
Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
38 Jesús dijo en respuesta: ¿Darás tu vida por mí? En verdad te digo, antes que cante un gallo habrás dicho tres veces que no eres mi discípulo.
Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”