< Job 8 >
1 Entonces Bildad el suhita respondió y dijo:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 ¿Cuánto tiempo dirás estas cosas y cuánto tiempo serán las palabras de tu boca como un viento fuerte?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 ¿Dios da decisiones equivocadas? ¿O es el Dios Todopoderoso no recto en su juicio?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 Si tus hijos hicieron lo malo contra él, entonces él los entregó a su castigo.
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 Si buscas a Dios con cuidado, y pones tu súplica ante él Dios Todopoderoso;
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 Si eres limpio y recto; entonces, ciertamente, será movido y prosperará, y tu justicia será tu morada.
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 Y aunque tu comienzo fue pequeño, tu final será muy grande.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Consulta ahora a las generaciones pasadas y presta atención a lo que han buscado sus padres:
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 Porque somos de ayer, y no tenemos conocimiento, porque nuestros días en la tierra se han ido como una sombra.
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 ¿No te darán enseñanza y sabiduría, te dirán palabras de todo corazón?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 ¿Crecerá él papiro sin pantanos? ¿Él junco crecerá sin agua?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 Sin embargo estando verde, sin ser cortado, se seca y muere antes que cualquier otra planta.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Así es el fin de todos los que no tienen a Dios en mente; y la esperanza del malvado no llega a nada:
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Cuya esperanza se corta, y cuya esperanza no es más fuerte que una telaraña.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 Él está buscando a su casa por apoyo, pero no está allí; Él pone su esperanza en su casa, pero se convierte en nada.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 Está lleno de fuerza ante el sol, y sus ramas salen por su jardín.
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 Sus raíces están retorcidas alrededor de las piedras, forzándose su camino entre ellas.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 Si lo sacan de su lugar, entonces dirá: No te he visto.
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Tal es el gozo de su camino, y del polvo otro brota para tomar su lugar.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 En verdad, Dios no renunciará al que está sin pecado, y no tomará de la mano a los que hacen el mal.
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Llegará el momento en que tu boca se llenará de risas y de tus labios saldrán gritos de alegría.
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Tus enemigos serán cubiertos de vergüenza, y la casa del pecador no volverá a ser vista.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.