< Job 6 >
1 Y Job respondió y dijo:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 ¡Si solo pudiera medirse mi pena, y ponerla en la balanza contra mi problema!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 Porque entonces su peso sería más que la arena de los mares, debido a esto mis palabras han sido cortadas.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Porque las flechas del Todopoderoso están dentro de mí, y su veneno bebe mi espíritu, su ejército de temores se pone en orden contra mí.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 ¿El asno de los campos emite su voz cuando tiene pasto? ¿O el buey hace sonidos sobre su comida?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 ¿Tomará un hombre comida que no tenga sabor sin sal? ¿O hay algún sabor en la clara del huevo?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 Mi alma no desea tales cosas, son como enfermedades en mi comida.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 ¡Si tan solo pudiera tener una respuesta a mi oración, y Dios me diera mi deseo!
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 Si solo él se complaciera en terminar conmigo; ¡Y soltaría su mano para destruirme!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Por lo tanto, todavía tendría consuelo y gozaría con los dolores de la muerte, porque siempre he respetado las palabras del Dios Santo.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 ¿Tengo fuerzas para seguir esperando o tengo algún fin para estar esperando?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 ¿Es mi fortaleza la fuerza de las piedras, o es mi carne de bronce?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 No tengo ayuda en mí mismo, y la sabiduría se me ha ido por completo.
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 El que tiene el corazón cerrado contra su amigo que sufre, ha renunciado al temor del Todopoderoso.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 Mis amigos han sido desleales como un arroyo, como arroyos en los valles que llegan a su fin.
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 Que son oscuros por el hielo y la nieve que cae en ellos;
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 Bajo el ardiente sol se secan, y no llegan a nada debido al calor.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 Las caravanas de camellos se desvían de su camino; van al vacío y son destruidos.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 Las caravanas de camellos de Tema los buscaron y de Saba, los esperaban.
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 Ellos vinieron, fueron avergonzados por su esperanza; y confundida su esperanza.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 Así son ustedes ahora; Ven mi triste condición y tienen miedo.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 ¿Dije, dame algo? o ¿Hacer un pago para mí de su riqueza?
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 ¿O me sacas del poder de mi enemigo? o ¿Dar dinero para que me rescaten del poder de los malvados?
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 Dame la enseñanza y estaré callado; Y hazme ver mi error.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 ¡Qué agradables son las palabras rectas! ¿Pero qué prueba hay en tus argumentos?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Mis palabras pueden parecer malas, pero las palabras de quien no tiene esperanza son para el viento.
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 En verdad, ustedes echarían suerte sobre un huérfano, y capaz de vender a su propio amigo.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Ahora pues, vuelvan sus ojos hacia mí, porque de verdad no diré lo que es falso en mi rostro.
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Deja que tu mente sea cambiada, y no tengas una mala opinión de mí; Sí, cambia, porque mi justicia todavía está en mí.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 ¿Hay mal en mi lengua? ¿No puede mi paladar discernir destrucción?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?