< Job 40 >

1 Continúa él Señor y dijo a Job.
Bwana akamwambia Ayubu:
2 ¿Es sabiduría discutir con él Todopoderoso? Él que reprende a Dios, dé una respuesta.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Y respondió Job en respuesta al Señor:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 En verdad, no tengo ningún valor; ¿Qué respuesta puedo darte? Pondré mi mano en mi boca.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 He dicho una vez, e incluso dos veces, lo que tenía en mente, pero no lo volveré a hacer.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Entonces el Señor respondió a Job desde él torbellino:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Reúne tus fuerzas como un hombre de guerra, te haré preguntas y tú me darás las respuestas.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 ¿Me condenarás, harás que mi juicio no tenga ningún valor? ¿Dirás que estoy equivocado para dejar en claro que tienes razón?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 ¿Tienes un brazo como Dios? ¿Tienes una voz de trueno como la de él?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Ponte los adornos de tu orgullo; vístete de gloria y poder.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Deja que tu ira se desborde; que tus ojos vean a todos los hijos del orgullo, y humíllalos.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Envía destrucción a todos los que son orgullosos, quebrantando a los impíos de sus lugares.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Sean cubiertos en el polvo; venda sus rostros en el lugar oculto.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Entonces te alabaré, diciendo que tu diestra puede darte la salvación.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Mira ahora al hipopótamo, a quien hice, como yo te hice a ti; Toma pasto para comer, como el buey.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Su fuerza está en su cuerpo, y su fuerza en los músculos de su estómago.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Su cola está curvada como un cedro; los tendones de sus piernas están entrelazados.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Sus huesos son tubos de bronce, sus piernas son como varillas de hierro.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Él es la primicia de los caminos de Dios, hecho por él, y solo él le acerque la espada.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Come de la hierba que produce las montañas, donde juegan todas las bestias del campo.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Él descansa debajo de las cañas del río, y en él pantano.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Está cubierto por las ramas de los árboles; Los álamos del arroyo están a su alrededor.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 En verdad, si el río se desborda, no le da ninguna causa para el miedo; no tiene sentido del peligro, incluso si él río Jordán está corriendo contra su boca.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Lo tomará alguien cuando esté vigilando, con trampas le perforará la nariz?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >