< Job 39 >
1 ¿Sabes cuando paren las cabras monteses? ¿Has visto a las ciervas dar a luz a sus crías?
Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
2 ¿Sabes los meses de su preñez? ¿O Sabes el momento en que van a parir?
Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
3 Se arrodillan, dan a luz a sus crías, pasan los dolores.
Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
4 Sus crías son fuertes, viven en el campo abierto; Salen y no vuelven.
Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
5 ¿Quién ha dejado libre el asno de los campos? ¿O soltó las ataduras del asno salvaje?
Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
6 A quien le he dado el desierto por morada, y la tierra estéril como lugar de vida.
ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
7 Él se burla del ruido de la ciudad; la voz del conductor no llega a sus oídos;
Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
8 Él va a buscar sus pastizales en las montañas, buscando cada cosa verde.
Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
9 ¿Será tu siervo el buey de las montañas? ¿O es el lugar de descanso de su noche en su pesebre?
Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
10 ¿Estará tirando tu arado con cuerdas, subiendo los valles detrás de ti?
Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
11 ¿Pondrás tu fe en él, porque su fuerza es grande? ¿Confiarás tu trabajo a su cuidado?
Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
12 ¿Le tendrás fe de que te devolverá tu grano, que lo recogerá del piso de trituración?
Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
13 ¿Hermosas y alegres plumas le has dado al pavo real; o alas y plumas al avestruz,
Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
14 Abandona sus huevos en el suelo, para que se incuben en el polvo.
Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
15 ¿Sin pensar que pueden ser aplastados por el pie, y destrozados por las bestias del campo?
husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
16 Es cruel con sus crías, como si no fueran de ella; su trabajo no tiene ningún propósito; ella no tiene miedo.
Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
17 Porque Dios le ha quitado sabiduría a su mente y no le ha dado ninguna medida de conocimiento.
kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
18 Cuando ella agita sus alas en lo alto, se burla del caballo y del que está sentado sobre él.
Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
19 ¿Le das fuerza al caballo? ¿Es por tu mano que su cuello está cubierto de crin?
Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
20 ¿Lo harás temblar como a un saltamontes, él vigor de su resoplido espanta?
Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
21 Él escarba en la tierra, y se alegra en su fuerza; sale al encuentro del equipo militar.
Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
22 Se burla del temor, no se acobarda y no se aleja de la espada.
Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
23 El arco suena contra él aljaba; Ve el punto brillante de lanza y el escudo.
Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
24 Temblando de pasión, él está mordiendo la tierra; no es capaz de guardar silencio ante el sonido de la bocina;
Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
25 Cuando llega a sus oídos, dice: ¡Ajá! Está oliendo la lucha desde lejos, y oyendo el trueno de los capitanes y los gritos de guerra.
Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
26 ¿Es por tu conocimiento que el halcón eleva su vuelo, extendiendo sus alas hacia el sur?
Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
27 ¿O es por tu mandato que el águila sube y hace su lugar de descanso en lo alto?
Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
28 Sobre la roca está su morada; su fortaleza, sobre la cima de la montaña allí permanece.
Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
29 Desde allí él acecha la presa; su ojo lo ve desde lejos.
Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
30 Sus polluelos se alimentan de sangre, y donde están los cuerpos muertos, allí está ella.
Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.