< Job 37 >

1 A esto me tiembla el corazón; se mueve fuera de su lugar.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Escucha el ruido de su voz; al sonido hueco que sale de su boca.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Él lo envía a través de todo el cielo, y su trueno llama hasta los confines de la tierra.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Después de esto suena una voz que truena la palabra de su poder; no retiene sus truenos; de su boca suena la voz.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Él hace maravillas, más de lo que se puede comprender; grandes cosas de las cuales no tenemos conocimiento;
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Porque dice a la nieve: Moja la tierra; Y a la tormenta de lluvia, baja.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Él pone fin a la obra de cada hombre, para que todos puedan ver su obra.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Entonces las bestias se meten en sus agujeros, y descansan.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Del sur sale el viento de tormenta y el frío del norte.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Por el aliento de Dios se hace hielo, y las anchas aguas se congelan.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 La nube espesa está cargada con una llama de trueno, y la nube emite su luz;
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Y va por este camino, dando la vuelta, girándose por su guía, para hacer lo que él ordene que se haga, en la superficie del mundo, la tierra de los hombres,
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Por corrección, o por su tierra, o por misericordia, las hará venir.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Escucha esto, oh Job, y guarda silencio en tu lugar; y toma nota de las maravillas hechas por Dios.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 ¿Tienes conocimiento del orden de Dios de sus obras, cómo hace que se vea la luz de su nube?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 ¿Tienes conocimiento como flotan las nubes, las maravillas de aquel que es perfecto en sabiduría?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Tú, cuya ropa es cálida, cuando la tierra está tranquila debido al viento del sur,
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 ¿Harás, con él, los cielos suaves y fuertes como un espejo pulido?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Dejame claro lo que debemos decirle; No podemos poner nuestra causa ante él, debido a la oscuridad.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 ¿Cómo puede él conocer mi deseo de hablar con él? ¿O algún hombre dijo alguna vez: ¿Puede la destrucción venir a mí?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Y ahora no se ve la luz, porque es oscura a causa de las nubes; Pero viene un viento que las aleja.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Una luz brillante sale del norte; La gloria de Dios es grandemente temible.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 No alcanzaremos al Todopoderoso; su fuerza y su juicio son grandes; Él está lleno de justicia, no haciendo nada malo.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Por esta causa los hombres van por temor a él; no tiene respeto por los sabios de corazón.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >