< Job 36 >

1 Y Eliu continuó diciendo:
Elihu akaendelea kusema:
2 Dame un poco más de tiempo para declarar; porque todavía tengo algo que decir en defensa de Dios.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Obtendré mi conocimiento de lejos, y le daré justicia a mi Hacedor.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Porque verdaderamente mis palabras no son falsas; Uno que es perfecto en su conocimiento está hablando contigo.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 He aquí, Dios es grande, no aborrece, es poderoso en la virtud de su corazón.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 No perdona la vida al impio, y da a los oprimidos sus derechos;
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 No apartará los ojos de los justos, hasta el trono de los reyes, los afirma para siempre, exaltandolos.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 Y si han sido encarcelados en cadenas, y cautivos en cuerdas de aflicción,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 Entonces les deja claro lo que han hecho, incluso las obras malvadas de las que se enorgullecen.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 Su oído está abierto a su enseñanza, y él les da órdenes para que sus corazones se vuelvan del mal.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 Si escuchan su voz y cumplen su palabra, entonces él les da larga vida y años llenos de placer.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 Pero si no, perecerán a espada llegan y morirán sin conocimiento.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Los que no temen a Dios mantienen la ira acumulada en sus corazones; No dan gritos de ayuda cuando son hechos prisioneros.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Llegan a su fin cuando aún son jóvenes, su vida es corta como la de aquellos que se usan con fines sexuales en la adoración de sus dioses.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 Él salva al afligido en su aflicción, abriendo sus oídos en tiempos de opresión.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 También te apartará de la boca de tus adversarios, a lugar espacioso libre de angustias; te asentará mesa llena de grosura.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Pero tú has cumplido el juicio del malvado, contra la justicia y el juicio que lo sustenta todo.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Ten cuidado que en su ira no te quite con golpe, porque ni un gran rescate te libera.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Hará él estima de tus riquezas, ni tu oro ni la potencia de tu poder.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 No anheles la noche cuando la gente asciende a su lugar.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Ten cuidado, de no volverte al pecado, porque has escogido el mal, en lugar de la miseria.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Verdaderamente Dios es excelso en su potencia; ¿Quién es un maestro como él?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 ¿Quién alguna vez le dio órdenes, o le dijo, has hecho mal?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Mira que tienes que alabar su obra, sobre el cual los hombres hacen canciones.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Todas las personas la están mirando; él hombre la ve desde lejos.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 En verdad, Dios es grande, más grande que todo nuestro conocimiento; El número de sus años no pueden ser contados.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Porque toma las gotas del mar; los envía a través de su niebla como lluvia,
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Que desciende del cielo y cae sobre los pueblos.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 ¿Y quién sabe cómo se extienden las nubes o los truenos de su tienda?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Mira, él está extendiendo su niebla, cubriendo con ella las cimas de las montañas.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Porque por éstos da comida a los pueblos, y pan en plena medida.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 con las nubes encubre la luz, y le manda no brillar, interponiendo aquéllas.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 El trueno deja en claro su pasión, y la tormenta da noticias de su ira.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.

< Job 36 >