< Job 32 >

1 Así que estos tres hombres no dieron más respuestas a Job, porque él parecía tener razón.
Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 Y Eliu, el hijo de Baraquel el Buzita, de la familia de Ram, estaba enojado, ardiendo de ira contra Job, porque se parecía a sí mismo más justo que Dios;
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 Y estaba enojado con sus tres amigos, porque no habían podido darle una respuesta, y no habían dejado claro el pecado de Job.
Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 Ahora Eliú había guardado silencio mientras Job estaba hablando, porque eran más viejos que él;
Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 Y cuando Eliu vio que no había respuesta en la boca de los tres hombres, se enojó mucho.
Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 Y Eliú, el hijo de Baraquel el Buzita, respondió y dijo: Soy joven, y tú eres muy viejo, así que tenía miedo, y evité poner mi conocimiento delante de ti.
Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 Me dije a mí mismo: que los días hablarán y que muestren su sabiduría los muchos en años.
Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 Pero en verdad es el espíritu del Todopoderoso en el hombre, lo que les da conocimiento.
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
9 No son los viejos los que son sabios, y los que están llenos de años no tienen el conocimiento de lo que es correcto.
Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 Por eso digo: “Escúchame, y expondré mi conocimiento”.
“Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
11 Esperaba tus palabras, escuchaba tus sabios dichos; mientras estabas buscando qué decir,
Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 Estaba tomando nota; y verdaderamente ninguno de ustedes pudo aclarar el error de Job, o dar una respuesta a sus palabras.
niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 Cuida de no decir: Hemos encontrado la sabiduría; Dios puede vencerlo, pero no el hombre.
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 No propondré palabras como éstas, ni haré uso de tus palabras para responderle.
Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 El miedo los ha vencido, no tienen más respuestas que dar; Han llegado a su fin.
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 ¿Y voy a seguir esperando mientras no tienen nada que decir? ¿Mientras se callan y no dan más respuestas?
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 Daré mi respuesta; Voy a presentar mis conocimientos.
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 Porque estoy lleno de palabras, el espíritu dentro de mi me constriñe.
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19 Mi estómago es como el vino que no puede salir; Como las pieles llenas de vino nuevo, casi se rompe.
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20 Déjame decir lo que tengo en mente, para que pueda consolarme; Déjame contestar con la boca abierta.
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 No permitas que respete a ningún hombre, o que le dé nombres de honor a ningún ser vivo.
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 Porque no puedo dar nombres de honor a ningún hombre; y si lo hiciera, mi Creador me llevaría rápidamente.
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.

< Job 32 >