< Job 30 >
1 Pero ahora los que son más jóvenes que yo; se burlan de mi, aquellos cuyos padres aborrecería poner con los perros de mis rebaños.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 ¿De qué sirve la fuerza de sus manos para mí? toda fuerza se ha ido de ellos.
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Se desperdician por la necesidad de comida, mordiendo la tierra seca; Su única esperanza de vida está en la tierra baldía.
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 Ellos están arrancando verdolagas de la maleza, y comían raíces de árboles.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Ellos eran rechazados de entre los habitantes de sus ciudades, los hombres gritan contra ellos como ladrones.
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 Moraban en valles de terror; Tienen que vivir en las cuevas, en los barrancos y las rocas.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Bramaban entre la maleza; Se juntan bajo las espinas.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Son hijos de vergüenza, y de hombres sin nombre, que han sido expulsados de su pueblo.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Y ahora me he convertido en su canción, y soy la burla de todos.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Les soy asqueroso; Se alejan de mí y me escupen en la cara.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Porque ha desatado el cordón de mi arco, y me ha afligido; Él los enviado y se han desenfrenado delante de mí.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 A mi diestra se levantaron los jóvenes, empujaron mis pies, se pusieron en orden y alzaron sus caminos de destrucción contra mí:
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 Han destruido mis caminos, se benefician a causa de mi destrucción; aprovechan que nadie los detiene.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 A través de un agujero en la pared como un portillo, se avalanchan contra mi.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Me ha venido él temor. Mi esperanza se ha ido como el viento, y mi bienestar como una nube.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 Pero ahora mi alma se vuelve agua en mí, me superan días de problemas.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 El dolor penetra mis huesos, y no me dieron descanso; No hay fin a mis dolores.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 Con gran fuerza desfigura mi ropa, me ciñe como cuello de mi túnica.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 En verdad, Dios me ha rebajado hasta la tierra, y me he vuelto como el polvo.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 No respondes a mi clamor, y no tomas nota de mi oración.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Te has vuelto cruel conmigo; la fuerza de tu mano me aborrece.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Levantándome, me haces ir en las alas del viento; Estoy deshecho por la tormenta.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Porque estoy seguro de que me llevarás a la muerte y al lugar de reunión ordenado para todos los vivos.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 ¿No se ha extendido mi mano para ayudar a los pobres? ¿No he sido para él un salvador en su apuro?
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 ¿No he llorado por los oprimidos? ¿Y no estaba mi alma triste por el necesitado?
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Cuando buscaba el bien, vino el mal; Estaba esperando la luz, y se oscureció.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Mis sentimientos están fuertemente conmovidos, y no me dan descanso; Los días de angustia me han sobrepasado.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Ando en ropa oscura, incómodo; Me levanto en el lugar público, pidiendo ayuda.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 Me he convertido en un hermano de los chacales, y voy en compañía de avestruces.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Mi piel es negra y se me cae; y mis huesos arden con el calor de mi enfermedad.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Y mi arpa se ha convertido en luto, y el sonido de mi flauta en el ruido de lamento.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.