< Jeremías 50 >

1 La palabra que el Señor dijo acerca de Babilonia, sobre la tierra de los caldeos, por el profeta Jeremías.
Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
2 Proclámalo entre las naciones, hazlo público y deja que se levante bandera; da la palabra y no guardes nada; digamos: Babilonia está tomada, Bel está avergonzado, Merodac está destrozado, sus imágenes son destruidas, sus dioses están quebrados.
“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
3 Porque desde el norte una nación se enfrenta a ella, lo que hará que su tierra sea arruinada y un desierto; están huyendo, el hombre y la bestia se han ido.
Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
4 En aquellos días y en ese tiempo, dice el Señor, vendrán los hijos de Israel, ellos y los hijos de Judá juntos; ellos seguirán su camino llorando y buscando al Señor su Dios.
“Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
5 Se preguntarán sobre el camino a Sión, con los rostros girados en su dirección, diciendo: Ven, y únete al Señor en un acuerdo eterno que se tendrá en cuenta para siempre.
Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
6 Mi pueblo ha sido ovejas errantes; sus pastores los han hecho ir por el camino equivocado, dejándolos sueltos en las montañas; han ido de montaña a colina, sin tener memoria de su lugar de descanso.
“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
7 Fueron atacados por todos aquellos que se cruzaron con ellos; y sus atacantes dijeron: No estamos haciendo nada malo, porque han hecho lo malo contra el Señor en quien está la justicia, contra el Señor, la esperanza de sus padres.
Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
8 Huyan de Babilonia, salgan de la tierra de los caldeos, y como los cabríos que van delante del rebaño.
“Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
9 Porque mira, me estoy moviendo y enviando a Babilonia una multitud de grandes naciones del país del norte; y pondrán sus ejércitos en posición contra ella; y de allí será tomada; sus flechas serán como las de un experto en guerra; Nadie volverá en vano.
Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
10 Y la riqueza de Caldea caerá en manos de sus atacantes; todos los que la tomen tendrán suficiente, dice el Señor.
Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
11 Porque te alegras, porque te regocijas, destruyendo mi herencia, porque juegas como una novilla, y relinchas como caballo;
“Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
12 Tu madre será avergonzada; La que te dio a luz será despreciada; mira, ella será la última de las naciones, un lugar desolado, una tierra seca y sin agua.
mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
13 Debido a la ira del Señor, nadie vivirá en ella, y estará completamente asolada; todos los que pasen por Babilonia serán asombrados, y silbará sobre todas sus plagas.
Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
14 Pon tus ejércitos en posición contra Babilonia por todos lados, todos ustedes arqueros; suelten sus flechas hacia ella, sin retroceder, porque ella ha hecho el mal contra el Señor.
“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
15 Da un grito fuerte contra ella por todos lados; ella se ha entregado a sí misma, sus cimientos están caídos, sus muros están derribados; porque esta es la venganza del Señor; tomen venganza de ella; como ella lo ha hecho, así hazle a ella.
Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
16 Que él sembrador de semillas sea destruido de Babilonia, y todos los que usen la hoz en el momento del corte de grano; por temor a la espada destructora, todos se dirigirán a su pueblo, todos huirán a su tierra.
Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
17 Israel es una oveja errante; los leones lo han dispersado; primero fue devorado por el rey de Asiria, y ahora sus huesos fueron rotos por Nabucodonosor, rey de Babilonia.
“Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
18 Esto es lo que ha dicho el Señor de los ejércitos, el Dios de Israel: Mira, enviaré castigo al rey de Babilonia y a su tierra, como lo he castigado al rey de Asiria.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
19 Haré que Israel regrese a su lugar de descanso, y pastará en Carmel y Basán, y saciará su alma extensión en las colinas de Efraín y en Galaad.
Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
20 En aquellos días y en ese tiempo, dice el Señor, cuando se busque el mal de Israel, no habrá nada; y en Judá no se verán pecados, porque tendré perdón para aquellos a quienes guardaré.
Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
21 Sube contra la tierra de Merataim, contra esta, y contra la gente de Pecod; mata y envía destrucción tras ellos, dice el Señor, y haz todo lo que te he ordenado que hagas.
“Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
22 Hay un sonido de guerra en la tierra y de gran destrucción.
Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
23 ¡Cómo ha sido cortado y quebrado el martillo de toda la tierra en dos! ¿Cómo se ha convertido Babilonia en desolación entre las naciones?
Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
24 He puesto una red para ti, y has sido tomada, oh Babilonia, sin que lo supieras; has sido encontrada y presa porque provocaste al Señor.
Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
25 Desde su almacén, el Señor ha tomado los instrumentos de su ira; porque el Señor, el Señor de los ejércitos, tiene una obra que hacer en la tierra de los caldeos.
Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
26 Ve contra ella todos y cada uno, deja que sus almacenes se abran; conviértela en una masa de piedras, destrúyela por completo, hasta que no se vea nada de ella.
Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
27 Pon todos sus bueyes a la espada; Que bajen a la muerte; el dolor es de ellos, porque ha llegado su día, el tiempo de su castigo.
Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
28 La voz de los que están huyendo, que se han escapado a salvo de la tierra de Babilonia, para dar noticias en Sion del castigo del Señor nuestro Dios, la venganza de su Templo.
Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
29 Envía a los arqueros a unirse contra Babilonia, todos los arqueros; levanten sus tiendas contra ella por todos lados; que nadie se escape; dale la recompensa de su trabajo; como ella ha hecho, así también a ella; porque ha sido exaltada de orgullo contra el Señor, contra el Santo de Israel.
“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
30 Por esta causa sus jóvenes caerán en sus calles, y todos sus hombres de guerra serán destruidos en ese día, dice el Señor.
Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
31 Mira, estoy contra ti, oh soberbio, dice el Señor, el Señor de los ejércitos, porque ha llegado tu día, el momento en que te enviaré el castigo.
“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
32 Y el soberbio irá con pasos inciertos y tendrá una caída, y no habrá nadie que venga a ayudarlo; y pondré fuego en sus pueblos, quemando todo a su alrededor.
Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
33 Esto es lo que ha dicho el Señor de los ejércitos: Los hijos de Israel y los hijos de Judá son oprimidos juntos; todos los que los tomaron prisioneros los mantienen retenidos; No los dejarán ir.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
34 Su salvador es fuerte. El Señor de los ejércitos es su nombre; ciertamente tomará su causa, para que pueda dar descanso a la tierra y problemas a la gente de Babilonia.
Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
35 Hay una espada en los caldeos, dice el Señor, y en el pueblo de Babilonia, en sus gobernantes y en sus sabios.
“Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
36 Hay una espada contra los adivinos, y se volverán tontos; una espada contra sus hombres de guerra, y serán quebrantados.
Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
37 Hay una espada sobre todos los extranjeros que hay en ella, y se volverán como mujeres; una espada sobre sus almacenes, y serán tomados por sus atacantes.
Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
38 Una espada está sobre sus aguas, secándolas; porque es una tierra de imágenes, y se vuelven locos por dioses falsos.
Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
39 Por esta razón, las bestias de la tierra baldía con los lobos harán sus agujeros allí y los avestruces vivirán en ella; nunca más los hombres vivirán allí, será poblada de generación en generación.
“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
40 Como cuando Sodoma y Gomorra y sus pueblos vecinos fueron derrocados por Dios, dice el Señor, así ningún hombre vivirá en ella, y ningún hijo de hombre tendrá un lugar de descanso allí.
Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
41 Mira, viene un pueblo del norte; una gran nación y una serie de reyes serán puestos en movimiento desde las partes más internas de la tierra.
“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
42 Arcos y lanzas están en sus manos; son crueles y no tienen piedad; su voz es como el trueno del mar, y van sobre caballos; Todos en su lugar, como hombres que van a pelear, contra ti, hija de Babilonia.
Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
43 El rey de Babilonia ha tenido noticias de ellos, y sus manos se han debilitado; le han llegado problemas y dolor como el dolor de una mujer en el parto.
Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
44 Mira, él subirá como un león desde el espeso crecimiento del Jordán contra el lugar de descanso de Temán; pero de repente los haré huir de ella; y pondré sobre ella al hombre de mi elección, ¿quién es como yo? ¿Y quién presentará su causa contra mí? ¿Y qué guardián de ovejas mantendrá su lugar delante de mí?
Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
45 Escuchen la decisión del Señor que tomó contra Babilonia, y sus propósitos diseñados contra la tierra de los caldeos; En verdad, serán arrastrados por el rebaño más pequeño; En verdad, hará desperdiciar sus campos con ellos.
Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
46 Al grito, ¡Babilonia es tomada! la tierra tiembla, y el clamor llega a los oídos de las naciones.
Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.

< Jeremías 50 >