< Jeremías 49 >
1 Sobre los hijos de Amón. Estas son las palabras del Señor: ¿Israel no tiene hijos? ¿No tiene el heredero? ¿Por qué, entonces, Milcom ha tomado a Gad para sí mismo, poniendo a su gente en sus pueblos?
Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
2 Debido a esto, mira, vienen los días en que sonará un grito de guerra contra Raba, la ciudad de los hijos de Amón; se convertirá en un montón de muros rotos, y sus ciudades serán quemadas con fuego; entonces Israel tomará la herencia de aquellos que tomaron su herencia, dice el Señor.
Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
3 Gime, oh Hesbón, porque Ahí ha sido destruido; clamen, oh hijas de Rabá, y ustedes vístanse de silicio; entréguense a llorar, corran por aquí y por allá entre los muros; porque Milcom será hecho prisionero junto con sus gobernantes y sus sacerdotes.
Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
4 ¿Por qué te enorgulleces a causa de tus valles, de tu valle que fluye, oh hija que te apartas? ¿Quién pone su fe en su riqueza, diciendo: ¿Quién vendrá contra mí?
Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
5 Mira, te enviaré miedo, dice el Señor, el Señor de los ejércitos, de los que te rodean por todos lados; serás forzado a salir, cada hombre saldrá corriendo por su lado, y no habrá nadie para reunir a los errantes.
Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
6 Pero después de estas cosas, dejaré que cambie el destino de los hijos de Amón, dice el Señor.
Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
7 Sobre Edom. Esto es lo que ha dicho el señor de los ejércitos. ¿No hay más sabiduría en Teman? ¿Han terminado las sabias sugerencias entre los hombres de buen sentido? ¿Su sabiduría se ha corrompido?
Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
8 Ve en vuelo, regresa, busca refugio en lugares profundos, tú que vives en Dedán; porque le enviaré el quebrantamiento de Esaú, ha llegado el momento de su castigo.
Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
9 Si los hombres vinieran a recoger tus uvas, ¿no dejarían racimos? Si los ladrones vinieran de noche, ¿no harían desperdicio hasta que tuvieran suficiente?
Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
10 He despojado a Esaú, descubriendo sus lugares secretos, para que no se mantenga escondido; su descendencia, parientes y amigos, fueron destruidos y él ya no existe.
Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
11 Pon a mi cuidado a tus hijos que no tienen padre, y los mantendré a salvo; y que tus viudas pongan su fe en mí.
Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
12 Porque el Señor ha dicho: Aquellos para quienes no se preparó la copa ciertamente se verán obligados a tomarla; ¿Y vas a ir sin castigo? no estarás sin castigo, pero ciertamente serás obligado a tomar de la copa.
Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
13 Porque yo mismo he jurado, dice el Señor, que Bosra se convertirá en una causa de asombro, un nombre de vergüenza, un espanto y una maldición; y todos sus pueblos serán lugares desolados para siempre.
Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
14 Me han llegado noticias del Señor y un representante ha sido enviado a las naciones para decir: “Vengan juntos, suban contra ella y ocupen sus lugares para la lucha”.
Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
15 Porque mira, te he hecho pequeño entre las naciones, despreciado por los hombres.
“Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
16 El orgullo de tu corazón ha sido una falsa esperanza, oh tú, que estás viviendo en las grietas de la roca, manteniendo tu lugar en la cima de la colina; incluso si hiciste tu lugar de vida tan alto Como el águila, te haría bajar, dice el Señor.
Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
17 Y Edom se convertirá en un motivo de asombro; todos los que pasen serán asombrados, y emitirán sonidos de miedo al ver su castigos.
Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
18 Como en la caída de Sodoma y Gomorra y sus pueblos vecinos, dice el Señor, ningún hombre vivirá en ella, ningún hijo del hombre tendrá un lugar de descanso allí.
Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
19 Mira, él subirá como un león desde el espeso crecimiento del Jordán contra el lugar de descanso de Teman; pero de repente lo haré huir de ella; y pondré sobre ella al hombre de mi elección. ¿quién es como yo? ¿Y quién presentará su causa contra mí? ¿Y qué guardián de ovejas podrá mantener su lugar delante de mí?
Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
20 Por esta causa, escuche la decisión que el Señor, tomó contra Edom y sus propósitos diseñados contra la gente de Teman. En verdad, serán arrastrados hasta el rebaño más pequeño; En verdad, destruirán sus pastizales.
Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
21 La tierra tiembla con el ruido de su caída; Su llanto está sonando en el mar rojo.
Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
22 Mira, él subirá como un águila en vuelo, extendiendo sus alas contra Bosra: y los corazones de los hombres de guerra de Edom en ese día serán como el corazón de una mujer de parto.
Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
23 Mensaje sobre Damasco. Hamat es avergonzado, y Arpad; porque la palabra del mal ha llegado a sus oídos, su corazón en su temor se convierte como el mar que no se puede calmar.
Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
24 Damasco se ha debilitado, se ha convertido en un fugitivo, el miedo la ha agarrado; el dolor y las penas le han afectado, como a una mujer en los dolores de parto.
Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
25 Cómo se ha dejado el pueblo de alabanza, el lugar de la alegría.
Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
26 Entonces sus jóvenes caerán tendidos en sus calles, y todos los hombres de guerra morirán en ese día, dice el Señor de los ejércitos.
Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
27 Y prenderé fuego la pared de Damasco, quemando las grandes casas de Ben-adad.
“Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
28 Sobre Cedar y los reinos de Hazor, que Nabucodonosor, rey de Babilonia, venció. Esto es lo que el Señor ha dicho: ¡Arriba! Ve contra Cedar y ataca a los hijos del este.
Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
29 Tomarán sus tiendas y sus rebaños; quitarán para sí sus cortinas y todos sus utensilios, sus camellos; les gritarán: Hay terror por todos lados.
Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
30 Vete en vuelo, vaga lejos, escápate en lugares lejanos, oh pueblo de Hazor, dice el Señor; porque Nabucodonosor, rey de Babilonia, ha hecho un plan contra ti, tiene un propósito contra ti en mente.
Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
31 Levántate. Vayan contra una nación que vive cómodamente y sin temor al peligro, dice el Señor, sin puertas ni cerraduras, viviendo solo.
Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
32 Y sus camellos serán quitados de ellos por la fuerza, y sus grandes manadas vendrán a las manos de sus atacantes; a los que tienen cortados los cabos, los enviaré en vuelo a todos los rincones; y les enviaré su destrucción desde todos lados, dice el Señor.
Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
33 Y Hazor será un agujero para los chacales, un desierto para siempre; nadie vivirá en él, y ningún hijo de hombre tendrá un lugar de descanso allí.
Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
34 La palabra del Señor que vino a Jeremías profeta acerca de Elam, cuando Sedequías se convirtió por primera vez en rey de Judá, diciendo:
Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
35 Esto es lo que ha dicho el Señor de los ejércitos: Mira, tendré el arco de Elam, su fuerza principal, rota.
“Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
36 Y enviaré a Elam cuatro vientos de las cuatro cuartas partes del cielo, llevándolos a todos esos vientos; No habrá ninguna nación a la que no lleguen los errantes de Elam.
Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
37 Y permitiré que Elam tiemble ante sus enemigos, y ante aquellos que están haciendo planes contra sus vidas; Enviaré el mal sobre ellos, incluso mi ira ardiente, dice el Señor; y les enviaré la espada hasta que acabe con ellos.
Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
38 Pondré la sede de mi poder en Elam, y en Elam acabaré con los reyes y gobernantes, dice el Señor.
Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
39 Pero sucederá que, en los últimos días, dejaré que cambie el destino de Elam, dice el Señor.
na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”