< Jeremías 20 >
1 Llegó a oídos de Pasur, el hijo del sacerdote Imer, jefe de autoridad en la casa del Señor, que Jeremías estaba diciendo estas cosas;
Ikawa kuhani Pashuri mwana wa Imeri, mkuu wa maafisa wa Hekalu la Bwana, alipomsikia Yeremia akitoa unabii juu ya mambo haya,
2 Y Pasur le hizo azotar a Jeremías y le encadenaron los pies en un marco de madera en la entrada superior de Benjamín, que estaba en la casa del Señor.
akaamuru Yeremia nabii apigwe na kufungwa kwenye mkatale katika Lango la Juu la Benyamini huko Hekaluni la Bwana.
3 Y al día siguiente, Pasur soltó a Jeremías. Entonces Jeremías le dijo: El Señor te ha dado el nombre de Magor-misabib (Causa del miedo en todas partes), no Pasur.
Siku ya pili Pashuri alipomwachia kutoka kwenye mkatale, Yeremia akamwambia, “Bwana hakukuita jina lako kuwa Pashuri bali Magor-Misabibu.
4 Porque el Señor ha dicho: Mira, te haré una causa de temor para ti y para todos tus amigos: ellos morirán por la espada de sus enemigos, y tus ojos lo verán; y entregaré a todo Judá en manos del rey de Babilonia, y él los llevará a los prisioneros a Babilonia y los pondrá a la espada.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitakufanya kuwa hofu kuu kwako wewe mwenyewe na rafiki zako wote, na kwa macho yako mwenyewe utawaona wakianguka kwa upanga wa adui zao. Nitawatia Yuda wote mikononi mwa mfalme wa Babeli, ambaye atawachukua na kuwapeleka Babeli, ama awaue kwa upanga.
5 Y más que esto, daré toda la riqueza de esta ciudad y todos sus beneficios y todas sus cosas de valor, incluso todas las tiendas de los reyes de Judá entregaré en manos de sus enemigos, quienes los tomarán y llevarán a Babilonia.
Nitatia utajiri wote wa mji huu kwa adui zao: yaani mazao yao yote, vitu vyao vyote vya thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda. Watavitwaa kwa nyara na kuvipeleka Babeli.
6 Y tú, Pasur, y todos los que están en tu casa, se irán prisioneros; vendrás a Babilonia y allí morirás y serás enterrado, tú y todos tus amigos, a quienes has profetizado palabras falsas.
Nawe Pashuri pamoja na wote waishio katika nyumba yako mtakwenda uhamishoni Babeli. Mtafia humo na kuzikwa, wewe na rafiki zako wote ambao umewatabiria uongo.’”
7 Señor, tú me has persuadido, y me deje persuadir; eres más fuerte que yo, y me has superado; me he vuelto objeto de risa todo el día, todos me hacen burla.
Ee Bwana, umenidanganya, nami nikadanganyika; wewe una nguvu kuniliko, nawe umenishinda. Ninadharauliwa mchana kutwa, kila mmoja ananidhihaki.
8 Porque cada palabra que digo; Digo con voz fuerte: violencia y destrucción; porque la palabra del Señor ha venido a ser una afrenta para mí y una causa de burla todo el día.
Kila ninenapo, ninapiga kelele nikitangaza ukatili na uharibifu. Kwa hiyo neno la Bwana limeniletea matukano na mashutumu mchana kutwa.
9 Y si digo, no lo tendré en cuenta, no diré otra palabra en su nombre; entonces está en mi corazón como un fuego ardiente encerrado en mis huesos, trato de contenerla dentro, y no puedo hacerlo.
Lakini kama nikisema, “Sitamtaja wala kusema tena kwa jina lake,” neno lake linawaka ndani ya moyo wangu kama moto, moto uliofungwa ndani ya mifupa yangu. Nimechoka sana kwa kulizuia ndani mwangu; kweli, siwezi kujizuia.
10 Porque muchos de ellos dicen mal en secreto a mis oídos (hay temor por todos lados): dicen: Vengan, vamos acusarlo; todos mis amigos más cercanos, que están a la espera de mi caída, dicen: Puede ser que lo engañen, y lo sacaremos de encima y le daremos un castigo.
Ninasikia minongʼono mingi, “Hofu iko pande zote! Mshtakini! Twendeni tumshtaki!” Rafiki zangu wote wananisubiri niteleze, wakisema, “Labda atadanganyika; kisha tutamshinda na kulipiza kisasi juu yake.”
11 Pero el Señor está conmigo como un guerrero invencible, para ser temido grandemente; así mis atacantes caerán, y no me vencerán; serán avergonzados grandemente, pues no han triunfado, con afrenta perpetua porque nunca será olvidada.
Lakini Bwana yu pamoja nami kama shujaa mwenye nguvu; hivyo washtaki wangu watajikwaa na kamwe hawatashinda. Watashindwa, nao wataaibika kabisa; kukosa adabu kwao hakutasahauliwa.
12 Pero, oh Señor de los ejércitos, probando a los rectos y viendo los pensamientos y el corazón, déjame ver que tu castigo venga sobre ellos; porque yo he puesto mi causa delante de ti.
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe umjaribuye mwenye haki na kupima moyo na nia, hebu nione ukilipiza kisasi juu yao, kwa maana kwako nimeliweka shauri langu.
13 Haz melodía al Señor, alaba al Señor, porque ha liberado el alma del pobre de las manos de los malvados.
Mwimbieni Bwana! Mpeni Bwana sifa! Yeye huokoa uhai wa mhitaji kutoka mikononi mwa waovu.
14 Una maldición el día de mi nacimiento; que no haya bendiciones el día en que mi madre me tuvo.
Ilaaniwe siku niliyozaliwa! Nayo isibarikiwe ile siku mama yangu aliyonizaa!
15 Una maldición sobre el hombre que le dio la noticia a mi padre, diciendo: Tú tienes un hijo varón; haciéndolo muy alegre.
Alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, yule aliyemfanya afurahi sana, akisema, “Mtoto amezaliwa kwako, tena mtoto wa kiume!”
16 Que ese hombre sea como las ciudades derrocadas por el Señor sin piedad; que a la mañana llegue a sus oídos un clamor de auxilio, y alaridos al medio del día;
Mtu huyo na awe kama miji ile ambayo Bwana Mungu aliiangamiza bila huruma. Yeye na asikie maombolezo asubuhi na kilio cha vita adhuhuri.
17 Porque no me mató antes de que naciera, así, el cuerpo de mi madre habría sido mi tumba y ella habría estado embarazada para siempre.
Kwa sababu hakuniua nikiwa tumboni, hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, nalo tumbo lake la uzazi lingebaki kuwa kubwa daima.
18 ¿Por qué salí del cuerpo de mi madre para ver aflicción y problemas, para que mis días se desperdicien en vergüenza?
Kwa nini basi nilitoka tumboni ili kuona taabu na huzuni, na kuzimaliza siku zangu katika aibu?