< Isaías 7 >
1 Aconteció en los días de Acaz, hijo de Jotam, hijo de Uzías, rey de Judá, que llegaron Rezín, rey de Aram, y Peka, hijo de Remalías, rey de Israel. Hasta Jerusalén para hacer la guerra contra ella, pero no pudieron vencerla.
Wakati Ahazi mwana wa Yothamu, mwana wa Uzia, alipokuwa mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipanda kupigana dhidi ya Yerusalemu, lakini hawakuweza kuushinda.
2 Y llegó a la familia de David la noticia de que Aram había levantado sus tiendas en Efraín. Y el corazón del rey y los corazones de su pueblo se conmovieron, como los árboles del bosque temblando en el viento.
Wakati huu nyumba ya Daudi iliambiwa, “Aramu wameungana na Efraimu.” Kwa hiyo mioyo ya Ahazi na watu wake ilitikiswa, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.
3 Entonces el Señor le dijo a Isaías: Sal ahora, tú y Sear-jasub, tu hijo, y te encontrarás con Acaz al final de la corriente que fluye desde el estanque más alto, en la carretera del campo del lavandero;
Ndipo Bwana akamwambia Isaya, “Toka uende, wewe na mwanao Shear-Yashubu, mkutane na Ahazi huko mwisho wa mfereji wa Bwawa la Juu, kwenye barabara iendayo Shamba la Dobi.
4 Y dile: Cuídate y ten calma; no temas, y no dejes que tu corazón se debilite, debido a estos dos carbones humeantes, debido a la amarga ira de Rezín y Aram, y del hijo de Remalías.
Mwambie, ‘Uwe mwangalifu, utulie na usiogope. Usife moyo kwa ajili ya watu hawa wawili walio kama visiki vya kuni vifukavyo moshi, kwa ajili ya hasira kali ya Resini na Aramu na ya mwana wa Remalia.
5 Porque Aram ha tramado mal contra ti, diciendo:
Aramu, Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga shauri baya ili wakuangamize, wakisema,
6 Subamos contra Judá a invadir y aterroricemosla, y pongamos en ella un rey, el hijo de Tabeel.
“Tuishambulie Yuda, naam, tuirarue vipande vipande na kuigawa miongoni mwetu, na kumtawaza mwana wa Tabeeli awe mfalme juu yake.”
7 Esta es la palabra del Señor Dios: Esto jamas se realizará.
Lakini Bwana Mwenyezi asema hivi: “‘Jambo hili halitatendeka, halitatokea,
8 Porque la cabeza de Aram es Damasco, y la cabeza de Damasco es Rezín y dentro de sesenta y cinco años desde ahora, Efraín será quebrantado, y ya no será un pueblo:
kwa kuwa kichwa cha Aramu ni Dameski, na kichwa cha Dameski ni Resini peke yake. Katika muda wa miaka sitini na mitano, Efraimu atakuwa ameharibiwa kiasi kwamba hataweza tena kuwa taifa.
9 Y la cabeza de Efraín es Samaria, y la cabeza de Samaria es el hijo de Remalías. Si no lo creen, tu reino no permanecerá.
Kichwa cha Efraimu ni Samaria, na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia peke yake. Kama hamtasimama thabiti katika imani yenu, hamtaimarika kamwe.’”
10 Entonces Isaías volvió a decir a Acaz:
Bwana akasema na Ahazi tena,
11 Pide al Señor tu Dios una señal, una señal en los lugares profundos del inframundo o en los cielos altos. (Sheol )
“Mwombe Bwana Mungu wako ishara, iwe kwenye vina virefu sana, au kwenye vimo virefu sana.” (Sheol )
12 Pero Acaz dijo: No pondré a prueba al Señor haciendo tal petición.
Lakini Ahazi akasema, “Sitaomba; sitamjaribu Bwana.”
13 Y él dijo: Escucha ahora, oh familia de David: ¿no es suficiente que estés llevando a los hombres al disgusto? ¿Harás lo mismo con mi Dios?
Ndipo Isaya akasema, “Sikia sasa, ewe nyumba ya Daudi! Je, haitoshi kujaribu uvumilivu wa wanadamu? Je, mtaujaribu uvumilivu wa Mungu wangu pia?
14 Por esta causa, el mismo Señor te dará una señal; una joven ahora está embarazada, y ella dará a luz un hijo, y ella le dará el nombre de Emanuel.
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara: Bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, na ataitwa Imanueli.
15 La cuajada y la miel serán su alimento, cuando tenga la edad suficiente para tomar una decisión entre el mal y el bien.
Atakula jibini na asali atakapokuwa ameweza kukataa mabaya na kuchagua mema.
16 Porque antes de que el niño tenga la edad suficiente para tomar una decisión entre el mal y el bien, la tierra cuyos dos reyes que ahora temen se habrá convertido en un desperdicio.
Lakini kabla mtoto hajajua kukataa mabaya na kuchagua mema, nchi ya wafalme hao wawili unaowaogopa itafanywa ukiwa.
17 El Señor está a punto de enviarte a ti, a tu pueblo y a la casa de tu padre, un tiempo de angustia que no ha habido desde los días de la separación de Efraín de Judá; Incluso la venida del rey de Asiria.
Bwana ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuwako tangu Efraimu alipojitenga na Yuda: yeye atawaleteeni mfalme wa Ashuru.”
18 Y será en ese día que el Señor hará un sonido para la mosca que está al final de los ríos de Egipto, y para la abeja que está en la tierra de Asiria.
Katika siku ile Bwana atawapigia filimbi mainzi kutoka vijito vya mbali vya Misri, na nyuki kutoka nchi ya Ashuru.
19 Y vendrán, cubriendo todos los valles desolados, y los agujeros de las rocas, y las espinas, y todos los lugares de riego.
Wote watakuja na kukaa kwenye mabonde yenye miteremko, na kwenye nyufa za miamba, kwenye vichaka vyote vyenye miiba, na kwenye mashimo yote ya maji.
20 En ese día, el Señor rasurara el pelo de la cabeza y de los pies, así como el pelo de la cara, con una cuchilla alquilada del otro lado del río; con el rey de Asiria.
Katika siku ile Bwana atatumia wembe ulioajiriwa kutoka ngʼambo ya Mto, yaani mfalme wa Ashuru, kunyoa nywele za kichwa chako na malaika ya miguu yako, na kuziondoa ndevu zako pia.
21 Y será en ese día que un hombre dará comida a una vaca joven y dos ovejas;
Katika siku ile, mtu atahifadhi hai ndama mmoja na kondoo wawili.
22 Y darán tanta leche que él podrá tener cuajada para su comida; porque la cuajada y la miel serán la comida de todos los que aún viven en la tierra.
Kwa ajili ya wingi wa maziwa watakayotoa, atapata jibini ya kula. Wote watakaobakia katika nchi watakula jibini na asali.
23 Y será en ese día que en todos los lugares donde antes había mil vides valoradas en mil siclos de plata, no habrá más que maleza y espinas.
Katika siku ile, kila mahali palipokuwa na mizabibu elfu moja yenye thamani ya shekeli 1,000 za fedha, patakuwa na michongoma na miiba tu.
24 Los hombres vendrán allí con arcos y flechas, porque toda la tierra estará llena de maleza y espinos.
Watu watakwenda huko wakiwa na upinde na mshale, kwa maana nchi itafunikwa na michongoma na miiba.
25 Y enviarán los bueyes y las ovejas a todas las colinas que antes se trabajaban con azadón, porque solo es espinos y maleza y servirán solo para pastizales.
Kuhusu vilima vyote vilivyokuwa vikilimwa kwa jembe, hamtakwenda huko tena kwa ajili ya hofu ya michongoma na miiba. Patakuwa mahali ambapo ngʼombe wataachiwa huru, na kondoo kukimbia kimbia.