< Hebreos 13 >
1 Continúa amando a tus hermanos en la fe.
Endeleeni kupendana kama ndugu.
2 Cuídate de mantener la casa abierta: porque de esta manera algunos han tenido ángeles como invitados, sin ser conscientes de ello.
Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
3 Tenga en cuenta a los que están encadenados, como si estuvieran encadenados con ellos, y aquellos que son maltratados, como si estuvieran ustedes mismos en el cuerpo.
Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
4 Que la vida matrimonial sea honrada entre todos ustedes y no mancillar el lecho matrimonial; porque a los fornicarios y adúlteros serán juzgados por Dios.
Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
5 Libérate del amor al dinero y complacete con las cosas que tienes; porque él mismo dijo: Yo estaré contigo en todo momento, no te desampararé.
Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
6 Para que podamos decir confiadamente: El Señor es mi ayudador; No tendré miedo: ¿lo que me pueda hacer el hombre?
Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
7 Tengan en cuenta a los que estaban sobre ustedes, y que les hablaron de la palabra de Dios; viendo el resultado de su forma de vida, dejen que su fe sea como la de ellos.
Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
8 Jesucristo es el mismo ayer, hoy y siempre. (aiōn )
Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn )
9 No se dejen llevar por diferentes enseñanzas extrañas, porque es bueno que sus corazones sean fortalecidos por él amor de Dios, y en seguir reglas de alimentos, que no fueron de provecho para aquellos que se preocuparon tanto por eso.
Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
10 Tenemos un altar del cual los sacerdotes que están en el santuario no pueden comer.
Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
11 Porque los cuerpos de las bestias cuya sangre es llevada al lugar santo por el sumo sacerdote como una ofrenda por el pecado son quemados fuera del círculo del santuario.
Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12 Por esta razón, Jesús fue ejecutado fuera de las murallas, para que el pueblo se santificara con su sangre.
Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
13 Salgamos a él fuera del círculo del santuario llevando su vergüenza.
Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
14 Porque aquí no tenemos un lugar de descanso fijo, pero buscamos la que está por venir.
Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
15 Hagamos, pues, ofrendas de alabanza a Dios en todo momento por medio de él, es decir, el fruto de los labios que dan testimonio de su nombre.
Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
16 Pero sigan haciendo el bien y dándoles a los demás, porque Dios está complacido con tales ofrendas.
Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
17 Obedezcan a sus a sus líderes, y sujétense a ellos: porque guardan sus almas, dispuestos a dar cuenta de ellos; permitirles hacer esto con alegría y no quejándose, porque eso no sería beneficioso para ustedes.
Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18 Haz oraciones por nosotros, porque estamos seguros de que nuestros corazones están libres del sentido del pecado, deseando la forma correcta de vida en todas las cosas.
Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
19 Hago esta solicitud con más fuerza, con la esperanza de volver a ustedes más rápidamente.
Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
20 Ahora bien, el Dios de la paz, que resucitó de los muertos a nuestro Señor Jesucristo el gran pastor de su rebaño, a través de la sangre del eterno pacto, (aiōnios )
Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios )
21 Los haga aptos en todo buen trabajo y listo para hacer todos sus deseos trabajando en ustedes lo que es agradable a sus ojos a través de Jesucristo; y que la gloria le sea dada por los siglos de los siglos. Que así sea. (aiōn )
awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
22 Pero, hermanos, toma amablemente las palabras que he dicho para tu ganancia; porque no les he enviado una carta larga.
Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
23 Nuestro hermano Timoteo ha sido liberado de la prisión; y si viene aquí en poco tiempo, él y yo vendremos a ti juntos.
Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
24 Saludos a todos a los pastores, y a todos los santos. Los que están en Italia los saludan.
Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
25 La gracia sea con todos ustedes. Amén.
Neema iwe nanyi nyote. Amen.