< Hebreos 11 >

1 Ahora bien, la fe es la sustancia de lo que se espera, y la evidencia de que las cosas que no se ven son verdad.
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, na udhahiri wa mambo yasiyoonekana.
2 Porque por eso nuestros antepasados tuvieron la aprobación de Dios.
Maana baba zetu wa kale walipongezwa kwa haya.
3 Por la fe, nosotros entendemos que el orden de los mundos los formó mediante la palabra de Dios, de modo que lo que se ve, se ha hecho de las cosas que no se ven. (aiōn g165)
Kwa imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, vitu vyote vinavyoonekana havikuumbwa kutoka kwa vitu vinavyoonekana. (aiōn g165)
4 Por la fe Abel hizo una mejor ofrenda a Dios que Caín, y atestigua por medio de ella su justicia, dando Dios su aprobación de su ofrenda; y su voz aún nos llega a través de ella aunque él esté muerto.
Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu bora zaidi kuliko Kaini. Kwa imani alishuhudiwa kuwa mwenye haki, Mungu mwenyewe akazishuhudia sadaka zake. Kwa imani bado ananena ingawa amekufa.
5 Por la fe, Enoc fue llevado al cielo para que no viera la muerte; no se le vio más, porque Dios se lo llevó; porque antes de ser tomado, se le había dado testimonio de que agradaba mucho a Dios:
Kwa imani Enoki alitwaliwa kutoka maisha haya, kiasi kwamba hakuonja mauti. Hakuonekana, kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Kwa kuwa kabla hajatwaliwa alikuwa ameshuhudiwa kuwa ni mtu aliyempendeza Mungu.
6 Y sin fe no es posible agradar a Dios, porque es Es necesario para cualquiera que acuda a Dios tener la creencia de que Dios es, y que él es galardonador de todos aquellos que lo buscan con diligencia.
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana yeyote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.
7 Por la fe, Noé, movido por el temor de Dios, preparó un arca para la salvación de su familia, porque Dios le había dado noticias de cosas que no se habían visto en ese momento; y por medio de él el mundo fue juzgado por él, y obtuvo para su herencia la justicia que es por fe.
Kwa imani, Noa alipoonywa na Mungu kuhusu mambo ambayo hayajaonekana bado, kwa kumcha Mungu alitengeneza safina ili kuokoa jamaa yake. Kwa imani yake aliuhukumu ulimwengu na akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
8 Por la fe Abraham hizo como Dios dijo cuando se le ordenó salir a un lugar que se le iba a dar como herencia, y salió sin saber a dónde iba.
Kwa imani Abrahamu, alipoitwa aende mahali ambapo Mungu angempa baadaye kuwa urithi, alitii na akaenda, ingawa hakujua anakokwenda.
9 Por la fe él era un vagabundo en la tierra de la promesa, como en una tierra extraña, viviendo en tiendas con Isaac y Jacob, quienes tenían una parte con él en la misma herencia:
Kwa imani alifanya maskani yake katika nchi ya ahadi kama mgeni katika nchi ya kigeni; aliishi katika mahema, kama Isaki na Yakobo walivyofanya, waliokuwa pia warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
10 Porque él estaba buscando la ciudad con fundamentos firmes, cuyo constructor y creador es Dios.
Kwa maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi ya kudumu ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
11 Y por la fe, la misma Sara tuvo poder para concebir, y dio a luz aún cuando era muy vieja, porque tuvo fe en aquel que dio su palabra;
Kwa imani Abrahamu, ingawa alikuwa mzee wa umri, naye Sara mwenyewe aliyekuwa tasa, alipokea uwezo wa kuwa baba kwa sababu alimhesabu Mungu aliyemwahidi kuwa mwaminifu na kwamba angetimiza ahadi yake.
12 De modo que, de un hombre, que estaba cerca de la muerte, llegaron niños en número como las estrellas en el cielo, o como la arena junto al mar que no puede ser contada.
Hivyo kutokana na huyu huyu ambaye alikuwa sawa na mfu, wakazaliwa wazao wengi kama nyota za mbinguni na kama mchanga wa pwani usiohesabika.
13 Todos estos llegaron a su fin en la fe, sin haber tenido la herencia; pero habiendo visto con alegría lejos, dieron testimonio de que eran extranjeros vagabundos sobre la tierra.
Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.
14 Para aquellos que dicen tales cosas, dejan en claro que están buscando una patria.
Watu wasemao mambo kama haya, wanaonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
15 Y realmente, si hubieran tenido en cuenta el país del que salieron, tendrían posibilidades de regresar.
Kwa kweli kama wangekuwa wanafikiri kuhusu nchi waliyoiacha, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16 Pero ahora su deseo es un país mejor, es decir, celestial; y entonces no es ninguna vergüenza que Dios sea llamado su Dios; porque él ha preparado una ciudad para ellos.
Lakini badala yake walitamani nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao, kwa kuwa amekwisha kuandaa mji kwa ajili yao.
17 Por la fe, Abraham hizo una ofrenda de Isaac, cuando fue probado; y aquel con quien se había hecho este pacto entregó como ofrenda el único hijo de su cuerpo,
Kwa imani Abrahamu, alipojaribiwa na Mungu, alimtoa Isaki kuwa dhabihu. Yeye aliyekuwa amezipokea ahadi za Mungu alikuwa tayari kumtoa mwanawe, aliyekuwa mwanawe pekee awe dhabihu.
18 De quien se había dicho: De Isaac tomará tu simiente su nombre:
Ingawa Mungu alikuwa amemwambia Abrahamu, “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwa Isaki,”
19 Juzgando que Dios fue capaz de dar vida hasta a los muertos; y debido a esto, lo recuperó como si estuviera muerto.
Abrahamu alihesabu kuwa Mungu angaliweza kumfufua Isaki kutoka kwa wafu. Na kwa kusema kwa mfano, alimpata tena Isaki kutoka kwa wafu.
20 Por la fe, Isaac, bendiciendo a Jacob y a Esaú, dio noticias de lo que vendrá.
Kwa imani Isaki alimbariki Yakobo na Esau kuhusu maisha yao ya baadaye.
21 Por la fe, Jacob bendijo a cada uno de los hijos de José, cuando estaba cerca de la muerte; y le dio culto a Dios, apoyado por su palo.
Kwa imani Yakobo alipokuwa anakufa, alimbariki kila mmoja wa mtoto wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
22 Por la fe José, cuando se acercaba su fin, dijo que los hijos de Israel saldrían de Egipto; y dio órdenes sobre sus huesos.
Kwa imani, Yosefu alipokaribia mwisho wa maisha yake, alinena habari za kutoka kwa wana wa Israeli huko Misri na akatoa maagizo kuhusu mifupa yake.
23 Por la fe, Moisés fue guardado en secreto por su padre y su madre durante tres meses después de su nacimiento, porque vieron que era un niño hermoso; y no tenían miedo de las órdenes del rey.
Kwa imani, wazazi wa Mose walimficha kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa, kwa sababu waliona kuwa si mtoto wa kawaida, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24 Por la fe Moisés, cuando llegó a ser hombre, no tuvo deseos de ser nombrado hijo de la hija de Faraón;
Kwa imani, Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25 Sintiendo que era mejor experimentar dolor con el pueblo de Dios, que por un corto tiempo probar los placeres del pecado;
Akachagua kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha kwa anasa za dhambi kwa kitambo kidogo tu.
26 Considerando que una parte en la vergüenza de Cristo es mejor que toda la riqueza de Egipto; porque tenía puesta la mirada en su recompensa última no en la inmediata.
Aliona kushutumiwa kwa ajili ya Kristo ni utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri, maana alikuwa anatazamia kupata thawabu baadaye.
27 Por la fe salió de Egipto, no siendo apartado de su propósito por temor a la ira del rey; porque siguió su camino, porque se sostuvo como viendo al Invisible.
Kwa imani Mose aliondoka Misri bila kuogopa ghadhabu ya mfalme. Alivumilia kwa sababu alimwona yeye asiyeonekana kwa macho.
28 Por la fe celebró la Pascua y puso la señal de la sangre sobre las casas, para que el ángel de la destrucción no matara a sus hijos mayores.
Kwa imani akaadhimisha Pasaka na kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wazaliwa wa Israeli.
29 Por la fe atravesaron el Mar Rojo como si hubiera sido tierra firme, aunque los egipcios fueron vencidos por el agua cuando intentaron hacer lo mismo.
Kwa imani, watu walivuka Bahari ya Shamu kama vile juu ya nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo, walitoswa ndani ya maji.
30 Por la fe, los muros de Jericó descendieron, después de haber sido rodeados por un círculo durante siete días.
Kwa imani kuta za Yeriko zilianguka, baada ya watu kuzizunguka kwa siku saba.
31 Por la fe, Rahab, la mujer ramera, no fue ejecutada con los que habían ido en contra de las órdenes de Dios, porque ella había tomado en su casa en paz a los espías.
Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.
32 ¿Qué más puedo decir? Porque no habría tiempo para contar las historias de Gedeón, Barac, Sansón y Jefté, de David, Samuel y los profetas:
Basi niseme nini zaidi? Sina wakati wa kusema habari za Gideoni, Baraka, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii,
33 Que por la fe vencieron a los reinos, hicieron justicia, obtuvieron su recompensa, mantuvieron cerradas las bocas de los leones,
ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitekeleza haki, na wakapokea ahadi za Mungu; walifunga vinywa vya simba,
34 Apagaron fuegos violentos, evitaron el filo de la espada, se fortaleció cuando estaban débiles, se llenó de poder en la guerra y puso en fuga a los ejércitos extranjeros.
wakazima makali ya miali ya moto, na wakaepuka kuuawa kwa upanga; udhaifu wao uligeuka kuwa nguvu; pia walikuwa hodari vitani na kuyafukuza majeshi ya wageni.
35 Las mujeres recibieron sus muertos mediante la resurrección; otros fueron torturados, sin ningún deseo de liberarse, para obtener una mejor resurrección;
Wanawake walipokea watu wao waliokuwa wamekufa, wakafufuliwa. Lakini wengine waliteswa, nao wakakataa kufunguliwa, ili wapate ufufuo ulio bora zaidi.
36 Y otros sufrieron burlas y golpes, e incluso con cadenas y cárceles:
Wengine walidhihakiwa na kupigwa, hata walifungwa minyororo na kutiwa gerezani.
37 Fueron apedreados, fueron cortados con cuchillos, fueron probados, los mataron con la espada, anduvieron en pieles de oveja y en pieles de cabra; siendo pobres y afligidos y maltratados cruelmente,
Walipigwa kwa mawe; walipasuliwa vipande viwili kwa msumeno; waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na mbuzi, wakiwa maskini, wakiteswa na kutendwa mabaya,
38 Vagando por lugares deshechos y en montañas y en agujeros en las rocas; para quien el mundo no era lo suficientemente bueno.
watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao. Walizunguka majangwani na milimani, katika mapango na katika mahandaki ardhini.
39 Y ninguno de ellos obtuvo lo prometido del pacto, aunque todos tenían un buen testimonio por medio de la fe,
Hawa wote walishuhudiwa vyema kwa sababu ya imani yao, lakini hakuna hata mmoja wao aliyepokea yale yaliyoahidiwa.
40 Porque Dios había guardado algo mejor para nosotros, para que no fuesen ellos perfeccionados aparte de nosotros.
Kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea kitu kilicho bora zaidi ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.

< Hebreos 11 >