< Génesis 4 >
1 Y el varón tuvo relaciones con su mujer Eva, y quedó encinta, y dio a luz a Caín, y dijo: Me ha dado un hombre él Señor.
Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.”
2 Entonces ella volvió a tener un hijo y dio a luz a Abel, su hermano. Y Abel era pastor de ovejas, pero Caín era granjero.
Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake. Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima.
3 Y después de un tiempo, Caín le dio al Señor una ofrenda de los frutos de la tierra.
Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana.
4 Y Abel dio una ofrenda de los corderos de su rebaño y de su grasa. Y el Señor estaba complacido con la ofrenda de Abel;
Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake,
5 Pero en Caín y en su ofrenda no se complació. Y Caín estaba enojado y su rostro se puso triste.
lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.
6 Y él Señor dijo a Caín: ¿Por qué estás enojado? y por qué tu cara está triste?
Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni?
7 Si lo haces bien, ¿no tendrás honor? y si lo haces mal, el pecado te espera en la puerta, deseando tenerte, pero no dejes que sea tu amo.
Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”
8 Y dijo Caín a su hermano: Pasemos al campo; y estando ellos en el campo, Caín atacó a su hermano Abel y lo mató.
Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.
9 Y él Señor dijo a Caín: ¿Dónde está tu hermano Abel? Y él dijo: No tengo idea: ¿soy el guardián de mi hermano?
Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
10 Y él dijo: ¿Qué has hecho? la voz de la sangre de tu hermano me está llamando desde la tierra.
Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini.
11 Y ahora eres maldito de la tierra, cuya boca está abierta para recibir la sangre de tu hermano de tu mano;
Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako.
12 La tierra ya no te dará su fruto como la recompensa de tu trabajo; serás un vagabundo errante sobre la tierra.
Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”
13 Y dijo Caín: Mi castigo es mayor que mi fuerza.
Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili.
14 Me has enviado hoy de la faz de la tierra y de delante de tu rostro; Voy a ser un vagabundo errante sobre la tierra, y el que me vea me matará.
Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”
15 Y él Señor dijo: De cierto, si muere Caín, siete vidas serán tomadas por él. Y el Señor puso una marca en Caín para que nadie lo matara.
Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue.
16 Y se apartó Caín de delante de la faz del Señor, y se quedó a vivir en la tierra de Nod, al oriente del Edén.
Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.
17 Y Caín tuvo relaciones con su esposa, y ella engendró y dio a luz a Enoc; y él hizo una ciudad, y le dio a la ciudad el nombre de Enoc por su hijo.
Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake.
18 Y Enoc tuvo un hijo Irad; e Irad fue padre de Mehujael; y Mehujael padre de Metusael; y Metusael fue padre de Lamec.
Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.
19 Y Lamec tuvo dos mujeres; el nombre de uno era Ada, y el nombre del otro Zila.
Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila.
20 Y Ada dio a luz a Jabal; era el padre de los que viven en tiendas y tienen ganado.
Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama.
21 Y el nombre de su hermano era Jubal: él era el padre de todos los que tocan con arpa y flauta.
Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.
22 Y Zila dio a luz a Tubal-caín, que es el padre de todo fabricante de instrumentos de bronce y de hierro, y la hermana de Tubal-caín fue Naama.
Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.
23 Y dijo Lamec a sus mujeres, Ada y Zila, escucha mi voz; esposas de Lamec, presten atención a mis palabras, porque yo pondría a muerte a un hombre por una herida, y a un joven por un golpe;
Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
24 Si se quieren tomar siete vidas como castigo por la muerte de Caín, setenta y siete serán tomadas por las de Lamec.
Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”
25 Y Adán volvió a tener relaciones con su esposa, y ella dio a luz a un hijo al que dio el nombre de Set, porque ella dijo: Dios me ha dado otra simiente en lugar de Abel, a quien Caín mató.
Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”
26 Y Set tuvo un hijo, y le dio el nombre de Enós: en este tiempo los hombres primero hicieron uso del nombre del Señor en adoración.
Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.