< Génesis 22 >

1 Después de estas cosas, Dios puso a prueba a Abraham, y le dijo: ¡Abraham! y él dijo: Heme aquí.
Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!” Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”
2 Y él le dijo: Toma a tu hijo, tu único y amado hijo Isaac, y ve a la tierra de Moriah, y ofrécelo como holocausto en uno de los montes, del cual yo te daré conocimiento.
Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”
3 Y Abraham se levantó temprano en la mañana, y preparó su asno, y tomó consigo dos de sus jóvenes e Isaac, su hijo, y después de que se había cortado el leño para la ofrenda quemada, se fue en su camino al lugar del cual Dios le había dado la palabra.
Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia.
4 Y al tercer día, Abraham, alzando sus ojos, vio el lugar de lejos.
Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali.
5 Entonces dijo a sus jóvenes: Quédate aquí con el asno; y yo y el niño continuaremos y rendiremos culto y regresaremos a ti.
Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”
6 Y Abraham puso la leña para la ofrenda quemada en la espalda de su hijo, y él mismo tomó el fuego y él cuchillo en su mano, y los dos siguieron juntos.
Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja,
7 Entonces Isaac dijo a Abraham: Mi padre; y él dijo: Heme aquí, mi hijo. Y él dijo: Aquí tenemos leña y fuego, pero ¿dónde está el cordero para la ofrenda quemada?
Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!” Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.” Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
8 Y Abraham dijo: Dios mismo dará el cordero para el holocausto; y así continuaron juntos.
Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.
9 Y vinieron al lugar del cual Dios le había dado conocimiento; y allí hizo Abraham el altar, y puso la leña en su lugar, y cerrando las ataduras alrededor de su hijo Isaac, lo puso sobre la leña sobre el altar.
Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni.
10 Y extendiendo su mano, Abraham tomó el cuchillo para matar a su hijo.
Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe.
11 Pero la voz del ángel del Señor vino del cielo, diciendo: Abraham, Abraham, y él dijo: Heme aquí.
Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!” Akajibu, “Mimi hapa.”
12 Y él dijo: No se extienda tu mano contra el niño para hacerle nada; por ahora estoy seguro de que el temor de Dios está en tu corazón, porque no has retenido a tu hijo, tu único hijo, de mí.
Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”
13 Y alzando sus ojos, Abraham vio una oveja fijada por los cuernos en la maleza: y Abraham tomó las ovejas e hizo una ofrenda quemada en lugar de su hijo.
Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 Y dio Abraham aquel lugar el nombre del Señor proveerá, y dijo: Como se dice hasta hoy, en el monte del Señor se proveerá.
Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”
15 Y la voz del ángel del Señor vino a Abraham una segunda vez desde el cielo,
Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili,
16 Diciendo: He jurado por mi nombre, dice el Señor, porque has hecho esto y no has apartado de mí a tu único hijo amado,
akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee,
17 que ciertamente te daré mi bendición, y tu simiente será aumentada como las estrellas del cielo y la arena a la orilla del mar; tu simiente tomará la tierra de los que están en contra de ellos;
hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao,
18 Y tu descendencia será bendición para todas las naciones de la tierra, porque has hecho lo que te ordené que hicieras.
na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”
19 Entonces Abraham regresó con sus jóvenes y se fueron juntos a Beerseba, el lugar donde Abraham vivía.
Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.
20 Después de estas cosas, Abraham tuvo noticias de que Milca, la esposa de su hermano Nacor, había dado a luz a niños;
Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana:
21 Uz el mayor, y Buz su hermano, y Kemuel, padre de Aram,
Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu),
22 Y Quesed, Hazo, Pildas, Jidlaf, Betuel.
Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.”
23 Betuel fue el padre de Rebeca; estos ocho fueron los hijos de Milca y Nacor, hermano de Abraham.
Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane.
24 Y su concubina Reúma dio a luz a Teba, Gaham, Tahas y Maaca.
Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.

< Génesis 22 >