< Esdras 6 >

1 Entonces el rey Darío dio una orden y se hizo una búsqueda en la casa de los registros, donde las cosas de valor estaban almacenadas en Babilonia.
Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
2 Y en Ecbatana, en él palacio del rey en la tierra de Media, se encontraron con un rollo, en el cual esta declaración quedó registrada:
Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
3 En el primer año de Ciro el rey, Ciro el rey hizo una orden: En relación con él templo de Dios en Jerusalén, que él templo sea reconstruido, el lugar donde hacen ofrendas, y los fundamentos para las bases también; Que tenga sesenta codos de alto y sesenta codos de ancho;
Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
4 Con tres líneas de grandes piedras y una línea de nuevos soportes de madera; y que el dinero necesario salga del almacén del rey;
kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
5 Dejen que los recipientes de oro y plata de la casa de Dios, que Nabucodonosor tomó del Templo de Jerusalén a Babilonia, sean devueltos y devueltos al Templo de Jerusalén, cada uno en su lugar, y los pongan en su lugar en el templo de Dios.
Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
6 Así que ahora, Tatnai, gobernante de la tierra al oeste del río, y Setar-boznai y tu gente los Afarsaqueos al oeste del río, apártense de ese lugar:
Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
7 Que la obra de este templo de Dios continúe; que el gobernante de los judíos y sus hombres responsables levanten este templo de Dios en su lugar.
Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
8 Además, doy órdenes sobre lo que debe hacer por los hombres responsables de los judíos en relación con la reconstrucción de esta casa de Dios: la riqueza del rey, es decir, los impuestos reunidos en el otro lado del río, el dinero que se necesita se les debe dar a estos hombres sin demora, para que su trabajo no se detenga.
Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
9 Y todo lo que necesiten, becerros, ovejas y corderos, para las ofrendas quemadas al Dios del cielo, grano, sal, vino y aceite, todo lo que los sacerdotes en Jerusalén digan que es necesario, debe ser dado a día a día regularmente:
Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
10 Para que puedan hacer ofrendas de olor dulce al Dios del cielo, con oraciones por la vida del rey y de sus hijos.
ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
11 Y he dado órdenes de que si alguien hace algún cambio en esta palabra, uno de los maderos debe ser sacado de su casa, y él debe ser levantado y colgado al madero; y su casa ha de ser desechada a causa de esto;
Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
12 Y que el Dios que ha escogido a Jerusalén como un lugar de descanso para su nombre envíe destrucción a todos los reyes y pueblos cuyas manos están extendidas para hacer algún cambio en esto o para hacer daño a este templo de Dios en Jerusalén. Yo, Darío, he dado esta orden, que se haga prestamente.
Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
13 Entonces Tatnai, el gobernante de la pueblo que cruza el río Eufrates, y Setar-boznai y su gente, cumplieron a la orden dada por el rey Darío, hizo lo que había dicho con todo cuidado.
Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
14 Y los hombres responsables de los judíos continuaron con la reconstrucción del edificio, ayudados por la enseñanza del profeta Hageo y Zacarías, el hijo de Ido. Continuaron construyendo hasta que estuvo completo, de acuerdo con la palabra del Dios de Israel y las órdenes dadas por Ciro, Darío y Artajerjes, rey de Persia.
Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
15 Y la construcción de esta casa se completó el tercer día del mes Adar, en el sexto año del gobierno de Darío el rey.
Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
16 Y los hijos de Israel, los sacerdotes y los levitas, y el resto de los que habían regresado, celebraron la fiesta de la apertura del templo de Dios con alegría.
Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
17 Y dieron, como ofrendas en la apertura de esta casa de Dios, cien bueyes, doscientas ovejas, cuatrocientos corderos; y por una ofrenda por el pecado para todo Israel, doce chivos, siendo el número de las tribus de Israel.
Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
18 Y pusieron a los sacerdotes en sus turnos correspondientes y a los levitas en su orden, para la adoración de Dios en Jerusalén; Como está registrado en el libro de Moisés.
Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
19 Y los hijos de Israel que habían regresado, celebraron la Pascua el día catorce del mes primero.
Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
20 Porque los sacerdotes y los levitas se habían purificado juntos; todos estaban ritualmente limpios, y dieron muerte al cordero de la Pascua por todos los que habían regresado, por sus hermanos, los sacerdotes y por ellos mismos.
Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
21 Y los hijos de Israel, que habían regresado, y todos los que se habían unido a ellos, después de haberse separado de los malos caminos de la gente de la tierra para convertirse en siervos del Señor, el Dios de Israel, tomaron la pascua juntos,
Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
22 Y guardó con gozo la fiesta del pan sin levadura durante siete días: porque el Señor los había llenado de alegría, y convertido él corazón del rey de Asiria hacia ellos, para ayudarles en la obra de la casa de Dios, el Dios de Israel.
Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.

< Esdras 6 >