< Éxodo 40 >

1 Y él Señor dijo a Moisés:
Kisha Bwana akamwambia Mose:
2 El primer día del primer mes debes colocar el santuario de la Tienda de reunión.
“Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
3 Y en su interior pon el cofre del pacto, colgando el velo delante de ella.
Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
4 Y pon la mesa dentro, colocando todas las cosas en orden; y pongan el candelabro, y coloca al candelabro sus lámparas.
Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
5 Y pon el altar de oro para él incienso delante del cofre del pacto, y cuelga la cortina sobre la entrada del santuario.
Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
6 Y pondrás el altar de las ofrendas quemadas delante de la puerta de la Tienda de reunión.
“Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
7 Y que el vaso para lavatorio, con agua en él, se ponga entre la Tienda de reunión y el altar.
weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
8 Y pon las cortinas que forman el atrio alrededor de ella, con la cortina sobre su entrada.
Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
9 Y toma el aceite santo, y ungirás el tabernáculo todo lo que hay en él, y ungirás todos los utensilios; porque lo que está en él es santo;
“Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
10 Y ungirás como aceite el altar de la ofrenda quemada, y lo santificarás con todos sus vasos; este altar debe ser santísimo.
Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
11 Y ungirás la vasija de lavar y su base, y santifícalos.
Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
12 Entonces Aarón y sus hijos vayan a la puerta de la Tienda de reunión; y después de lavarlos con agua,
“Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
13 Debes vestir a Aarón con las vestiduras sagradas; y lo ungirás con aceite, y lo santificarás, para que sea mi sacerdote.
Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
14 Y lleven sus hijos con él, y vístanlos con las túnicas;
Walete wanawe na uwavike makoti.
15 Y y los ungirás con aceite como lo hiciste con su padre, para que sean mis sacerdotes; con la unción del aceite los convertirás en sacerdotes para siempre, de generación en generación.
Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
16 Y Moisés hizo esto; como el Señor le dio órdenes, así lo hizo.
Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
17 Así que en el primer día del primer mes en el segundo año el santuario fue levantado.
Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
18 Moisés levantó el santuario; colocando sus bases en posición y levantando sus montantes, colocando las varillas y plantando los pilares en su lugar;
Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
19 Extendiendo la tienda exterior sobre ella, y cubriéndola, como el Señor le había dado órdenes.
Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
20 Y él tomó la ley y la puso dentro del arca, y puso las varas a su lado y la cubierta sobre ella;
Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
21 Y llevó el cofre del pacto al santuario, colgando el velo delante de él, como el Señor le había dado órdenes.
Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
22 Y él puso la mesa en la Tienda de reunión, en el lado norte fuera del velo.
Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
23 Y puso el pan delante del Señor, como él Señor lo había dicho.
na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
24 El candelabro lo puso en la Tienda de reunión, frente a la mesa, en el lado sur:
Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
25 Encendiendo las luces delante del Señor, como el Señor le había dado órdenes.
na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
26 Y puso el altar de oro en la Tienda de reunión, delante del velo:
Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
27 Y quemó sobre él el incienso aromático, como el Señor le había dado órdenes.
na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
28 Y él puso la cortina en la puerta del santuario.
Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
29 Y a la puerta del santuario de la Tienda de reunión, él puso el altar de las ofrendas quemadas, ofreciendo en él las ofrendas quemadas y las ofrendas de cereales, como el Señor le había dado las órdenes.
Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
30 Y entre el altar y la Tienda de reunión, puso el recipiente con agua para lavar.
Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
31 En él se lavaron las manos y los pies de Moisés, Aarón y sus hijos,
Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
32 Cada vez que entraban en la Tienda de reunión, y cuando se acercaban al altar, como el Señor le había dado órdenes a Moisés.
Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Y él puso las cortinas que forman el atrio alrededor del santuario y el altar, y puso la cortina sobre la entrada. Entonces Moisés hizo el trabajo completo.
Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
34 Entonces la nube descendió y cubrió la tienda de reunión, y la casa estaba llena de la gloria del Señor;
Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
35 De modo que Moisés no pudo entrar en la Tienda de reunión, porque la nube descansaba sobre ella, porque él santuario estaba lleno de la gloria del Señor.
Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
36 Y cuando la nube se levantaba de la Casa, los hijos de Israel continuaban su viaje:
Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
37 Pero mientras la nube estaba allí, no hicieron ningún movimiento hasta que la nube se levantaba, tampoco ellos levantaban su campamento.
lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
38 Porque la nube del Señor estaba descansando en él santuario de día, y en la noche había fuego en la nube, ante los ojos de todo el pueblo de Israel, y así fue en todos sus viajes.
Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.

< Éxodo 40 >