< Éxodo 18 >

1 Entonces llegaron noticias a Jetro, el sacerdote de Madián, suegro de Moisés, de todo lo que Dios había hecho por Moisés y por su pueblo Israel, y porque el Señor había sacado a Israel de Egipto.
Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
2 Y Jetro, suegro de Moisés, tomó a Séfora, esposa de Moisés, después de haberla despedido,
Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
3 Y a sus dos hijos, uno de los cuales se llamaba Gersón, porque dijo: He estado viviendo en tierra extraña.
pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
4 Y el otro se llamaba Eliezer, porque dijo: El Dios de mi padre fue mi ayuda, y me mantuvo a salvo de la espada de Faraón.
Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
5 Y vino Jetro, suegro de Moisés, con sus hijos y su mujer, a donde Moisés había levantado su tienda en el desierto, junto al monte de Dios.
Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
6 Y él dijo a Moisés: Yo, tu suegro, he venido a ti, con tu mujer y tus dos hijos.
Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
7 Y salió Moisés a su suegro, y postrándose delante de él, le besó; y se dijeron unos a otros: ¿Estás bien? y ellos vinieron a la tienda.
Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
8 Y Moisés dio a su suegro cuenta de todo lo que el Señor había hecho a Faraón y a los egipcios a causa de Israel, y de todos los problemas que habían venido sobre ellos en el camino, y cómo el Señor les había dado la salvación.
Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
9 Y Jetro se alegró porque el Señor había sido bueno con Israel, liberándolos del poder de los egipcios.
Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
10 Y Jetro dijo: Alabado sea el Señor, que te ha tomado de la mano de Faraón y de la mano de los egipcios; liberando a la gente del yugo de los egipcios.
Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
11 Ahora estoy seguro de que el Señor es más grande que todos los dioses, porque los ha vencido en su orgullo.
Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
12 Entonces Jetro, suegro de Moisés, hizo una ofrenda quemada a Dios; y vino Aarón con los jefes de Israel, y comió con el suegro de Moisés, delante de Dios.
Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
13 Al día siguiente, Moisés se sentó para tomar decisiones por el pueblo; y la gente esperaba a Moisés desde la mañana hasta la tarde.
Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
14 Y cuando el suegro de Moisés vio todo lo que estaba haciendo, dijo: ¿Qué es esto que estás haciendo por la gente? ¿Por qué estás sentado aquí solo, con toda la gente esperándote desde la mañana hasta la tarde?
Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
15 Y dijo Moisés a su suegro: Porque el pueblo viene a mí para recibir instrucciones de Dios;
Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
16 Y si tienen alguna pregunta entre ellos, vienen a mí, y yo soy juez entre un hombre y su prójimo, y les doy las órdenes y las leyes de Dios.
Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
17 Y el suegro de Moisés le dijo: Lo que estás haciendo no es bueno.
Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
18 Tu fuerza y ​​la de las personas se agotarán por completo: este trabajo es más de lo que puedes hacer tu mismo.
Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
19 Escucha ahora mi sugerencia, y que Dios esté contigo: debes ser el representante del pueblo ante Dios, llevando sus causas a él:
Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
20 Enseñándoles sus reglas y sus leyes, guiándolos en la forma en que deben ir, y dejando en claro para ellos el trabajo que tienen que hacer.
Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
21 Pero por lo demás, toma de entre la gente hombres de valor, como los que tienen temor de Dios, hombres verdaderos que odian las ganancias hechas erróneamente; y pon a tales hombres sobre ellos, para ser capitanes de miles, capitanes de cientos y de cincuenta y de diez;
Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
22 Y sean jueces en las causas de las personas en todo momento: y pongan a su disposición todas las preguntas importantes, pero en cosas pequeñas, que tomen decisiones por sí mismos: de esta manera, será menos difícil para ustedes, y ellos te quitará el peso.
Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
23 Si haces esto, y Dios da la aprobación, entonces podrás continuar sin cansancio, y todo este pueblo irá a sus tiendas en paz.
Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
24 Entonces Moisés tomó nota de las palabras de su suegro e hizo como él lo había dicho.
Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
25 E hizo una selección de hombres capaces de todo Israel, y los hizo jefes sobre el pueblo, capitanes de miles, capitanes de cientos y de cincuenta y de diez.
Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
26 Y fueron jueces en las causas de la gente en todo tiempo: las preguntas difíciles las presentaron ante Moisés; pero en cada pequeño punto, ellos mismos dieron sus decisiones.
Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
27 Y Moisés dejó ir a su suegro, y volvió a su tierra.
Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.

< Éxodo 18 >