< Ester 9 >

1 Ahora, a los trece días del duodécimo mes, que es el mes de Adar, cuando llegó el momento de que se pusiera en práctica la orden del rey, el mismo día en que los que odiaban a los judíos esperaban poder gobernar sobre ellos; aunque había ocurrido lo contrario, y los judíos gobernaron a sus enemigos;
Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, yaani mwezi wa Adari, amri iliyoagizwa na mfalme ilikuwa itekelezwe. Siku hii adui wa Wayahudi walikuwa wametumaini kuwashinda, lakini sasa mambo yaliwageukia na Wayahudi wakawashinda wale waliokuwa wanawachukia.
2 En ese día, los judíos se reunieron en sus pueblos a través de todas las provincias del reino de Asuero, con el propósito de atacar a todos los que intentaban el mal contra ellos; y todos tenían que ceder ante ellos, por el temor a ellos había venido sobre todos los pueblos.
Wayahudi walikusanyika katika miji yao, katika majimbo ya Mfalme Ahasuero kuwashambulia wale waliokuwa wanatafuta kuwaangamiza. Hakuna yeyote aliyeweza kushindana nao, kwa sababu watu wa mataifa mengine yote waliwaogopa.
3 Y todos los jefes, los capitanes, los gobernantes y los que hicieron los negocios del rey dieron apoyo a los judíos; porque el miedo a Mardoqueo había venido sobre ellos.
Nao wakuu wote wa majimbo, majemadari, watawala na maafisa wa mfalme wakawasaidia Wayahudi, kwa sababu walimhofu Mordekai.
4 Porque Mardoqueo era poderoso en la casa del rey, y corrió la voz de su fama por todo el reino, porque el hombre Mardoqueo se hizo cada vez más poderoso.
Mordekai alikuwa mtu mashuhuri katika jumba la mfalme; sifa zake zilienea katika majimbo yote naye alipata uwezo zaidi na zaidi.
5 Entonces los judíos vencieron a todos sus atacantes con la espada y con la muerte y la destrucción, e hicieron a sus enemigos todo lo que quisieron.
Wayahudi waliwaangusha adui zao wote kwa upanga wakiwaua na kuwaangamiza, nao walifanya kile walichotaka kwa wale waliowachukia.
6 Y en Susa, los judíos mataron a quinientos hombres.
Katika ngome ya Shushani Wayahudi waliua na kuangamiza wanaume 500.
7 Mataron a Parsdata, Dalfon, Aspata,
Pia waliwaua Parshendatha, Dalfoni, Aspatha,
8 Porata, Adalia, Aridata,
Poratha, Adalia, Ardatha,
9 Parmasta, Arisai, Aridai y Vaizata,
Parmashta, Arisai, Aridai na Waizatha,
10 Los diez hijos de Amán, hijo de Hamedata, el enemigo de los judíos; Pero no echaron mano a ninguno de sus bienes.
wana kumi wa Hamani mwana wa Hamedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchukua nyara.
11 Ese día se dio al rey el número de los que habían muerto en la ciudad de Susa.
Mfalme aliarifiwa siku iyo hiyo hesabu ya waliouawa katika ngome ya Shushani.
12 Y el rey dijo a la reina Ester: Los judíos han matado a quinientos hombres en Susa, así como a los diez hijos de Amán: ¡qué más habran hecho en el resto del reino! Ahora cuál es tu deseo? porque te será dado; ¿Qué otra petición tienes? y será hecho.
Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wamewaua wanaume 500 na wana kumi wa Hamani ndani ya ngome ya Shushani. Wamefanyaje katika majimbo mengine ya mfalme yaliyobaki? Je, sasa haja yako ni nini? Nayo pia utapewa. Nalo ombi lako ni nini? Nalo utafanyiwa.”
13 Entonces Ester dijo: Si es un placer del rey, que se dé autoridad a los judíos en Susa para que hagan mañana como se ha hecho hoy, y que se den órdenes para el ahorcamiento de los diez hijos de Amán.
Esta akajibu, “Ikimpendeza mfalme, uwape ruhusa Wayahudi walioko Shushani warudie amri ya leo kesho pia, na wana wa Hamani kumi wanyongwe mahali pa kunyongea watu.”
14 Y el rey dijo que esto iba a hacerse, y la orden fue dada en Susa, y el ahorcamiento de los diez hijos de Amán fue efectuado.
Basi mfalme akaamuru kwamba hili litendeke. Amri ilitolewa huko Shushani, nao wakawanyonga wana kumi wa Hamani.
15 Porque los judíos que estaban en Susa se reunieron de nuevo el día catorce del mes Adar y mataron a trescientos hombres en Susa. Pero no pusieron una mano sobre sus bienes.
Wayahudi huko Shushani wakakusanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, nao wakawaua wanaume 300 huko Shushani, lakini hawakuchukua nyara zao.
16 Y los demás judíos de todas las provincias del reino se unieron, lucharon por sus vidas, obtuvieron la salvación de sus enemigos y mataron a setenta y cinco mil de ellos; Pero no pusieron mano a sus bienes.
Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao 75,000 lakini hawakugusa nyara zao.
17 Esto hicieron el día trece del mes Adar; y el día catorce del mismo mes tomaron su descanso y lo convirtieron en un día de fiesta y alegría.
Hili lilitendeka siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari na siku ya kumi na nne walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
18 Pero los judíos en Susa se reunieron el trece y el catorce día del mes; y en el decimoquinto día tomaron su descanso, y lo hicieron un día de fiesta y alegría.
Wayahudi huko Shushani, hata hivyo, walikuwa wamekusanyika siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne, pia siku ya kumi na tano walipumzika na kuifanya siku ya karamu na furaha.
19 Entonces, los lugares de los judíos del país que viven en pueblos sin murallas, hacen del decimocuarto día del mes Adar un día de fiesta y alegría y un buen día, un día para enviar ofrendas uno a otro.
Ndiyo sababu Wayahudi wanaokaa vijijini na katika miji midogo huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu, siku ambayo wao hupeana zawadi mmoja kwa mwingine.
20 Y Mardoqueo envió cartas a todos los judíos en todas las provincias del reino de Asuero, cercanas y lejanas.
Mordekai aliandika matukio haya, naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote walioko katika majimbo ya Mfalme Ahasuero, majimbo yaliyo mbali na karibu,
21 Ordenándoles que guarden el decimocuarto día del mes Adar y el decimoquinto día del mismo mes, todos los años.
akiwataka kila mwaka washerehekee siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ya mwezi wa Adari
22 Como días en que los judíos descansaron de sus enemigos, y el mes que para ellos se convirtió de tristeza en alegría, y de llanto a gozo: y que debían guardarlos como días de fiesta y alegría, de enviar ofrendas unos a otros y cosas buenas a los pobres.
kama wakati ambao Wayahudi walipata nafuu kutoka kwa adui zao na kama mwezi ambao huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha na kuomboleza kwao kuwa siku ya kusherehekea. Aliwaandikia kushika siku hizo kama siku za karamu na za furaha na kupeana zawadi za vyakula wao kwa wao na zawadi kwa maskini.
23 Y los judíos dieron su palabra para continuar como lo habían estado haciendo y como Mardoqueo les había dado órdenes por escrito;
Hivyo Wayahudi walikubali kuendeleza sherehe walizokuwa wamezianza, wakifanya lile Mordekai alilokuwa amewaandikia.
24 Porque Aman, el hijo de Hamedata de Agag, el que odia a todos los judíos, había hecho planes para su destrucción, intentando obtener una decisión de Pur es decir, de probabilidad con el fin de acabar con ellos y destruirlos;
Kwa maana Hamani mwana wa Hamedatha Mwagagi, adui wa Wayahudi wote, alikuwa amepanga hila dhidi ya Wayahudi ili kuwaangamiza, na alikuwa amepiga puri (yaani kura) kwa ajili ya maangamizi na uharibifu wao.
25 Pero cuando Ester se presentó ante el rey, dio órdenes por cartas que el malvado plan que había hecho contra los judíos debía volverse contra sí mismo; y que él y sus hijos iban a morir por ahorcamiento.
Lakini wakati shauri hilo baya lilipoarifiwa kwa mfalme, alitoa amri iliyoandikwa kwamba mipango mibaya ambayo Hamani ameipanga dhidi ya Wayahudi inapasa imrudie juu ya kichwa chake mwenyewe, na kwamba yeye na wanawe waangikwe mahali pa kunyongea watu.
26 Así que estos días fueron nombrados Purim, después del nombre de Pur. Y así, debido a las palabras de esta carta, y de lo que habían visto en relación con este negocio, y lo que les había tocado vivir.
(Kwa hiyo siku hizi ziliitwa Purimu, kutokana na neno puri.) Kwa sababu ya kila kitu kilichoandikwa kwenye barua hii na kwa sababu ya yale waliyoyaona na yale yaliyowatokea,
27 Los judíos establecieron una regla y se comprometieron, haciendo que su simiente y todos los que se unieron a ellos hicieran lo mismo, para que esté vigente para siempre, que mantendrían esos dos días, según lo ordenado en la carta, en el horario fijo de cada año;
Wayahudi wakachukua na kuifanya desturi kwamba wao na wazao wao na wote ambao walijiunga nao wangefanya bila kuacha kushika siku hizi mbili kila mwaka, kwa njia ilivyoelekezwa na kwa wakati wake.
28 Y que esos días debían guardarse en la memoria a través de cada generación y cada familia, en cada provincia del reino y en cada ciudad, para que nunca haya un momento en que estos días de Purim no se olvidarán entre los judíos, ni su memoria se extinguiera de su descendencia.
Siku hizi zinapasa zikumbukwe na kuadhimishwa katika kila kizazi, kila jamaa na katika kila jimbo na kila jiji. Nazo siku hizi za Purimu kamwe zisikome kusherehekewa na Wayahudi, wala kumbukumbu zake zisipotee miongoni mwa wazao wake.
29 Entonces Ester la reina, hija de Abihail, y Mardoqueo, el judío, enviaron una segunda carta para confirmar su autoridad a la orden sobre Purim.
Basi Malkia Esta binti Abihaili, pamoja na Mordekai, Myahudi, waliandika kwa mamlaka yote kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu.
30 Y envió cartas a todos los judíos en las ciento veintisiete provincias del reino de Asuero, con palabras de paz y verdad.
Naye Mordekai akatuma barua kwa Wayahudi wote katika majimbo 127 ya ufalme wa Ahasuero, barua zenye maneno ya amani na matumaini,
31 Ordenando que se celebrará estos días de Purim en sus tiempos fijos, tal como lo había ordenado Mardoqueo Judío y Ester la reina, y de acuerdo con las reglas que ellos mismos habían establecido para ellos y su simiente, en conexión con su tiempo con ayuno y su clamor de ayuda.
ili kuimarisha siku hizi za Purimu katika majira yake yaliyowekwa, kama Mordekai, Myahudi na Malkia Esta walivyowaamuru, na walivyojiimarisha wenyewe na wazao wao kuhusu nyakati za kufunga na kuomboleza.
32 La orden dada por Ester confirmó la ley para celebrar él Purim; Y fue grabado en el libro.
Amri ya Esta ilithibitisha taratibu hizi kuhusu Purimu, nayo ikaandikwa katika kumbukumbu.

< Ester 9 >