< Eclesiastés 2 >
1 Dije en mi corazón: Te daré alegría por una prueba; así que toma tu placer, pero fue sin ningún propósito.
Nikasema moyoni, “Njoo, na nitakujaribu kwa kwa furaha. Kwa hiyo furahia.” Lakini tazama, huu nao ulikuwa ni upepo wa muda.
2 De risa dije: Es insensato; y de alegría - ¿De qué sirve?
Nikasema juu ya kicheko, “Ni wazimu,” na kuhusu furaha, “Yafaa nini?”
3 Hice una búsqueda con mi corazón para dar placer a mi carne con vino, todavía guiando mi corazón con sabiduría, y perseguir cosas tontas, para poder ver lo que era bueno para los hijos de los hombres hacer bajo Los cielos todos los días de su vida.
Nikajipeleleza moyoni mwangu katika jinsi ya kutimiza hamu yangu kwa mvinyo. Nikaruhusu akili yangu iongozwe na hekima ingawa bado nilikuwa nikishikilia ujinga. Nilitaka kutafuta jambo lililo jema kwa wanadamu kufanya chini ya mbingu wakati wa siku za maisha yao.
4 Realicé grandes obras, construyéndome casas y plantando viñas.
Nilitimiza mambo makubwa. Nilijenga nyumba kwa ajili yangu na kupanda miti ya mizabibu.
5 Me hice jardines y huertos, plantando en ellos árboles frutales de todo tipo.
Nilitengeneza bustani na viwanja; nikapanda aina zote za matunda ndani yake.
6 Hice estanques para regar los bosques donde crecían los árboles.
Nikatengeneza mabwawa ya maji ili kumwagilia msitu mahali miti ilikuwa imepandwa.
7 Compré siervos y sirvientas, y dieron a luz hijos e hijas en mi casa. Tenía una gran riqueza de rebaños y manadas, más que todos los que estaban en Jerusalén antes que yo.
Nilinunua watumwa wa kiume na wa kiume; nilikuwa na watumwa waliozaliwa katika ikulu yangu. Pia nikawa na makundi makubwa na wanyama wa kufugwa, zaidi ya mfalme yeyote aliyetawala kabla yangu katika Yerusalemu.
8 Reuní plata y oro y la riqueza de los reyes y de los países. Me hice de creadores de canto, cantores y cantoras; y las delicias de los hijos de los hombres, y concubinas.
Pia nilijikusanyia fedha na dhahabu, hazina ya wafalme na majimbo. Nikapata waimbaji wanaume na wanawake kwa ajili yangu, na kufurahia kutoka kwa wana wa wanadamu, masulia na wanawake.
9 Y me engrandecí; aumentando más que todos los que habían estado antes que yo en Jerusalén, y mi sabiduría todavía estaba conmigo.
Hivyo nikawa mkuu na tajiri kuliko wote waliokuwa Yerusalemu kabla yangu, na hekima yangu ilikuwa ndani yangu.
10 Y nada de lo que mis ojos deseaban les negué; No guardé ninguna alegría de mi corazón, porque mi corazón se complació en todo mi trabajo, y esta fue mi recompensa.
Lolote ambalo macho yangu yalikitamani sikuyazuia. Sikuuzuia moyo wangu katika furaha yeyote, kwa sababu moyo wangu ulifurahi katika katka kazi yangu zote na furaha ilikuwa ni tunu kwa kazi zangu zote.
11 Entonces vi todas las obras que mis manos habían hecho, y todo aquello por lo que había estado trabajando; y vi que todo era inútil y aflicción de espíritu, y que no había ganancia bajo el sol.
Kisha nikatazama matendo yote ambayo mikono yangu iliyokwisha kuyatimiliza na juu ya kazi niliyokuwa nimeifanya, lakini tena, kila kitu kilikuwa ni mvuke na kujaribu kuuchunga upepo. Hakukuwa na faida chini ya jua.
12 Volví a buscar sabiduría y caminos necios. ¿Qué puede hacer el hombre que viene después del rey? Lo que él ha hecho antes.
Kisha nikageuka kuipambanua hekima, na upumbavu na ujinga. Kwa maana ni kitu gani mfalme anayekuja baada yangu afanye, ambacho hakijafanyika?
13 Entonces vi que la sabiduría es mejor que la insensatez, y que la luz es mejor que la oscuridad.
Kisha nikaanza kuelewa kwamba hekima ina faida kuliko upumbavu, kama nuru ilivyo bora kuliko giza.
14 Los ojos del sabio están en su cabeza, pero el necio va caminando en la oscuridad; Pero aun así vi que el mismo suceso les llega a todos.
Mwenye hekima hutumia macho yake katika kichwa chake kuona mahali anakoenda, lakini mpumbavu hutembea katika giza, ingawa ninafahamu kuwa mwisho wa aina moja umetunzwa kwa kila mmoja.
15 Entonces dije en mi corazón: En lo que se refiere al hombre necio, así vendrá a mí; así que ¿para qué he sido demasiado sabio? Entonces dije en mi corazón: Esto de nuevo no tiene ningún propósito.
Kisha nikasema moyoni mwangu, “Kinachotokea kwa mpumbavu, ndicho kitachotokea na kwangu. Hivyo kuna utofauti gani kama mimi ni mwenye hekima sana?” Nikahitimisha moyoni mwangu, “Huu pia ni mvuke tu.”
16 Del sabio, como del necio, no hay memoria para siempre, ya que aquellos que ahora son habrán desaparecido de la memoria en los próximos días. ¡Mira cómo la muerte llega a los sabios como a los necios!
Kwa kuwa mwenye hekima, kama mpumbavu, hakumbukwi kwa muda mrefu. Katika siku zijazo, kila kitu kitakuwa kimesahauliwa. Mwenye hekima hufa kama navyokufa mpumbavu.
17 Entonces odiaba la vida, porque todo lo que estaba debajo del sol era malo para mí, no tiene ningún propósito y todo es aflicción de espíritu.
Hivyo nikauchukia uhai kwa sababu kazi zote zilizofanyika chini ya jua zilikuwa mbaya kwangu. Hii ni kwa sababu kila kitu ni mvuke na kujaribu kuuchunga upepo.
18 Yo odiaba todo el fruto de mi trabajo que había hecho, porque lo dejaré al hombre que viene después de mí.
Nikachukia yote niliyoyatimiza, ambayo nilikuwa nimekwisha yafanya chini ya jua kwa sababu ni lazima niyaache kwa mtu anaye kuja baada yangu.
19 ¿Y quién puede decir si ese hombre será sabio o insensato? Pero tendrá poder sobre todo el trabajo que he hecho y en el que he sido sabio bajo el sol. Esto de nuevo no tiene ningún propósito.
Na ni nani ajuaye kama atakuwa mwenye hekima au mpumbavu? Ila atakuwa msimamizi juu ya kila kitu chini ya jua ambayo kazi yangu na hekima yangu imeyajenga. Huu pia ni mvuke.
20 Así que mi mente se convirtió en dolor por todos los problemas que había tomado y toda mi sabiduría bajo el sol.
Kwa hiyo moyo wangu ukaanza kukata tamaa juu ya kazi zote nilizozifanya chini ya jua.
21 Porque hay un hombre cuyo trabajo ha sido hecho con sabiduría, con conocimiento y con mano experta; pero uno que no ha hecho nada por él, lo tendrá por su herencia. Esto de nuevo no tiene ningún propósito y es un gran mal.
Kwa kuwa kunaweza kuwa na mtu anayefanya kazi kwa hekima, ufahamu, na umahili, lakini ataacha kila kitu alichonacho kwa mtu ambaye hajafanya chochote. Huu nao ni mvuke na hatari kubwa.
22 ¿Qué obtiene un hombre por todo su trabajo y por el peso del cuidado con el que ha hecho su trabajo bajo el sol?
Kwa maana ni faida gani mtu hupata ambaye hufanya kazi kwa juhudi na kujaribu moyoni mwake kutimiza kazi zake chini ya jua?
23 Todos sus días son dolor, y su obra está llena de dolor. Incluso en la noche su corazón no tiene descanso. Esto de nuevo no tiene ningún propósito.
Kila siku kazi yake ni maumivu na masikitiko, hivyo wakati wa usiku roho yake haipumziki. Huu pia ni mvuke.
24 No hay nada mejor para un hombre que comer y beber, y deleitarse en su trabajo. Esto que nuevamente vi fue de la mano de Dios.
Hakuna jambo jema kwa mtu yeyote zaidi ya kula na kunywa na kuridhika na kile kilichochema katika kazi yake. Nikaona kwamba ukweli huu unatoka kutoka mkononi mwa Mungu.
25 ¿Quién puede comer o tener placer sin él?
Kwa kuwa ni nani anaweza kula au anaweza kupata furaha yoyote tofauti na Mungu?
26 Al hombre con quien se complace, Dios le da sabiduría, conocimiento y gozo; pero al pecador le da el trabajo de juntar bienes y acumular riquezas, para dar a aquel en quien Dios tiene placer. Esto de nuevo no tiene ningún propósito y es aflicción de espíritu.
Kwa kuwa kwa kila anayemfurahisha yeye, Mungu humpa hekimana ufahamu ba furaha. Ingawa, kwa mwenye dhambi humpa kazi ya kukusanya na kutunza ili kwamba ampe mtu anayempendeza Mungu. Huu pia ni sawa na mvuke na kujaribu kuuchunga upepo.