< Deuteronomio 22 >

1 Si ves que el buey o la oveja de tu hermano deambulan, no te vayas sin ayudar, llévalos a tu hermano.
Hautakiwi kumtazama ng’ombe au kondoo wa Muisraeli mwenzako akikosea njia na ukajificha kwao; hakika unapaswa kuwarejesha kwake.
2 Si su dueño no está cerca, o si no estás seguro de quién es, llevala bestia a tu casa y guárdela hasta que su dueño la busque, y luego debes devolvérsela.
Iwapo Muisraeli mwenzako hayupo karibu nawe, au kama haumfahamu, basi unapaswa kumleta mnyama huyo nyumbani kwako, na lazima uwe naye mpaka pale mwenyewe atakapomtafuta, na kisha lazima umrejeshee mwenyewe.
3 Haz lo mismo con su asno o su túnica o cualquier cosa que haya perdido tu hermano y con la que te hayas encontrado. No lo ignores.
Unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa punda wake; unapaswa kufanya vivyo hivyo na vazi lake; unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa kila kitu alichopoteza Muisraeli mwenzako, kitu chochote alichopoteza na ukakipata; hautakiwi kujificha.
4 Si ves que el buey o el asno de tu hermano caen en el camino, no pases sin darle ayuda para levantarlo.
Haupaswi kumwona punda wa Muisraeli mwenzako au ng’ombe wake kaanguka chini barabarani na kujificha dhidi yao; hakika unapaswa kumsaidia kumwinua tena.
5 No es correcto que una mujer se vista con ropa de hombre, o que un hombre se ponga una túnica de mujer; quien hace tales cosas es repugnante para el Señor tu Dios.
Mwanamke hatakiwi kuvaa kinachokusudiwa kwa mwanamume, vilevile mwanamume hapaswi kuvaa mavazi ya mwanamke; kwa maana yeyote afanyaye vitu hivi ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
6 Si por casualidad ves un lugar que un ave se ha forjado en un árbol o en la tierra, con crías o huevos, y la ave madre sentada sobre los polluelos o sobre los huevos, no tomes la madre ave con los polluelos.
Iwapo kiota cha ndege kikaonekana barabarani mbele yako, kwenye mti wowote au juu ya ardhi, kikiwa na makinda ya ndege au mayai ndani mwake, na mama yao akiwa juu yao au juu ya mayai, haupaswi kumchukua mama pamoja na makinda au mayai yake.
7 Fíjate de dejar ir a la madre pájaro, pero a los polluelos puedes tomar; Así te irá bien y tendrás una larga vida.
Hakika unapaswa kumuacha mama aende zake, ila makinda yake unaweza kuyachukua. Tii amri hii ili uenende vyema, na siku zako ziweze kurefushwa.
8 Si estás construyendo una casa, haz una barandilla para el techo, de modo que no se culpe a la familia de muerte si alguien cae de la azotea.
Ujengapo nyumba mpya, basi unapaswa kujenga kitalu kwa ajili ya paa yako ili usilete damu juu ya nyumba yako mtu akianguka kutoka pale.
9 No haga que su jardín de viñas tenga dos tipos de semillas: o todo puede convertirse en una pérdida, la semilla que sembraron, así como el viñedo.
Haupaswi kupanda shamba lako la mizabibu kwa mbegu mbili, ili kwamba mavuno yote yasichukuliwe na sehemu takatifu, mbegu uliyoipanda pamoja na matunda ya mzabibu.
10 No hagas el arado con un buey y un asno juntos.
Haupaswi kulimia ng’ombe na punda kwa pamoja.
11 No lleve ropa hecha de dos tipos de hilo, lana y lino juntos.
Haupaswi kuvaa kitambaa kilichotengenezwa kwa sufu na kitani kwa pamoja.
12 En los cuatro bordes de tu túnica, con los que está cubierto tu cuerpo, coloca adornos de hilos retorcidos.
Unapaswa kutengeneza pindo katika pembe nne za nguo unayoivaa.
13 Si un hombre toma esposa y ha tenido relaciones sexuales con ella, y después la aborrece.
Iwapo mwanamume kachukua mke, kisha kalala naye, na baadae kumchukia,
14 Y dice cosas malas sobre ella y le da mala fama, diciendo: Tomé a esta mujer, y cuando tuve contacto con ella me quedó claro que no era virgen.
na kisha kumtuhumu kwa vitu vya aibu na kumharibia sifa yake kwa kusema, “Nilimchukua huyu mwanamke, lakini nilipomkaribia sikukuta ushahidi waubikra kwake”.
15 Luego, que el padre y la madre de la niña pongan delante de los hombres responsables del pueblo, en el lugar público, señales de que la niña era virgen:
Kisha baba na mama mzazi wa binti wanatakiwa kupeleka ushahidi wa ubikra wake kwa wazee mlangoni mwa mji.
16 Y que el padre de la niña diga a los hombres responsables, le di mi hija a este hombre por su esposa, pero él no la ama;
Baba wa binti anapaswa kuwaambia wazee, “nilimpatia binti yangu kwa mwanamume huyu awe mkewe, naye anamchukia.
17 Ahora él la ha avergonzado, diciendo que no es virgen; Pero aquí está la señal de que ella es virgen. Luego deben poner su ropa delante de los hombres responsables del pueblo.
Tazama, amemtuhumu na vitu vya aibu na kusema, “Sikukuta ushahidi wa ubikra kwa binti yako”. Lakini ushahidi huu hapa wa ubikra wa binti yangu”. Kisha watatandaza shuka mbele ya wazee wa mji.
18 Entonces los hombres responsables del pueblo deben darle al hombre su castigo;
Wazee wa mji wanapaswa kumchukua mwanamume huyo na kumuadhibu;
19 Lo multarán cien siclos de plata, que le serán entregados al padre de la niña, porque le ha dado un mal nombre a una virgen de Israel: ella seguirá siendo su esposa. Mientras viva él, no podrá divorciarse de ella.
nao wanapaswa kumtoza faini ya shekeli mia moja ya fedha, na kumpatia baba wa binti, kwa sababu mwanamume kasababisha sifa mbaya kwa bikra wa Israeli. Binti huyu anapaswa kuwa mke wake; mwanamume huyu hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote.
20 Pero si lo que él ha dicho es cierto, y se ve que ella no es virgen,
Ila kama jambo hili ni la kweli, kwamba ushahidi wa bikra ya binti haukupatikana,
21 Luego deben hacer que la niña venga a la puerta de la casa de su padre y los hombres del pueblo la apedrearán hasta morir, porque ha hecho el mal y ha avergonzado a Israel, prostituyéndose en la casa de su padre, así que debes quitar el mal de en medio de ti.
basi wanapaswa kumpeleka binti mlangoni kwa baba yake, na kisha wanamume wa mji wake wanatakiwa kumpiga kwa mawe hadi afe, kwa sababu amefanya jambo la aibu katika Israeli, kwa kutenda kama kahaba chini ya nyumba ya baba yake, nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu.
22 Si un hombre es tomado en el acto de ir a una mujer casada, los dos, el hombre y la mujer, deben ser condenados a muerte, por lo tanto, debe deshacerse del mal que haya en medio de Israel.
Iwapo mwanamume kakutwa analala na mwanamke ambaye ni mke wa mtu, basi wote wanapaswa kufa, mwanamume aliyelala na mwanamke pamoja na mwanamke mwenyewe; nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu.
23 Si una joven virgen ha dado su palabra para casarse con un hombre, y otro hombre que se encuentra con ella en el pueblo, se acuesta con ella;
Iwapo kuna msichana bikra, ambaye amechumbiwa na mwanamume, kisha mwanamume mwingine kamkuta mjini na kulala naye,
24 Luego debes llevarlos a la puerta de la ciudad y llevarlos ante el tribunal; la joven virgen, porque ella no gritó pidiendo ayuda, aunque estaba en la ciudad, y el hombre, porque ha avergonzado a la esposa de su vecino: así que debes quitar el mal de en medio de ti.
wachukueni wote wawili malangoni mwa mji, na kuwapiga mawe. Unapaswa kumpiga msichana mawe, kwa sababu hakupaza sauti kuomba msaada, ingawa alikuwa ndani ya mji. Unapaswa kumpiga mwanamume mawe, kwa sababu amemwingilia mke wa jirani yake; nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu
25 Pero si el hombre, encontrándose con una virgen así en el campo, la toma por la fuerza, entonces solo el hombre debe ser condenado a muerte;
Lakini kama mwanamume amemkuta msichana aliyechumbiwa shambani, na kama akamkamata na kulala naye, basi mwanamume pekee aliyelala naye ndiye lazima afe.
26 No se debe hacer nada a la virgen, porque no hay causa de muerte en ella: es lo mismo que si un hombre atacara a su prójimo y lo matara:
Lakini kwake msichana msifanye chochote; hakuna dhambi inayostahili kifo kwake msichana. Kwa maana suala hili ni kama mwanamume amshambuliapo jirani yake na kumuua.
27 Porque él la encontró en el campo abierto, y no había nadie para ayudar a la virgen en respuesta a su clamor.
Kwa maana alimkuta shambani; msichana huyu aliyechumbiwa alipaza sauti, lakini hapakuwa na mtu wa kumuokoa.
28 Si un hombre ve a una joven virgen que no ha dado su palabra de casarse con nadie, y la toma por la fuerza y ​​se acuesta con ella, y son descubiertos;
Iwapo mwanamume amemkuta msichana ambaye ni bikra lakini hajachumbiwa, na kama akamkamata na kulala naye, na kama wakagundulika,
29 Entonces el hombre tendrá que dar al padre de la virgen cincuenta siclos de plata y convertirla en su esposa, porque la ha violado; Él nunca podrá divorciarse de ella en toda su vida.
basi mwanamume aliyelala naye lazima atoe shekeli hamsini za fedha kwa baba wa msichana, naye lazima awe mke wake, kwa sababu amemdhalilisha. Hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote.
30 Un hombre no puede tomar a la esposa de su padre o tener relaciones sexuales con una mujer que es de su padre.
Mwanamume hapaswi kumchukua mke wa baba yake kama wake; hatakiwi kuchukua haki za ndoa za baba yake.

< Deuteronomio 22 >