< Colosenses 4 >
1 Maestros, denle a sus siervos justicia y equidad, conscientes de que tienen un Maestro en el cielo.
Ninyi mabwana, watendeeni watumwa wenu yaliyo haki na yanayostahili, mkitambua ya kwamba ninyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 Perseveren a orar en todo momento, velando con acción de gracias;
Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru.
3 Y haciendo oración por nosotros, para que Dios nos dé una puerta abierta para la predicación de la palabra, el misterio de Cristo, por el cual estoy ahora encadenado;
Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena, ili tupate kuitangaza siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake pia mimi nimefungwa.
4 Para que pueda dejarlo en claro, como debo hacerlo.
Ombeni ili nipate kuitangaza Injili kwa udhahiri kama ipasavyo kunena.
5 Sean prudentes en su comportamiento con los que están afuera, haciendo un buen uso del tiempo.
Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.
6 Deje que su charla sea con gracia, mezclada con sal, para que pueda dar una respuesta a todos.
Maneno yenu yawe yamejaa neema siku zote, yanayofaa, ili mjue jinsi iwapasavyo na inavyofaa kumjibu kila mtu.
7 Tíquico te dará noticias de todos mis asuntos: es un hermano querido y verdadero siervo y ayudador en la palabra;
Tikiko atawaambia habari zangu zote. Yeye ni ndugu mpendwa, mtendakazi mwaminifu na mtumishi mwenzangu katika Bwana.
8 Y se los lo he enviado para este fin, para que tengan noticias de cómo somos, y para que él les dé consuelo a su corazón;
Nimemtuma kwenu kwa madhumuni haya ili mpate kufahamu hali yetu, na pia awatie moyo.
9 Y con él he enviado a Onésimo, el verdadero y querido hermano, que es uno de ustedes. Ellos les darán noticias de todo lo que está sucediendo aquí.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa na mwaminifu, ambaye ni mmoja wenu. Watawaambia mambo yote yanayotendeka hapa kwetu.
10 Aristarco, mi hermano-prisionero, los saluda, y Marcos, un pariente de Bernabé (sobre quien te han dado órdenes: si viene a ustedes sé amable con él),
Aristarko aliye mfungwa pamoja nami anawasalimu, vivyo hivyo Marko, binamu yake Barnaba. (Mmeshapata maagizo yanayomhusu; akija kwenu, mpokeeni.)
11 Y Jesús, cuyo otro nombre es Justo; estos son de la circuncisión: son mis únicos hermanos trabajadores para el reino de Dios, que me han consolado.
Yesu, yeye aitwaye Yusto, pia anawasalimu. Hawa peke yao ndio Wayahudi miongoni mwa watendakazi wenzangu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, nao wamekuwa faraja kwangu.
12 Epafras, que es uno de ustedes, un siervo de Cristo Jesús, les envía saludos, siempre pensando en ustedes en sus oraciones, para que puedan estén firmes y completamente seguros de todo el propósito de Dios.
Epafra, ambaye ni mmoja wenu na mtumishi wa Kristo Yesu, anawasalimu. Yeye siku zote anawaombea kwa bidii kwamba msimame imara katika mapenzi yote ya Mungu, mkiwa wakamilifu na thabiti.
13 Porque doy testimonio de él, que él se ha angustiado mucho por ustedes y por los que están en Laodicea y en Hierápolis.
Ninashuhudia kumhusu kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, na kwa ajili ya ndugu wa Laodikia na wale wa Hierapoli.
14 Lucas, nuestro querido amigo médico, y Demas, les envían saludos.
Rafiki yetu mpenzi Luka yule tabibu, pamoja na Dema, wanawasalimu.
15 Dale mi amor a los hermanos en Laodicea y a Ninfas y la iglesia que está en su casa.
Wasalimuni ndugu wote wa Laodikia, na pia Nimfa, pamoja na kanisa linalokutana katika nyumba yake.
16 Y cuando esta carta se haya hecho pública entre ustedes, que se haga lo mismo en la iglesia de Laodicea; y ustedes a su vez lean la carta que les llega de allá.
Baada ya barua hii kusomwa kwenu, hakikisheni kwamba inasomwa pia katika kanisa la Walaodikia. Nanyi pia msome barua inayotoka Laodikia.
17 Di a Arquipo: Mira que hagas la obra que el Señor te ha encomendado.
Mwambieni Arkipo hivi: “Hakikisha kuwa unakamilisha ile huduma uliyopokea katika Bwana.”
18 Yo, Pablo, te doy esta palabra de amor en mi letra. Mantengan en memoria que soy un prisionero. La gracia sea con ustedes.
Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Kumbukeni minyororo yangu. Neema iwe nanyi. Amen.