< Colosenses 2 >
1 Porque quiero que sepan del gran conflicto que tengo por ustedes y para aquellos en Laodicea, y por todos los que no han visto mi rostro en la carne;
Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi.
2 Para que sus corazones se consuelen, y para que se reúnan en amor, lleguen a la plenitud del conocimiento cierto del secreto de Dios, Cristo mismo,
Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe,
3 En quienes están todos los depósitos secretos de sabiduría y conocimiento.
ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.
4 Digo esto para que nadie los engañe con palabras persuasivas.
Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi.
5 Porque aunque no estoy presente en la carne, aún estoy con ustedes en espíritu, viendo con gozo su orden y su fe inmutable en Cristo.
Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.
6 Que ha llegado a ustedes, así como en todo el mundo está dando fruto constantemente y creciendo, así lo ha estado haciendo también entre ustedes, desde él día que oyeron y comprendieron la gracia De Dios en verdad.
Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake,
7 Arraigados y unidos en él, fuertes en la fe que la enseñanza les dio, alabando a Dios en todo momento.
mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.
8 Cuídate de que nadie los engañe, por la sabiduría y el engaño del hombre, siguiendo las creencias de los hombres y las teorías del mundo, y no según Cristo:
Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.
9 Porque en Cristo toda la plenitud del ser de Dios tiene una forma viviente,
Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu,
10 Y ustedes están completos en él, porque están unidos a Cristo que es la cabeza de todos los seres espirituales que tienen poder y autoridad:
nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka.
11 En el cual tuviste una circuncisión no hecha con manos, en la posposición del cuerpo de la carne, sino con la que consiste en ser librados de la naturaleza pecadora, en la circuncisión de Cristo;
Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo,
12 Habiendo sido muertos con él en el bautismo, con el cual resucitaron con él, por la fe en la obra de Dios, que lo hizo volver de entre los muertos.
mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
13 Y ustedes, estaban muertos espiritualmente por sus pecados, en otro tiempo, y por no haber sido circuncidados; él dio vida juntamente con él, y el perdón de todos nuestros pecados;
Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote,
14 Habiendo puesto fin a la letra de la ley que estaba contra nosotros, que nos obligaba con sus requisitos legales, clavándola en la cruz;
akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake.
15 Por medio de Cristo Dios venció a los seres espirituales que tienen poder y autoridad, y los humilló públicamente llevándolos como prisioneros en su desfile victorioso.
Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.
16 Por lo cual, nadie los juzgue en lo que se refiere a comida, bebida o fiesta, ni a lunas nuevas, ni a sábados;
Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato.
17 Porque esto es solo la sombra de lo que ha de venir; pero el cuerpo es de Cristo.
Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo.
18 Que nadie les quite su recompensa deleitándose en la humildad falsa de sí mismo, y adorando a los ángeles; basándose en las cosas que ha visto, siendo envanecido sin causa en su mente carnal,
Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu.
19 Y no unidos a la Cabeza, de quien todo el cuerpo, dotado de fuerza y mantenido unido a través de sus coyunturas y ligamentos, tiene su crecimiento conforme al plan de Dios.
Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.
20 Si fuiste hecho libre, por tu muerte con Cristo, de las reglas del mundo, ¿por qué te pones bajo la autoridad de las órdenes?
Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri:
21 Que dicen que no puedes tocar, no comas aquello o tomes eso en tus manos,
“Msishike! Msionje! Msiguse!”?
22 (Reglas que terminan con su uso) después de las órdenes y la enseñanza de los hombres?
Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu.
23 Estas cosas parecen tener una especie de sabiduría en la adoración y culto voluntario, humildad, y ser cruel con el cuerpo, pero no tienen valor alguno contra los apetitos de la carne.
Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.