< 2 Samuel 13 >

1 Después de esto, se supo que Absalón, el hijo de David, tenía una hermosa hermana, cuyo nombre era Tamar; y el hijo de David, Amnón, estaba enamorado de ella.
Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
2 Y estaba tan profundamente enamorado que se enfermó a causa de su hermana Tamar; porque ella era virgen, por lo que a Amnón le resultaba difícil hacerle algo.
Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
3 Pero Amnón tenía un amigo que se llamaba Jonadab, el hijo de Simea, el hermano de David: y Jonadab era un hombre muy sabio.
Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
4 Y él le dijo: Oh hijo del rey, ¿por qué te debilitas cada día? ¿No dirás cuál es tu problema? Y Amnón le dijo: Estoy enamorado de Tamar, la hermana de mi hermano Absalón.
Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
5 Entonces Jonadab le dijo: Ve a tu cama y que parezca que estás enfermo. Y cuando tu padre venga a verte, dile: Deja que venga mi hermana Tamar, y prepare la comida delante de mí, para que pueda verla y comerla de su mano.
Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
6 Entonces, Amnón se acostó y se puso enfermo: y cuando el rey fue a verlo, Amnón le dijo al rey: Por favor, que mi hermana Tamar venga y me prepare uno o dos pasteles delante de mis ojos, para que Puedo tomar comida de su mano.
Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
7 Luego, David envió a la casa a buscar a Tamar y le dijo: Ve ahora a la casa de tu hermano Amnón y consigue una comida para él.
Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
8 Entonces Tamar fue a la casa de su hermano Amnón; y él estaba en la cama. Y ella tomó pasta e hizo pasteles ante sus ojos, cocinándolos sobre el fuego.
Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
9 Entonces ella tomó la olla y puso los pasteles delante de él, pero él no los tomó. Y Amnón dijo: Deja que todos se vayan de mí. Así que todos salieron.
Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
10 Entonces Amnón dijo a Tamar: Toma la comida y entra en mi habitación, para que pueda tomarla de tu mano. Así que Tamar tomó los pasteles que había hecho y se fue con ellos al dormitorio de su hermano Amnón.
Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
11 Cuando ella los tomó para dárselos, él la abrazó y le dijo: Ven a la cama, hermana mía.
Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
12 Respondiendo, ella dijo: Oh hermano mío, no me avergüences; no está bien que se haga algo así en Israel. No hagas tal infamia.
Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
13 ¿Qué será de mí en mi vergüenza? y en cuanto a ti, serás despreciable por todo Israel. Ahora, ve y haz tu pedido al rey, porque él no me alejará de ti.
Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
14 Pero él no le prestaría atención a lo que ella decía, pero siendo más fuerte que ella, la tomó por la fuerza y la violó.
Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
15 Entonces Amnón estaba lleno de odio por ella, odiándola con un odio más grande que su amor anterior por ella. Y él le dijo: Levántate y vete.
Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
16 Y ella le dijo: No es así, hermano mío, porque este gran error al despedirme es peor que lo que me hiciste antes. Pero él no le prestó atención.
Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
17 Entonces dio un grito al siervo que lo estaba esperando y le dijo: Saca a esta mujer y que la puerta quede cerrada con llave.
Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
18 Ahora tenía puesta una túnica larga, como en tiempos pasados que vestían las hijas vírgenes del rey. Entonces el criado la sacó, cerrando la puerta con llave.
Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
19 Y Tamar, en su dolor, puso polvo sobre su cabeza; y ella puso su mano en su cabeza y se fue llorando a gritos.
Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
20 Y su hermano Absalón le dijo: ¿Ha estado tu hermano Amnón contigo? Pero ahora, deja que termine tu llanto, hermana mía, él es tu hermano, no te tomes esto en serio. Entonces Tamar siguió viviendo devastada en la casa de su hermano Absalón.
Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
21 Pero cuando el rey David tuvo noticias de todas estas cosas, se enojó mucho; pero no causó problemas a su hijo Amnón, porque era querido por David, siendo su hijo mayor.
Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
22 Pero Absalón no le dijo nada a su hermano Amnón, ni bueno ni malo: porque estaba lleno de odio por él, porque se había llevado a su hermana Tamar por la fuerza.
Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
23 Después de dos años completos, Absalón hizo que los hombres cortaran la lana de sus ovejas en Baal Hazor, que está cerca de Efraín, e invitó todos los hijos del rey a su banquete.
Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
24 Entonces Absalón se acercó al rey y le dijo: Mira, mis siervos están cortando la lana de sus ovejas; ¿Se complacerá el rey y sus siervos acompañarme?
Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
25 Y el rey dijo a Absalón: No, hijo mío, no vamos todos, o el número será demasiado grande para ti. E hizo nuevamente su petición, pero no quiso ir, pero le dio su bendición.
Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
26 Entonces Absalón dijo: Si no quieres ir, deja que mi hermano Amnón vaya con nosotros. Y el rey le dijo: ¿Hay alguna razón para que vaya contigo?
Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
27 Pero Absalón siguió pidiéndole hasta que dejó que Amnón y todos los hijos del rey lo acompañaran. Y Absalón hizo una gran fiesta como una fiesta para un rey.
Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
28 Ahora Absalón había dado órdenes a sus sirvientes, diciendo: Ahora, tomen nota cuando el corazón de Amnón se alegra con el vino; y cuando les diga: ataca a Amnón, mátalo sin miedo: ¿no te he dado órdenes? Séan fuertes y valientes.
Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
29 Así que los sirvientes de Absalón hicieron con Amnón como Absalón les había dado órdenes. Entonces todos los hijos del rey se levantaron, y todos los hombres se subieron a su mula y salieron huyendo.
Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
30 Ahora, mientras iban en camino, se le dio a David la noticia de que Absalón había dado muerte a todos los hijos del rey y que ninguno de ellos aún vivía.
Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
31 Entonces el rey se levantó con gran dolor, tendiéndose sobre la tierra; y todos sus siervos estaban a su lado, con sus ropas rasgadas.
Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
32 Y Jonadab, el hijo de Simea, hermano de David, dijo: No se dé a mi señor la idea de que todos los hijos del rey han sido ejecutados; porque sólo Amnón ha muerto: esto lo propuso Absalom desde el día en que tomó a su hermana Tamar por la fuerza.
Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
33 Así que ahora, no permita que mi señor el rey tome esto en serio, con la idea de que todos los hijos del rey están muertos, porque sólo Amnón está muerto.
Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
34 Pero Absalón salió huyendo. Y el joven que vigilaba, alzando los ojos, vio que una gran banda de personas bajaba la pendiente por el camino que estaba a sus espaldas; y el vigilante se acercó y le dijo al rey, diciendo: Vi a hombres que bajaban por el camino, desde la ladera.
Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
35 Y Jonadab dijo al rey: Mira, vienen los hijos del rey; Como dijo tu siervo, así es.
Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
36 Y mientras él hablaba, los hijos del rey vinieron, llorando y gritando: y el rey y todos sus siervos lloraron amargamente.
Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
37 Entonces Absalón salió huyendo y vino a Talmai, el hijo de Amiud, el rey de Gesur, donde estuvo durante tres años.
Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
38 Y el rey estaba sufriendo por su hijo todo el tiempo.
Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
39 Y el corazón de David deseaba ver a Absalón, pues ya había sido consolado por la muerte de Amnón.
Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.

< 2 Samuel 13 >