< 2 Samuel 11 >

1 Ahora en la primavera, cuando los reyes salen a la guerra, David envió a Joab y sus siervos y todo Israel con él; y destruyeron la tierra de los hijos de Amón, y tomaron su posición ante Rabá, sitiaron. Pero David se quedó en Jerusalén.
Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
2 Una tarde, David se levantó de su cama y, mientras caminaba por el techo de la casa del rey, vio a una mujer bañándose; Y la mujer era muy hermosa.
Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
3 Y David envió a averiguar quién era la mujer. Y uno dijo: ¿No es ésta Betsabé, la hija de Eliam, la esposa de Urías, el hitita?
naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
4 Entonces David la envió y la tomó; y ella vino a él, y él la llevó a su cama. Después de que se purificó de su inmundicia; luego regresó a su casa.
Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Y la mujer quedó embarazada. y ella le dijo a David que estaba embarazada.
Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
6 Entonces envió David a Joab, diciendo: Envíame a Urías el hitita. Y Joab envió a Urías a David.
Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
7 Y cuando Urías se acercó a él, David le hizo preguntas sobre cómo era Joab y el pueblo, y cómo iba la guerra.
Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
8 Entonces David dijo a Urías: Baja a tu casa, y lava tus pies. Y Urías se fue de la casa del rey, y una ofrenda del rey fue enviada tras él.
Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
9 Pero Urías tomó su descanso en la puerta de la casa del rey, con todos los siervos de su señor, y no bajó a su casa.
Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
10 Y cuando se le dijo a David que Urías no había bajado a su casa, David le dijo a Urías, ¿No has venido de un viaje? ¿Por qué no fuiste a tu casa?
Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
11 Y Urías dijo a David: Israel y Judá con el arca viven en tiendas, y mi señor Joab y los otros siervos de mi señor duermen en campo abierto; ¿Debo ir a mi casa y comer y beber, y acostarme con mi esposa? Por el Señor vivo, y por la vida de tu alma, no haré tal cosa.
Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
12 Entonces David dijo a Urías: Estate aquí hoy, y después de eso te dejaré ir. Entonces Urías estuvo en Jerusalén ese día y el siguiente.
Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
13 Y enviándole David, David comió y bebió, y David logró emborracharlo. Y al caer la noche, se fue a descansar en su cama con los criados de su señor, pero él No bajó a su casa.
Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
14 A la mañana siguiente, David le dio a Urías una carta para llevar a Joab.
Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
15 Y en la carta dijo: Ten cuidado de poner a Urías en el frente de la línea, donde la lucha es más violenta, y déjenlo solo, para que pueda ser vencido y condenado a muerte.
Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
16 Entonces, mientras Joab observaba la ciudad, puso a Urías en el lugar donde estaba claro para él que eran los mejores guerreros.
Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
17 Salieron los hombres de la ciudad y se pelearon con Joab; y varios de los hombres de David murieron en la lucha, y con ellos Urías el hitita.
Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
18 Entonces Joab envió a David noticias de todo lo que había ocurrido en la guerra:
Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
19 Y dio órdenes al hombre que recibió la noticia, diciendo: Después de que le hayas dado al rey todas las noticias sobre la guerra,
Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
20 Si el rey está enojado y dice: ¿Por qué te acercaste tanto al pueblo para pelear? ¿No era cierto que sus arqueros estarían en la pared?
hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
21 ¿Quién mató a Abimelec, hijo de Jerobaal? ¿Acaso una mujer no le arrojó una gran piedra desde la pared y lo mató en Thebez? ¿Por qué te acercaste tanto a la pared? Entonces dile: Tu siervo Urías el hitita está entre los muertos.
Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
22 Entonces el hombre fue y vino a David, y le dio todas las noticias que Joab le había enviado para dar; luego David se enojó con Joab y dijo: ¿Por qué te acercaste tanto a la ciudad para la pelea? ¿No era cierto que sus arqueros estarían en la pared? ¿Quién mató a Abimelec, el hijo de Jerobaal? ¿Acaso una mujer no le arrojó una gran piedra desde la pared y lo mató en Thebez? ¿Por qué te acercaste tanto a la pared?
Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
23 Y el hombre dijo a David: En verdad, los hombres nos vencieron y salieron contra nosotros al campo abierto, pero los enviamos de regreso a las mismas puertas del pueblo.
Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
24 Y los arqueros enviaron sus flechas a tus siervos desde el muro, y algunos de los siervos del rey murieron, y entre ellos está tu siervo Urías el hitita.
Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
25 Entonces David dijo al hombre: Ve y dile a Joab: No permitas que esto te cause pena; porque un hombre puede llegar a su muerte por la espada como otro: lucha aún más fuerte contra la ciudad, y tomarla: y anímalo.
Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
26 Y cuando la esposa de Urías tuvo noticias de que su esposo había muerto, ella se entregó a llorar por él.
Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
27 Y cuando pasaron los días de llanto, David la llamó y la llevó a su casa, y ella se convirtió en su esposa y le dio un hijo. Pero el Señor no estaba complacido con lo que David había hecho.
Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.

< 2 Samuel 11 >