< 2 Reyes 13 >

1 En el año veintitrés de Joás, hijo de Ocozías, rey de Judá, Joacaz, hijo de Jehú, se convirtió en rey de Israel en Samaria, y gobernó durante diecisiete años.
Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
2 Hizo lo malo ante los ojos del Señor, copiando los pecados de Jeroboam, el hijo de Nebat, lo que hizo e hizo que Israel hiciera; no se apartó de ellos.
Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
3 Entonces la ira del Señor se encendió contra Israel, y los entregó al poder de Hazael, rey de Siria, y al poder de Benadad, el hijo de Hazael, una y otra vez.
Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
4 Entonces Joacaz oró al Señor, y el Señor le escuchó, porque vio cuán cruelmente oprimido era Israel por el rey de Siria.
Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
5 Y el Señor le dio a Israel un salvador, para que se liberaran de las manos de los sirios, y los hijos de Israel vivían en sus tiendas como en el pasado.
Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
6 Pero aun así no abandonaron el pecado de Jeroboam, lo que hizo que Israel hiciera, sino que continuaron con él; y había una imagen de Asera en Samaria.
Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
7 Porque de todo su ejército, Joacaz tenía sólo cincuenta jinetes y diez carruajes y diez mil soldados de infantería; el rey de Siria los había entregado a la destrucción, y hecho polvo.
Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
8 Los demás hechos de Joacaz, y todo lo que hizo, y su gran poder, ¿no están registrados en el libro de las crónicas de los reyes de Israel?
Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
9 Y Joacaz durmió con sus padres, y fue enterrado en Samaria; y su hijo Joás se convirtió en rey en su lugar.
Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
10 En el año treinta y siete del gobierno de Joás, rey de Judá, Joás, hijo de Joacaz, se convirtió en rey de Israel en Samaria, y gobernó durante dieciséis años.
Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
11 Hizo lo malo ante los ojos del Señor, sin apartarse del pecado de Jeroboam, el hijo de Nabat, que hizo pecar a Israel, y siguió adelante pecando.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
12 El resto de los hechos de Joás, y todo lo que hizo, y la fuerza con que fue a la guerra contra Amasías, rey de Judá, no están registrados en el libro de las crónicas de los reyes de Israel?
Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
13 Y Joás durmió con sus padres, y Jeroboam tomó su lugar como rey; y Joás fue enterrado en Samaria con los reyes de Israel.
Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
14 Entonces Eliseo se enfermó con la enfermedad que causó su muerte y descendió a él Joás, rey de Israel, y llorando sobre él, dijo: Mi padre, mi padre, los carros de Israel y sus jinetes.
Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
15 Entonces Eliseo le dijo: Toma arco y flechas, y él tomó arco y flechas.
Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
16 Entonces dijo al rey de Israel: Pon tu mano sobre el arco, y él puso su mano sobre él. y Eliseo puso sus manos sobre las manos del rey.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
17 Entonces dijo: Que la ventana se abra hacia el este: y la abrió. Entonces Eliseo dijo: Deja ir la flecha; y lo dejó ir. Y él dijo: La flecha de salvación del Señor, de la salvación contra Siria; porque vencerás a los sirios en Afec y les pondrás fin.
Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
18 Y él dijo: Toma las flechas, y él las tomó. Y dijo al rey de Israel: Envíalos a la tierra; Y lo hizo tres veces y no más.
Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
19 Entonces el hombre de Dios se enojó con él y le dijo: Si lo hubieras hecho cinco o seis veces, habrías vencido a Siria completamente; Pero ahora solo los superarás tres veces.
Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
20 Y vino la muerte a Eliseo, y lo enterraron. Ahora, en la primavera del año, las bandas armadas de moabitas venían con frecuencia, invadiendo la tierra.
Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
21 Y mientras estaban sepultando a un hombre, vieron venir una banda; y pusieron al hombre rápidamente en el lugar donde estaba el cuerpo de Eliseo; y el hombre muerto, al tocar los huesos de Elisea, volvió a la vida y se puso de pie.
Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
22 E Israel fue oprimido bajo el poder de Hazael, rey de Siria, todos los días de Joacaz.
Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
23 Pero el Señor fue amable con ellos y tuvo compasión de ellos, cuidándolos, debido a su acuerdo con Abraham, Isaac y Jacob; no los destruiría ni los enviaría lejos de su rostro hasta ahora.
Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
24 Entonces Hazael, rey de Siria, llegó a su fin; y Ben-adad su hijo se convirtió en rey en su lugar.
Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Y Joás, el hijo de Joacaz, volvió a tomar de Ben-adad, el hijo de Hazael, las ciudades que había tomado de Joacaz su padre en la guerra. Tres veces Joás lo venció y volvió a los pueblos de Israel.
Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.

< 2 Reyes 13 >