< 2 Reyes 11 >
1 Cuando Atalía, la madre de Ocozías, vio que su hijo estaba muerto, ella hizo que todo el resto de la simiente del reino fuera muerto.
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme.
2 Más Josaba, la hija del rey Joram, hermana de Ocozías, tomó en secreto a Joás, hijo de Ocozías, con la mujer que lo cuidaba, lejos de entre los hijos del rey que fueron ejecutados, y él y la nodriza se escondieron en el dormitorio; y lo mantuvieron a salvo de Atalía, para que no fuera condenado a muerte.
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, aliyekuwa pia dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa.
3 Y por seis años lo mantuvo a salvo en la casa del Señor, mientras Atalía estaba gobernando la tierra.
Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake katika Hekalu la Bwana kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
4 Luego, en el séptimo año, Joiada mandó llamar a los capitanes de cientos de cereteos hombres armados, y llevándolos a la casa del Señor, hizo un acuerdo con ellos y les hizo prestar juramento la casa del Señor, y les mostró al hijo del rey.
Katika mwaka wa saba, Yehoyada akatumania wakuu wa vikundi vya mamia, na Wakari, na walinzi, nao wakaletwa kwake katika Hekalu la Bwana. Alifanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu la Bwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme.
5 Y les dio órdenes, diciendo: Esto es lo que deben hacer: la tercera parte de ustedes, vigile la casa del rey el día de reposo, el sábado,
Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaoingia zamu siku ya Sabato, theluthi yenu inayolinda jumba la kifalme,
6 Otra tercera parte estaré en el Sur, y la otra tercera parte parte en la puerta posterior del cuartel de la guardia. Así cubrirán ustedes por turnos la guardia del palacio.
theluthi nyingine Lango la Suri, na theluthi nyingine lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu,
7 Y las dos divisiones de ustedes, que salen el sábado y vigilan el templo del Señor junto al rey.
nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme.
8 Harán un círculo alrededor del rey, cada uno de los hombres armados; y el que entre dentro de tus líneas ha de ser muerto; acompañarán al rey, cuando sale y cuando entra.
Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi. Yeyote anayesogelea safu zenu lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
9 Y los capitanes de centenares hicieron como el sacerdote Joiada les dio órdenes; Todos tomaron con él a sus hombres, los que entraron y los que salieron el sábado, y se presentaron al sacerdote Joiada.
Wakuu wa vikosi vya mamia wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada.
10 Y el sacerdote dio a los capitanes de centenares las lanzas y escudos que habían sido del rey David, y que se guardaban en la casa del Señor.
Ndipo akawapa wale wakuu mikuki na ngao zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana.
11 Entonces los hombres armados tomaron sus posiciones, cada uno con sus instrumentos de guerra en la mano, desde el lado derecho de la casa hacia la izquierda, alrededor del altar y la casa.
Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
12 Luego sacó al hijo del rey, puso la corona sobre él y los brazaletes, y lo hizo rey, y puso aceite santo sobre él. y todos ellos, haciendo sonidos de alegría con sus manos, dijeron: Larga vida al rey.
Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano, na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
13 Ahora, Atalía, oyendo el ruido hecho por la gente, vino a la gente en el templo del Señor;
Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu la Bwana.
14 Al mirar, vio al rey en su lugar habitual junto a la columna, y los capitanes y los cuernos cerca de él; y toda la gente de la tierra dando señales de alegría y haciendo sonar los cuernos. Entonces Atalía, separando violentamente sus ropas, lanzó un grito, diciendo: ¡Traición!
Akaangalia, na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kulia, “Uhaini! Uhaini!”
15 Entonces el sacerdote Joiada dio órdenes a los que estaban en autoridad sobre el ejército, diciendo: Llévala fuera de las filas, y que cualquiera que la persiga sea condenado a muerte con espada, porque él dijo: No se le dé muerte en la casa del Señor.
Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu la Bwana.”
16 De modo que pusieron sus manos sobre ella, y ella fue a la casa del rey junto a la puerta de los caballos, y allí la mataron.
Basi wakamkamata Athalia, na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamuulia hapo.
17 Y Joiada llegó a un acuerdo entre el Señor, el rey y el pueblo, de que serían el pueblo del Señor; y de la misma manera entre el rey y el pueblo.
Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Bwana na mfalme na watu kwamba watakuwa watu wa Bwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu.
18 Entonces todos los habitantes de la tierra fueron a la casa de Baal y la derribaron, sus altares y sus imágenes se rompieron en pedazos, y Matan, el sacerdote de Baal, lo mataron ante los altares. Y el sacerdote puso supervisores sobre él templo del Señor.
Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu na sanamu, na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu. Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu la Bwana.
19 Luego tomó a los capitanes de cientos, a los cereteos, a los hombres armados y a toda la gente de la región; y descendieron con el rey de la casa del Señor, a través de la puerta de los hombres armados, a la casa del rey. Y él tomó su lugar en el asiento de los reyes.
Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana na kwenda kwenye jumba la mfalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi,
20 Y se alegraron todos los habitantes de la tierra, y el pueblo quedó en silencio; y mataron a Atalía con la espada en la casa del rey.
nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga nyumbani kwa mfalme.
21 Y Joás tenía siete años cuando comenzó a reinar.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.