< 2 Corintios 8 >

1 Y ahora les damos noticias, hermanos, acerca de la gracia de Dios que se ha dado a las iglesias de Macedonia;
Basi sasa ndugu, nataka ninyi mjue kuhusu ile neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia.
2 Mientras estaban pasando por todo tipo de problemas, y estaban en la mayor necesidad, se tomaron la mayor alegría de poder dar libremente a las necesidades de los demás.
Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha waliyokuwa nayo ilikuwa kubwa, ingawa walikuwa maskini kupindukia, kwa upande wao walifurika kwa wingi wa ukarimu.
3 Porque les doy testimonio de que pudieron dar, y aún más de lo que pudieron, de todo corazón de su propia iniciativa,
Kwa maana nashuhudia kwamba wao walitoa kwa kadiri wawezavyo, hata na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe,
4 Rogándonos que pudieran participar en este privilegio de servir y apoyar en las necesidades de los santos:
wakitusihi kwa bidii wapewe fursa ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watakatifu.
5 Y yendo más lejos que nuestra esperanza, primero se entregaron al Señor y a nosotros según el propósito de Dios.
Wala hawakufanya tulivyotazamia, bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwa ajili yetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
6 De modo que pedimos a Tito que, como había comenzado antes, así él podría completar está colecta entre ustedes.
Kwa hiyo tulimsihi Tito, kwa kuwa ndiye alianzisha jambo hili, akamilishe tendo hili la neema kwa upande wenu.
7 Y que como están llenos de todo lo bueno, de fe, de la palabra, de conocimiento, de una mente dispuesta, y de amor para nosotros, así puedan sobresalir en está obra de caridad.
Lakini kama vile mlivyo mbele sana katika yote: Katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika uaminifu wote na katika upendo wenu kwetu sisi, vivyo hivyo tunataka pia mzidi katika neema hii ya kutoa.
8 No te estoy dando una orden, sino usando la mente dispuesta de los demás como una prueba de la sinceridad de su amor.
Siwaamrishi, lakini nataka kujaribu unyofu wa upendo wenu kwa kuulinganisha na bidii ya wengine.
9 Porque tú ves la gracia de nuestro Señor Jesucristo, que aunque tuvo riquezas, se hizo pobre por ustedes, para que por su pobreza tengas riquezas.
Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri.
10 Y en esto doy mi opinión: ya que es para su beneficio, quienes fueron los primeros en comenzar el año anterior, no solo para hacer esto, sino para dejar en claro que sus mentes estaban más que dispuestas a hacerlo.
Ushauri wangu kuhusu lile lililo bora kwenu juu ya jambo hili ni huu: Mwaka uliopita ninyi mlikuwa wa kwanza si tu kutoa lakini pia mlikuwa na shauku ya kufanya hivyo.
11 Ahora haz que se complete; con la misma disposición que mostraron al principio, cuando decidieron hacerlo.
Sasa ikamilisheni kazi hii kwa shauku kama mlivyoanza, jitoleeni kulingana na uwezo wenu.
12 Porque si hay una mente dispuesta, un hombre tendrá la aprobación de Dios en la medida de lo que tiene, y no de lo que no tiene.
Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kulingana na kile mtu alicho nacho, wala si kwa kile ambacho hana.
13 Y no estoy diciendo esto para que otros puedan liberarse de esta carga, mientras que el peso recae sobre ustedes:
Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka, bali pawe na uwiano.
14 Pero para que las cosas sean iguales; que en este tiempo de abundancia sobre ustedes, puedan suplir su necesidad, y que la abundancia de ellos supla la necesidad de ustedes de la misma manera, haciendo las cosas iguales.
Kwa wakati huu, wingi wa vitu mlivyo navyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao watakapokuwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu.
15 Como se dice en la Escritura, el que había recogió mucho, no tuvo más y el que recogió poco, no tuvo escasez.
Ndipo patakuwa na usawa, kama ilivyoandikwa: “Aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”
16 Pero alabado sea Dios, que pone la misma preocupación que yo tengo por ustedes en el corazón de Tito.
Ninamshukuru Mungu ambaye amemtia Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali.
17 Mientras que de buena gana prestó oído a nuestra petición, estaba lo suficientemente interesado en ir a ustedes de su propia voluntad.
Si kwamba Tito amekubali tu ombi letu, bali anakuja kwenu akiwa na shauku kuliko wakati mwingine, tena kwa hiari yake mwenyewe.
18 Y con él hemos enviado un hermano cuya alabanza en las buenas nuevas ha pasado por todas las iglesias;
Nasi tunamtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili.
19 Y no solo eso, sino que fue escogido por las iglesias para ir con nosotros en este acto de caridad, que es administrado por nosotros que hemos emprendido para la gloria del Señor y para dejar en claro su buena voluntad para dar:
Zaidi ya hayo, alichaguliwa na makanisa ili asafiri pamoja nasi tulipokuwa tunapeleka matoleo ya ukarimu, kwa ajili ya utukufu wa Bwana mwenyewe, na ili kuonyesha hisani yetu kuwasaidia.
20 Y para que ningún hombre pueda decirnos algo en contra de nosotros en la administración de esta gran ofrenda que ha sido puesta en nuestras manos:
Tunataka kuepuka lawama yoyote kuhusu jinsi tunavyosimamia matoleo haya ya ukarimu.
21 Y por eso procuramos hacer lo bueno y honesto para tener la aprobación, no solo del Señor, sino de los hombres.
Kwa kuwa tunakusudia kufanya kile kilicho haki si machoni mwa Bwana peke yake, bali pia machoni mwa watu wengine.
22 Y hemos enviado con ellos a nuestro hermano, cuyo entusiasmo de espíritu nos ha sido aclarado a veces y en innumerables momentos, pero ahora lo es aún más debido a la cierta fe que él tiene en ustedes.
Pamoja nao, tunamtuma ndugu yetu ambaye mara kwa mara ametuthibitishia kwa njia nyingi kwamba ana shauku, naam, zaidi sana sasa kwa sababu analo tumaini kuu kwenu.
23 Si surge alguna pregunta sobre Tito, él es mi hermano trabajador, que trabaja conmigo para ustedes o sobre los otros, ellos son los representantes de las iglesias para la gloria de Cristo.
Kwa habari ya Tito, yeye ni mwenzangu na mtendakazi pamoja nami miongoni mwenu. Kwa habari za ndugu zetu, wao ni wawakilishi wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
24 Hazles claro a ellos, como representantes de las iglesias, muéstrales que verdaderamente los aman y que tenemos razón al estar satisfechos de ustedes.
Kwa hiyo waonyesheni wazi hawa ndugu uthibitisho wa upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, mbele ya makanisa, ili yapate kuona.

< 2 Corintios 8 >