< 2 Corintios 13 >
1 Esta es la tercera vez que vengo a ustedes. De la boca de dos o tres testigos, cada palabra tendrá que decidirse.
Hii ndiyo mara ya tatu mimi kuja kwenu. “Shtaka lolote lazima lithibitishwe na mashahidi wawili au watatu.”
2 He dicho antes, y todavía lo digo antes de venir, como estar presente por segunda vez, aunque todavía estoy lejos de ustedes, a los que han pecado antes, y a todos, no les tendré consideración;
Nimekwisha kuwaonya nilipokuwa pamoja nanyi mara ya pili. Sasa narudia wakati sipo, kwamba nikija tena sitawahurumia wale waliokuwa wametenda dhambi hapo awali na wengine wote,
3 Al ver que estás buscando una señal de Cristo de que habla por mí; quien no es débil en relación con usted, pero es poderoso en ustedes:
kwa kuwa mnadai uthibitisho kwamba Kristo anazungumza kwa kunitumia mimi. Yeye si dhaifu katika kushughulika nanyi, bali ana nguvu kati yenu.
4 porque fue crucificado en debilidad, pero está viviendo por el poder de Dios. Y somos débiles en él, pero viviremos con él a través del poder de Dios para servirles a ustedes.
Kwa kuwa alisulubiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Vivyo hivyo, sisi tu dhaifu kupitia kwake, lakini katika kuwashughulikia ninyi tutaishi pamoja naye kwa nguvu za Mungu.
5 Haz una prueba de ustedes mismos, si están en la fe; asegúrense de ustedes mismos ¿O no están conscientes de que Jesucristo está en ustedes, si son verdaderamente de Cristo?
Jichunguzeni wenyewe mwone kama mnaishi katika imani. Jipimeni wenyewe. Je, hamtambui ya kuwa Yesu Kristo yumo ndani yenu? Kama sivyo, basi, mmeshindwa kufikia kipimo hicho!
6 Pero espero que no tengan dudas de que somos verdaderamente de Cristo.
Natumaini mtaona kuwa sisi hatukushindwa.
7 Ahora nuestra oración a Dios es que no hagan mal alguno; no para que pueda ser acreditado a nosotros, sino para que ustedes hagan lo correcto, sea lo que sea que parezcamos.
Lakini tunamwomba Mungu msije mkatenda kosa lolote, si ili sisi tuonekane kuwa tumeshinda hilo jaribio, bali ili ninyi mtende lililo haki, hata kama tutaonekana kuwa tumeshindwa.
8 Porque no podemos hacer nada en contra de lo que es verdadero, sino solo por la verdad.
Kwa maana hatuwezi kufanya lolote kinyume na kweli, bali kuithibitisha kweli tu.
9 Porque nos alegramos cuando somos débiles y ustedes fuertes; y esta es nuestra oración, incluso para que sean perfeccionados.
Tunafurahi wakati wowote sisi tunapokuwa dhaifu, lakini ninyi mkawa na nguvu. Nayo maombi yetu ni kwamba mpate kuwa wakamilifu.
10 Por esta razón escribo estas cosas mientras estoy ausente, de modo que pueda haber necesidad de que, cuando esté presente, haga uso de medidas severas, por la autoridad que el Señor me ha dado para edificar y no para destrucción.
Hii ndiyo sababu nawaandikia mambo haya wakati sipo, ili nikija nisiwe mkali katika kutumia mamlaka yangu, mamlaka Bwana aliyonipa ya kuwajenga ninyi wala si ya kuwabomoa.
11 Que esta sea mi última palabra, hermanos; estén contento; sean perfeccionados; Sean de buen consuelo, sean de la misma mente; estén en paz el uno con el otro; y el Dios de amor y paz estará con ustedes.
Hatimaye, ndugu zangu, kwaherini. Kuweni wakamilifu, mkafarijike, kuweni wa nia moja, kaeni kwa amani. Naye Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
12 Dense unos a otros un beso santo.
Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu.
13 Todos los santos los saludan.
Watakatifu wote wanawasalimu.
14 La gracia de nuestro Señor Jesucristo, y el amor de Dios, y la comunión el Espíritu Santo estén con todos ustedes.
Neema ya Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote. Amen.