< 2 Corintios 11 >
1 Ojalá que me toleren un poco de locura! pero, de verdad, tolérenme.
Laiti mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni kidogo.
2 Porque tengo un gran celo por ustedes: porque es un celo santo pues los he desposado con un solo esposo, y quiero presentarlos como una virgen pura a Cristo.
Ninawaoneeni wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
3 Pero tengo miedo de que, de alguna manera, como Eva fue engañada por el engaño de la serpiente, sus mentes puedan ser apartadas de su amor simple y santo por Cristo.
Lakini naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa, fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
4 Porque si alguno viene a predicar a otro Jesús de aquel cuyos predicadores somos, o si tienen un espíritu diferente, o una clase diferente de buenas nuevas de los que vinieron a ustedes, soportan con gusto estas cosas.
Maana mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa na ile mliyopokea kutoka kwetu!
5 Porque en mi opinión, soy de ninguna manera menos que el más importante de los Apóstoles.
Sidhani kwamba mimi ni mdogo kuliko hao “mitume wakuu.”
6 Pero aunque soy rudo en mi manera de hablar, no lo soy en conocimiento, como hemos aclarado a todos por nuestros actos entre ustedes.
Labda sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi kwenu, kila mahali na kila wakati.
7 ¿O hice mal en humillarme para que puedan ser enaltecidos, porque les di las buenas nuevas de Dios sin cobrarles?
Mimi niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
8 He despojado de dinero a otras iglesias como pago por mi trabajo, para que yo pudiera servirlos a ustedes;
Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine. Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
9 Y cuando estuve presente entre ustedes, y tuve necesidad, no dejé que ningún hombre fuera responsable de mí; porque los hermanos, cuando venían de Macedonia, me dieron todo lo que se necesitaba; y en todo, evité que fuera un problema para ustedes, y continuaré haciéndolo.
Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
10 Como la verdadera palabra de Cristo está en mí, no dejaré que nadie me quite esta mi causa de orgullo en toda la región de Acaya.
Naahidi kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
11 ¿Por qué porque no los amo? Dios sabe que si los quiero.
Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba nawapenda!
12 Pero lo que hago, eso seguiré haciendo, para no dar oportunidad a aquellos que andan buscando pretexto para tener una satisfacción como la nuestra;
Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
13 Porque tales hombres son falsos apóstoles, hacedores de engaño, haciéndose parecer apóstoles de Cristo.
Maana, hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa Kristo.
14 Y no es de extrañar; porque incluso Satanás mismo puede tomar la forma de un ángel de luz.
Wala si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
15 Así que, no se extrañen si sus siervos se hacen parecer siervos de la justicia; cuyo fin será la recompensa de sus obras.
Kwa hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo yao.
16 Digo de nuevo: No me vean como un loco; pero si lo hacen, escúchame como tal, para que pueda tomar un poco de gloria para mí mismo.
Tena nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi, nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
17 Lo que estoy diciendo ahora no es por orden del Señor, sino como una persona tonta, tomándome crédito, como parece.
Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna, nasema tu kama mtu mpumbavu.
18 Al ver que hay quienes se reconocen a sí mismos según la carne, haré lo mismo.
Maadam wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
19 Porque has aguantado de buena gana a los insensatos, siendo sabios.
Ninyi ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
20 Han aguantado a aquellos que los obligan a servir, que los explotan, los hace prisioneros, se enaltece, y les dan golpes en la cara.
Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
21 Digo esto para vergüenza mía, nosotros mismos, hemos sido débiles para portarnos así. Pero si alguien tiene osadía (estoy hablando como una persona tonta), haré lo mismo.
Kwa aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu yeyote anayethubutu kujivunia kitu—nasema kama mtu mpumbavu—mimi nathubutu pia.
22 ¿Son hebreos? Yo también. ¿Son de Israel? Yo también. ¿Son ellos la simiente de Abraham? Yo también.
Je, wao ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa Abrahamu? Hata mimi.
23 ¿Son siervos de Cristo? (Estoy hablando tontamente) Soy más; He tenido más experiencia en el trabajo duro, en las cárceles, en los golpes más que en las medidas, en la muerte.
Wao ni watumishi wa Kristo? Hata mimi—nanena hayo kiwazimu—ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
24 Cinco veces los judíos me dieron cuarenta golpes, pero uno.
Mara tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
25 Tres veces fui azotado con varas, una vez fui apedreado, tres veces el barco en el que estuve fue destruido en el mar, una noche y un día he estado en el agua;
Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
26 En viajes frecuentes, en peligros en ríos, en peligros de bandidos, en peligros de mis compatriotas, en peligros de los gentiles, en peligros en la ciudad, en peligros en el desierto, en peligros en el mar, en peligros entre falsos hermanos;
Kila mara safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama; hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine; hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu wa uongo
27 En trabajo duro y cansancio, en vigilias frecuentes, sin comida y bebida, frío y con necesidad de ropa.
Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
28 Además de todas las otras cosas, está todo lo que sucede todos los días, el cuidado de todas las iglesias.
Na, licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
29 ¿Quién enferma y yo no enfermo? ¿A Quién se le hace tropezar y no estoy enojado?
Kama mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa na wasiwasi.
30 Si tengo que jactarme, lo haré en las cosas en las que soy débil.
Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
31 El Dios y Padre de nuestro Señor Jesucristo, a quien alabado sea para siempre, es testigo de que lo que digo es verdad. (aiōn )
Mungu na Baba wa Bwana Yesu—jina lake litukuzwe milele—yeye anajua kwamba sisemi uongo. (aiōn )
32 En Damasco, el gobernante bajo el rey Aretas vigilaba la ciudad del pueblo de Damasco, para arrestarme.
Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
33 Y siendo descolgado me bajaron en un canasto por una ventana, de la muralla de la ciudad, me liberé de sus manos.
Lakini, ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani, nikachopoka mikononi mwake.