< 2 Crónicas 4 >

1 Luego hizo un altar de bronce de veinte codos de largo, veinte codos de ancho y diez codos de alto.
Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
2 E hizo una gran pila de bronce, de forma redonda, que medía diez codos de borde a borde; tenía cinco codos de alto y treinta codos de circunferencia.
Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
3 Y debajo de él había un diseño de Bueyes a su alrededor, de diez a un codo, que rodeaba el recipiente de agua en dos líneas; estaban fundidos al mismo tiempo que el recipiente de agua.
Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
4 Se apoyaba en doce bueyes, tres orientados hacia el norte, tres hacia el oeste, tres hacia el sur y tres hacia el este, la vasija de agua que descansaba sobre ellos; Sus partes traseras estaban todas giradas hacia el medio.
Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
5 Era tan gruesa como la mano abierta de un hombre, y su borde estaba curvado como el borde de una copa, como una flor de lirio; tomaría tres mil baños.
Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
6 E hizo diez recipientes de lavado, poniendo cinco en el lado derecho y cinco en el izquierdo; las cosas que se usaron para hacer la ofrenda quemada fueron lavadas en ellos; pero los sacerdotes debían usar el gran recipiente de agua para lavarse.
Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
7 E hizo los diez candelabros de oro para las luces, según las instrucciones dadas, y las puso en el Templo, cinco en el lado derecho y cinco en el izquierdo.
Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
8 Hizo diez mesas y las puso en el Templo, cinco en el lado derecho y cinco en el izquierdo. E hizo cien tazones de oro.
Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
9 Luego hizo el atrio para los sacerdotes, y el gran atrio y sus puertas, enchapando las puertas con bronce.
Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
10 Puso la gran vasija de agua en el lado derecho de la casa hacia el este, mirando hacia el sur.
Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
11 Hiram hizo todas las ollas, las palas y los tazones. Entonces llegó al final de todo el trabajo que hizo para el rey Salomón en la casa de Dios:
Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
12 Los dos pilares, y las dos coronas en la parte superior de los pilares, y la rejilla que cubre las dos copas de las coronas en la parte superior de los pilares;
zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
13 Y las cuatrocientas granadas para la rejilla, dos líneas de granadas para la rejilla que cubren las dos copas de las coronas sobre los pilares.
yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
14 E hizo las diez bases y los diez recipientes de lavado que estaban en las bases;
vishikio pamoja na masinia yake;
15 El gran recipiente de agua con los doce bueyes debajo.
hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
16 Todas las ollas y las espadas y los tenedores y sus vasijas, que Hiram, que era como su padre, hizo para el rey Salomón para la casa del Señor, eran de bronce pulido.
pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
17 El rey los hizo de bronce fundido en las tierras bajas de Jordania, en la tierra blanda entre Sucot y Saretan.
Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
18 Así que Salomón hizo todas estas vasijas, una gran cantidad de ellas, y el peso del bronce utilizado no se midió.
Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
19 E hizo Salomón todas las vasijas usadas en la casa de Dios, el altar de oro y las mesas sobre las cuales se colocaba el pan santo,
Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
20 Y los candelabros con sus luces, para arder de manera regular frente al Lugar Santísimo, del mejor oro;
vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
21 Las flores y las vasijas para las luces y los instrumentos utilizados para ellas, eran todos de oro; Fue el mejor oro.
maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
22 Las tijeras y las pilas y las cucharas y los incensarios, del mejor oro; y las puertas interiores del templo, que se abren al Lugar Santísimo, y las puertas del Templo, eran todas de oro.
mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.

< 2 Crónicas 4 >