< 2 Crónicas 31 >

1 Ahora que todo esto había terminado, todos los hombres de Israel que estaban presentes salieron a las ciudades de Judá, causando que los pilares de piedra se rompieran y los pilares de madera representaciones de Asera, derribando los lugares altos y los altares en todo Judá y Benjamín, así como en Efraín y Manasés, hasta que todos se fueron. Entonces todos los hijos de Israel volvieron a sus ciudades, cada uno a su propiedad.
Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
2 Entonces Ezequías puso en orden los turnos de los sacerdotes y levitas, cada uno en su división, en relación con su servicio, por las ofrendas quemadas y las ofrendas de paz, y por la ordenación de la adoración y por alabar a Dios; y sirvieran en las puertas de la casa del Señor.
Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
3 Y le dio al rey parte de su propiedad privada por las ofrendas quemadas, es decir, por las ofrendas de la mañana y de la tarde, y las ofrendas para el sábado y las lunas nuevas y las fiestas regulares, como se registra en la ley del Señor.
Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
4 Además, dio órdenes a la gente de Jerusalén para que les dieran a los sacerdotes y levitas la parte que les pertenecía por derecho, para que pudieran ser fuertes en el cumplimiento de la ley del Señor.
Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
5 Y cuando se hizo pública la orden, los hijos de Israel dieron de inmediato, en grandes cantidades, los primeros frutos de su grano y vino y aceite y miel, y del producto de sus campos; y tomaron en una décima parte de todo, una gran cantidad.
Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
6 Y los hijos de Israel y Judá, que vivían en las ciudades de Judá, vinieron con la décima parte de sus bueyes y ovejas, y una décima parte de todas las cosas consagradas que debían ser dadas al Señor su Dios, y los pusieron por montones.
Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
7 La primera reserva de cosas se dejó en el tercer mes, y en el séptimo mes terminaron.
Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
8 Y cuando Ezequías y los gobernantes vinieron y vieron toda la reserva de bienes, alabaron al Señor y a su pueblo Israel.
Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
9 Entonces Ezequías hizo preguntas a los sacerdotes y levitas sobre el almacén de bienes.
Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
10 Y Azarías, el principal sacerdote de la familia de Sadoc, dijo en respuesta: Desde el momento en que las personas llegaron por primera vez con sus ofrendas a la casa del Señor, hemos comido lo suficiente, y más que suficiente, porque la bendición del Señor está sobre su pueblo; Y toda esta cantidad a sobrado.
naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
11 Entonces Ezequías dijo que los almacenes debían estar listos en la casa del Señor; y esto fue hecho.
Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
12 Y en ellos pusieron todas las ofrendas, las décimas y las porciones consagradas, sin guardar nada, y sobre ellos estaba Conanias el levita, y a Simei, su hermano, le siguió.
Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
13 Y Jehiel, Azazias, Nahat, Asael y Jerimot y Jozabad y Eliel e Ismaquias, Mahat y Benaía eran supervisores, bajo la dirección de Conanias y Simei su hermano, por orden de Ezequías el rey y Azarías, el gobernante de la casa de Dios.
Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
14 Y Core, el hijo de Imna el levita, el guardián de la puerta del este, tenía el control de las ofrendas dadas gratuitamente a Dios, y la distribución de las ofrendas del Señor y las porciones consagradas.
Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
15 Y debajo de él estaban Edén y Miniamin y Jesua y Semaías, Amarías y Secanias, en los pueblos de los sacerdotes, quienes se hicieron responsables de dar el reparto de las porciones, por turnos, a pequeños y grandes:
Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
16 Así como a todos los varones, de tres años y más, enumerados por sus familias, que entraron en la casa del Señor para hacer lo que se necesitaba día a día, para su trabajo especial con sus turnos.
Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
17 Las familias de los sacerdotes fueron nombradas por los nombres de sus padres, pero los levitas, de veinte años en adelante, fueron listados en relación a su servicio en sus turnos;
Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
18 Y en las listas estaban todos sus pequeños y sus esposas y sus hijos e hijas, todo la familia, porque se consagraban fielmente a la santidad.
Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
19 Y en cuanto a los hijos de Aarón, los sacerdotes, que viven en el campo en las afueras de sus pueblos, en cada pueblo diferente había hombres, inscritos por su nombre, para dar su parte de los bienes a todos los hombres, entre los sacerdotes, y a todos los que estaban incluidos entre los levitas.
Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
20 Esto hizo Ezequías a través de todo Judá; hizo lo que era bueno, correcto y verdadero delante del Señor su Dios.
Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
21 Y por todo lo que hizo, en relación con el servicio del templo de Dios y su ley y sus órdenes, recibió instrucciones de Dios y lo hizo con un propósito serio; Y por eso fue prosperado.
Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.

< 2 Crónicas 31 >