< 2 Crónicas 30 >

1 Entonces Ezequías envió un mensaje a todo Israel y a Judá, y envió cartas a Efraín y Manasés, invitándolos que vinieran a la casa del Señor en Jerusalén para celebrar la Pascua al Señor, el Dios de Israel.
Hezekia akatuma ujumbe kuwaita Israeli wote na Yuda, pia akaandika barua kwa Efraimu na Manase, kuwakaribisha ili waje hekaluni mwa Bwana huko Yerusalemu kuadhimisha Pasaka kwa Bwana, Mungu wa Israeli.
2 Porque el rey, después de una discusión con sus jefes y todo el cuerpo del pueblo en Jerusalén, había tomado la decisión de celebrar la Pascua en el segundo mes.
Mfalme na maafisa wake pamoja na kusanyiko lote katika Yerusalemu waliamua kuadhimisha Pasaka katika mwezi wa pili.
3 No era posible mantenerlo en ese momento, porque no había suficientes sacerdotes que se hubieran purificado, y la gente no se había reunido en Jerusalén.
Kwa sababu makuhani hawakuwa wamejitakasa idadi ya kutosha na watu wakawa hawajakusanyika huko Yerusalemu, hawakuwa wameweza kuadhimisha Pasaka kwa wakati wake wa kawaida.
4 Y la cosa estaba bien ante los ojos del rey y de todo el pueblo.
Mpango huu ukaonekana wafaa kwa mfalme na kusanyiko lote.
5 Así que se ordenó que la palabra fuera enviada a través de todo Israel, desde Beerseba hasta Dan, para que vinieran a guardar la Pascua al Señor, el Dios de Israel, en Jerusalén; porque muchos no lo tenían en práctica de acuerdo con la ley.
Wakaamua kupeleka tangazo Israeli kote, kuanzia Beer-Sheba hadi Dani, wakiwaita watu waje Yerusalemu kuadhimisha Pasaka ya Bwana, Mungu wa Israeli. Ilikuwa haijaadhimishwa na idadi kubwa ya watu kama hiyo kufuatana na yale yaliyokuwa yameandikwa.
6 Y los mensajeros fueron con cartas del rey y sus jefes por todo Israel y Judá, por orden del rey, diciendo: Oh hijos de Israel, regresa de nuevo al Señor, el Dios de Abraham, Isaac e Israel, para que pueda volver a esa pequeña banda tuya que se ha mantenido a salvo de las manos de los reyes de Asiria.
Kwa amri ya mfalme, matarishi wakapita katika Israeli na Yuda kote wakiwa na barua kutoka kwa mfalme na kutoka kwa maafisa wake zikisema: “Watu wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Abrahamu, Isaki na Israeli, ili naye awarudie ninyi mliosalia, mlionusurika kutoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru.
7 No seas como sus padres y sus hermanos, que fueron pecadores contra el Señor, el Dios de sus padres, de modo que Él los envió a la desolación, como pueden ver.
Msiwe kama baba zenu na ndugu zenu, ambao hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Mungu wa baba zao, hivyo akawafanya kitu cha kushangaza kama mnavyoona.
8 Ahora, no seas de corazón duro, como lo fueron tus padres; sino entrégate al Señor, y entra en su lugar santo, que él ha hecho suyo para siempre, y sean siervos del Señor tu Dios, para que el calor de su ira se aleje de ustedes.
Msiwe na shingo ngumu, kama baba zenu walivyokuwa, bali nyenyekeeni kwa Bwana. Njooni mahali patakatifu, alipopatakasa milele. Mtumikieni Bwana Mungu wenu, ili hasira yake kali igeuziwe mbali nanyi.
9 Porque si regresas al Señor, los que se llevaron a tus hermanos y a tus hijos tendrán compasión delante de los que los llevaron cautivos, y volverán a está tierra; porque el Señor tu Dios está lleno de gracia y de misericordia, y su rostro no se apartará de ustedes si vuelven a él.
Kama mkimrudia Bwana ndipo wale ndugu zenu waliotekwa pamoja na watoto wenu watakapoonewa huruma na wale waliowateka na kuwaachia warudi katika nchi hii, kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni mwenye neema na huruma, hatageuzia uso wake mbali nanyi kama ninyi mkimrudia yeye.”
10 Así que los corredores fueron de ciudad en ciudad a través de todo el país de Efraín y Manasés hasta Zabulón, pero la gente se reía y se burlaban de ellos.
Matarishi wakaenda mji hadi mji katika Efraimu na Manase, wakafika mpaka Zabuloni, lakini watu wakawadharau na kuwadhihaki.
11 Sin embargo, algunos de Aser y Manasés y Zabulón se humillaron ante Dios y acudieron a Jerusalén.
Lakini, baadhi ya watu wa Asheri, Manase na Zabuloni, wakajinyenyekeza wakaja Yerusalemu.
12 Y en Judá, el poder de Dios les dio un solo corazón para cumplir las órdenes del rey y los capitanes, conforme a la palabra del Señor.
Pia katika Yuda mkono wa Mungu ulikuwa juu ya watu kuwapa umoja katika kutenda yale ambayo mfalme na maafisa wake waliwaamuru, kulingana na neno la Bwana.
13 Entonces, un gran número de personas se reunieron en Jerusalén para celebrar la fiesta del pan sin levadura en el segundo mes.
Basi umati mkubwa wa watu ukakusanyika huko Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu katika mwezi wa pili.
14 Y se pusieron a trabajar y se llevaron todos los altares de Jerusalén, y los echaron todas las vasijas para quemar incienso en él arroyo de Cedrón.
Wakajitia kazini kuyaondoa yale madhabahu yaliyokuwa huko Yerusalemu, wakayaondoa pia yale madhabahu ya kufukizia uvumba kwa miungu na kuyatupa Bonde la Kidroni.
15 Y a los catorce días del segundo mes mataron a los corderos de la Pascua; y los sacerdotes y los levitas se avergonzaron, se purificaron y llevaron ofrendas quemadas a la casa del Señor.
Kisha wakamchinja mwana-kondoo wa Pasaka katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi waliona aibu, wakajitakasa na kuleta sadaka za kuteketezwa katika Hekalu la Bwana.
16 Y tomaron sus lugares en el orden correcto, como estaba ordenado en la ley de Moisés, el hombre de Dios; los sacerdotes rociaban sobre el altar la sangre que les dieron los levitas.
Kisha wakachukua nafasi zao za kawaida kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. Makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa na Walawi.
17 Porque todavía había un número de personas que no se habían purificado; así los levitas tuvieron que dar muerte a los corderos de la Pascua por aquellos que no estaban purificados, y consagrarlos para el Señor.
Kwa kuwa wengi waliokuwa katika lile kusanyiko walikuwa hawajajitakasa, iliwapasa Walawi wachinje wana-kondoo wengine wa Pasaka kwa ajili ya wale watu ambao hawakuwa safi, kwa kufuata taratibu za ibada ili kuwatakasa kwa Bwana.
18 Para un gran número de personas de Efraín y Manasés, Isacar y Zabulón, no se habían purificado, pero tomaron la comida de la Pascua, aunque no de la manera correcta. Pero Ezequías había orado por ellos, diciendo: Que el buen Señor tenga misericordia de todos aquellos que de corazón sincero lo buscan,
Ingawa watu wengi miongoni mwa wale waliotoka Efraimu, Manase, Isakari na Zabuloni walikuwa hawajajitakasa, hata hivyo walikula Pasaka kinyume na ilivyoandikwa. Lakini Hezekia akawaombea, akisema, “Bwana, ambaye ni mwema na amsamehe kila mmoja
19 Que con todo su corazón se dirige a Dios el Señor, el Dios de sus antepasados, aunque no hayan sido purificados según las reglas del santuario.
ambaye anauelekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Bwana, Mungu wa baba zake, hata kama yeye si safi kulingana na sheria za mahali patakatifu.”
20 Y él Señor oyó a Ezequías, y sanó a la gente.
Naye Bwana akamsikia Hezekia akawaponya watu.
21 Entonces los hijos de Israel que estaban presentes en Jerusalén celebraron la fiesta del pan sin levadura durante siete días con gran gozo: y los levitas y los sacerdotes alababan al Señor día tras día, haciendo la melodía con instrumentos al Señor y con voz fuerte.
Waisraeli waliokuwa Yerusalemu wakaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, nao Walawi na makuhani walikuwa wakiimba kila siku, wakiwa na ala za uimbaji za kumsifu Bwana.
22 Entonces Ezequías dijo palabras amables a los levitas que eran expertos en la ministración de la adoración al Señor: así celebraron la fiesta durante siete días, ofreciendo ofrendas de paz y alabando al Señor, el Dios de sus antepasados.
Hezekia akazungumza akiwatia moyo Walawi wote, ambao walionyesha ustadi katika kumtumikia Bwana. Hivyo watu wakala chakula cha sikukuu kwa siku saba, wakitoa sadaka za amani na kumshukuru Bwana, Mungu wa baba zao.
23 Y por el deseo de todo el pueblo, la fiesta duró otros siete días, y guardaron los siete días con alegría.
Kisha kusanyiko lote likakubali kuendelea na sikukuu kwa siku saba zaidi, kwa hiyo kwa siku saba nyingine wakaendelea kuiadhimisha kwa furaha.
24 Porque Ezequías, rey de Judá, dio al pueblo por ofrendas, mil bueyes y siete mil ovejas; y los príncipes dieron mil bueyes y diez mil ovejas; y muchos sacerdotes se purificaron.
Hezekia, mfalme wa Yuda akatoa mafahali 1,000, kondoo na mbuzi 7,000 kwa ajili ya kusanyiko, nao maafisa wakatoa mafahali 1,000 pamoja na kondoo na mbuzi 10,000. Idadi kubwa ya makuhani wakajiweka wakfu.
25 Y todo el pueblo de Judá, con los sacerdotes y los levitas, y los que habían venido de Israel, y los hombres extranjeros que habían venido de Israel o que vivían en Judá, se alegraron con gran alegría.
Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na lile kusanyiko lote lililotoka Israeli, pamoja na wale wageni waliotoka Israeli na wale walioishi katika Yuda wakafurahi.
26 Y hubo gran gozo en Jerusalén: porque nada como esto había sido visto en Jerusalén desde el tiempo de Salomón, el hijo de David, rey de Israel.
Kulikuwa na furaha kubwa katika Yerusalemu, kwa sababu tangu siku za Mfalme Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli halijakuwepo jambo kama hili katika Yerusalemu.
27 Entonces los sacerdotes y los levitas dieron a las personas una bendición; y la voz de su oración subió al lugar santo de Dios en el cielo.
Ndipo makuhani na Walawi wakasimama wakawabariki watu, naye Mungu akawasikia, kwa sababu maombi yao yalifika mbinguni, makao yake matakatifu.

< 2 Crónicas 30 >