< 2 Crónicas 13 >

1 En el año dieciocho del rey Jeroboam, Abías se convirtió en rey de Judá.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Fue rey en Jerusalén durante tres años; El nombre de su madre era Maaca, la hija de Uriel de Guibea. Y hubo guerra entre Abías y Jeroboam.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibea. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
3 Y Abías salió a pelear con un ejército de hombres de guerra, cuatrocientos mil de sus mejores hombres; y Jeroboam alineó sus fuerzas contra él, ochocientos mil de sus mejores hombres de guerra.
Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye uwezo wa kupigana, naye Yeroboamu akapanga jeshi dhidi ya Abiya akiwa na jeshi la watu 800,000 wenye uwezo.
4 Y Abías tomó posición en el monte Zemaraim, en la región montañosa de Efraín, y dijo: Escúchenme, Jeroboam y todo Israel:
Abiya akasimama juu ya Mlima Semaraimu, katika nchi ya vilima ya Efraimu, naye akasema, “Yeroboamu na Israeli yote, nisikilizeni mimi!
5 ¿No te queda claro que el Señor, el Dios de Israel, le dio el gobierno de Israel a David y sus hijos para siempre, por un acuerdo hecho con sal?
Hamfahamu kwamba Bwana, Mungu wa Israeli, alimpa Daudi na wazao wake ufalme juu ya Israeli milele kwa Agano la chumvi?
6 Más Jeroboam, hijo de Nabat, siervo de Salomón, hijo de David, tomó las armas contra su señor.
Hata hivyo Yeroboamu mwana wa Nebati afisa wa Solomoni mwana wa Daudi, aliasi dhidi ya bwana wake.
7 Y ciertos hombres insensatos y perversos se unieron a él y se impusieron contra Roboam, el hijo de Salomón, pues era joven y débil de carácter, y no podía retenerlos.
Baadhi ya watu wasiofaa kitu, wabaya kabisa walimkusanyikia na kumpinga Rehoboamu mwana wa Solomoni alipokuwa kijana mdogo asiyekuwa na uamuzi, asiye na nguvu za kuweza kupingana nao.
8 Ahora es su propósito ponerse en contra de la autoridad que el Señor ha puesto en manos de los hijos de David, y ustedes, son una gran multitud y tienen con ustedes los bueyes de oro que hizo Jeroboam para ser sus dioses.
“Hata sasa unapanga kupingana na ufalme wa Bwana ambao uko mikononi mwa wazao wa Daudi. Kweli ninyi ni jeshi kubwa nanyi mnazo ndama za dhahabu Yeroboamu alizozitengeneza kuwa miungu yenu.
9 Y después de expulsar a los sacerdotes del Señor, los hijos de Aarón y los levitas, ¿no han hecho sacerdotes de entre ustedes mismos como lo hacen los pueblos de otras tierras? para que cualquiera que venga a hacerse sacerdote ofreciendo un buey o siete ovejas, pueda ser un sacerdote de aquellos que no son dioses.
Lakini je, hamkuwafukuza makuhani wa Bwana, wana wa Aroni na Walawi na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama yafanyavyo mataifa ya nchi nyingine? Yeyote anayekuja kujiweka wakfu akiwa na ndama dume na kondoo dume saba aweza kuwa kuhani wa kile ambacho ni miungu kwenu.
10 Pero en cuanto a nosotros, el Señor es nuestro Dios, y no nos hemos apartado de él; tenemos sacerdotes que hacen la obra del Señor, incluso los hijos de Aarón y los levitas en sus lugares;
“Lakini kwetu sisi, Bwana ndiye Mungu wetu, wala hatujamwacha. Makuhani wanaomtumikia Bwana ni wana wa Aroni, nao Walawi wakiwasaidia.
11 Por quienes las ofrendas quemadas y los inciensos son enviados en humo delante del Señor cada mañana y cada tarde; y pusieron el pan sagrado sobre su mesa y los candelabros de oro con sus luces encendidas cada noche; porque guardamos las órdenes que nos dio el Señor nuestro Dios, pero ustedes se han alejado de él.
Kila asubuhi na jioni wao hutoa sadaka za kuteketezwa na kufukiza uvumba wa harufu nzuri kwa Bwana. Wao huweka mikate juu ya meza safi kwa taratibu za kiibada na kuwasha taa kwenye kinara cha dhahabu kila jioni. Sisi tunazishika kanuni za Bwana Mungu wetu. Lakini ninyi mmemwacha Mungu.
12 Y ahora Dios está con nosotros a la cabeza, y sus sacerdotes con sus fuertes cuernos sonando contra ti. Oh hijos de Israel, no hagan guerra contra el Señor, el Dios de sus antepasados, porque no les irá bien.
Mungu yu pamoja nasi, yeye ndiye kiongozi wetu. Makuhani wake wakiwa na tarumbeta zao watapiga baragumu ya vita dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane dhidi ya Bwana, Mungu wa baba zenu, kwa maana hamtashinda.”
13 Pero Jeroboam había puesto a algunos de sus hombres para que los atacaran por la espalda, por lo que algunos se enfrentaban a Judá y otros estaban apostados en secreto a sus espaldas.
Basi Yeroboamu alikuwa ametuma jeshi kuzunguka nyuma ya Yuda ili kwamba akiwa mbele ya Yuda, jeshi liwavizie kwa nyuma.
14 Y Judá, volviendo sus rostros, vio que estaban siendo atacados por delante y por detrás; y clamaron al Señor para pedir ayuda, mientras los sacerdotes hacían sonar sus cuernos.
Basi Yuda wakageuka na kuona kwamba wanashambuliwa mbele na nyuma. Ndipo wakamlilia Bwana. Makuhani wakapiga tarumbeta zao,
15 Y los hombres de Judá dieron un fuerte clamor; y ante su clamor, Dios derrotó a Jeroboam y a todo Israel delante de Abías y de Judá.
nao watu wa Yuda wakapaza sauti ya kilio cha vita. Katika kupiga kelele za vita, Mungu akawafukuza Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Mfalme Abiya na Yuda.
16 Y huyeron los hijos de Israel delante de Judá, y Dios los entregó en sus manos.
Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao.
17 Y Abías y su pueblo los mataron con gran destrucción; quinientos mil de los mejores de Israel fueron puestos a filo de espada.
Abiya na watu wake wakawachinja kwa machinjo makuu, hata wakawepo majeruhi 500,000 miongoni mwa watu wenye uwezo wa Israeli.
18 Entonces en ese tiempo los hijos de Israel fueron humillados, y los hijos de Judá prevalecieron, porque confiaron en el Señor, el Dios de sus padres.
Watu wa Israeli walitiishwa katika tukio lile, nao watu wa Yuda wakawa washindi kwa sababu walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.
19 Y Abías fue tras Jeroboam y tomó algunas de sus ciudades, Bethel con sus pueblos pequeños y Jesana con sus pueblos pequeños y Efron con sus pueblos pequeños.
Abiya akamfuatia Yeroboamu na kuteka miji ya Betheli, Yeshana na Efroni kutoka kwake, pamoja na vijiji vinavyoizunguka miji hiyo.
20 Y Jeroboam no volvió a recuperar su poder en la vida de Abías; y el SEÑOR envió muerte sobre él.
Yeroboamu hakupata nguvu tena wakati wa utawala wa Abiya. Naye Bwana akampiga Yeroboamu akafa.
21 Pero Abías se engrandeció, y tuvo catorce esposas, y fue padre de veintidós hijos y dieciséis hijas.
Lakini Abiya akapata nguvu. Alioa wanawake kumi na wanne na alikuwa na wana ishirini na wawili na binti kumi na sita.
22 Y el resto de los hechos de Abías, y sus caminos y sus dichos, están registrados en el relato del profeta Iddo.
Matukio mengine ya utawala wa Abiya, pamoja na mambo aliyofanya na aliyosema, yameandikwa katika kitabu cha maelezo cha nabii Ido.

< 2 Crónicas 13 >