< 1 Samuel 16 >

1 Entonces el Señor le dijo a Samuel: ¿Cuánto tiempo más seguirás lamentando a Saúl, viendo que lo he rechazado como rey sobre Israel? Toma aceite en tu cuerno y vete; Te enviaré a Isaí, el de Belén, porque tengo un rey para mí entre sus hijos.
BWANA akamwambia Samweli, “Utamlilia Sauli kwa muda gani, ikiwa nimemkataa asiwe mfalme juu ya Israeli? Ijaze pembe yako mafuta na uende. Nitakutuma kwa Yese akaaye Bethlehemu, maana nimejichagulia mfalme katika wanawe.
2 Y Samuel dijo: ¿Cómo puedo ir? Si Saúl recibe noticias de eso, me matará. Y el Señor dijo: Llévate una becerra y di: He venido para hacer una ofrenda al Señor.
Samweli akasema, “Jinsi gani nitaenda? Kama Sauli akisikia jambo hili, ataniua.” BWANA akasema, “chukua mtamba na useme, 'Nimekuja kutoa dhabihu kwa BWANA.'
3 Envía a Isaí para que esté presente en la ofrenda, y te diré lo que debes hacer, y debes ungir el aceite santo sobre aquel cuyo nombre te doy.
Umwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonesha kile utakachofanya. Utamtia mafuta kwa ajili yangu yule nitakaye kuambia.”
4 Entonces Samuel hizo lo que el Señor le dijo y fue a Belén. Y los ancianos del pueblo se acercaron temerosos y le dijeron: ¿Vienes en paz?
Samweli akafanya kama BWANA alivyosema na akaenda Bethlehemu. Wazee wa mji walikuwa wakitetemeka walipokuja kuonana naye na wakasema, “Je, umekuja kwa amani?”
5 Y él dijo: En paz, he venido para hacer una ofrenda al Señor; consagrense y vengan conmigo a hacer la ofrenda. E hizo consagrar a Isaí y a sus hijos, y envió a que estuvieran presentes en la ofrenda.
Naye akasema, “kwa amani; Nimekuja kutoa dhabihu kwa BWANA. Jitoeni wenyewe kwa BWANA kwa ajili ya dhabihu na muandamane nami,” Na akamweka wakfu Yese na watoto wake kwa BWANA, na baadaye aliwaita wote kwenye dhabihu.
6 Cuando llegaron, mirando a Eliab, dijo: Claramente, el hombre de la selección del Señor está delante de él.
Walipofika, akamwangalia Eliabu na akajisemea mwenyewe kwamba mtiwa mafuta wa BWANA hakika amesimama mbele yake.
7 Pero el Señor le dijo a Samuel: No tomes nota de su rostro ni de cuán alto sea, porque no lo tendré; porque el punto de vista del Señor no es del hombre; el hombre toma nota de la forma externa, pero el Señor ve el corazón.
Lakini BWANA akamwambia Samweli, “Usimwangalie sura yake ya nje, au kimo cha umbo lake; kwa sababu nimemkataa. Maana BWANA haangalii kama mtu aangaliavyo; mtu hutazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.”
8 Entonces Isaí envió a buscar a Abinadab y lo hizo venir ante Samuel. Y él dijo: El Señor no ha escogido este.
Kisha Yese akamwita Abinadabu akamwambia apite mbele ya Samweli. Na Samweli akasema, “Hata huyu BWANA hakumchagua.”
9 Entonces Isaí hizo que Sama viniera delante de él. Y él dijo: El Señor no ha escogido a este.
Kisha Yese akmwambia Shama apite karibu. Na Samweli akasema, “Hata huyu BWANA hakumchagua.”
10 E hizo Isaí que sus siete hijos fueran antes que Samuel. Y Samuel dijo a Isaí: El Señor no ha escogido a ninguno de estos.
Yese akawaleta watoto wake saba wakapita mbele ya Samweli. Na Samweli akamwambia Yese, “Hakuna hata mmoja aliyechaguliwa na BWANA kati ya hawa.”
11 Entonces Samuel dijo a Isaí: ¿Están todos tus hijos aquí? Y él dijo: Todavía hay el más joven, y él está cuidando las ovejas. Y Samuel dijo a Isai: envía y haz que venga aquí, porque no nos sentaremos hasta que él esté aquí.
Kisha Samweli akamuulia Yese, “Je, watoto wako wote wako hapa?” Naye akajibu, “Yupo mdogo kabisa lakini anachunga kondoo.” Samweli akamwambia Yese, “Tuma watu wakamwite; maana hatutakaa chini hadi atakapofika hapa.”
12 Entonces envió y lo hizo entrar. Ahora tenía el pelo rojo y ojos hermosos y bien parecido. Y el Señor dijo: Ven, úngelo con aceite, porque este es él.
Yese akawatuma watu wakamleta. Naye kijana huyu alikuwa mwekundu na mwenye macho mazuri na mwenye muonekano mzuri. BWANA akasema, “Amka, umtie mafuta; maana huyu ndiye.”
13 Entonces Samuel tomó el cuerno de aceite y puso el aceite sobre él entre sus hermanos; y desde ese día el espíritu del Señor vino sobre David con poder. Entonces Samuel volvió a Ramá.
Ndipo Samweli akachukua pembe yenye mafuta na kumtia mafuta katikati ya kaka zake. Roho wa BWANA akamwijia Daudi kwa nguvu tangu siku hiyo na kuendelea. Kisha Samweli akanyanyuka na kwenda Rama.
14 Ahora el espíritu del Señor había dejado a Saúl, y un espíritu maligno de parte de Señor lo estaba molestando.
Basi Roho wa BWANA akamwacha Sauli, badala yake roho ya ubaya kutoka kwa BWANA ikamsumbua.
15 Y los siervos de Saúl le dijeron: Mira, un espíritu maligno de Dios te está molestando.
Watumishi wa Sauli wakamwambia, “Tazama, roho ya ubaya kutoka kwa Mungu inakusumbua.
16 Ahora da órdenes a tus siervos que están aquí delante de ti para que vayan en busca de un hombre que sea un experto en tocar un instrumento con cuerda: y será que cuando el espíritu maligno de Dios esté sobre ti, tocará música para ti en su instrumento, y te pondrás bien.
Haya bwana wetu hebu sasa amuru watumishi wako walio mbele yako wamtafute mtu mwenye ujuzi wa kupiga kinubi. Basi ikwa roho wa ubaya kutoka kwa Mungu yuko juu yako, atakipiga kinubi nawe utajisikia vizuri.”
17 Entonces Saúl dijo a sus siervos: Consígueme un hombre que toque bien música y haz que venga a mí.
Sauli akawaambia watumishi wake, “Mnitafutie mtu anayeweza kupiga vizuri na mmlete kwangu.”
18 Entonces uno de los sirvientes en respuesta dijo: He visto a un hijo de Isaí, de belén, entrenado en música y toca bien, y un hombre fuerte y un hombre de guerra; y él es sabio en sus palabras, y agradable en apariencia, y el Señor está con él.
Ndipo kijana mmoja kati yao akajibu, na kusema, “Nimemuona mtoto wa Yese Mbethtelehemu, aliye mjuzi katika kupiga, ni mwenye nguvu, mtu jasiri, mtu wa vita, mwenye busara aongeapo, mtu mzuri kwa uso; na BWANA yuko pamoja naye.”
19 Entonces Saúl envió a sus siervos a Isaí y dijo: Envíame a tu hijo David, que está con las ovejas.
Hivyo Sauli akawatuma wajumbe kwa Yese, na kusema, “Nitumie mtoto wako Daudi, anayewatunza kondoo.” 1 Samweli! 6: 20-21
20 Entonces Isaí envío un asno cargado con cinco tartas de pan y una piel de vino y un cabrito y las envió a Saúl con David.
Yese akamchukua punda aliyebeba mikate, na kiriba cha divai, na mwana-mbuzi, na akamtuma kwa Sauli pamoja na vitu hivyo.
21 Vino David a Saúl, que esperaba delante de él, y se hizo muy querido por Saúl, que lo hizo su siervo y le hizo su paje de armas.
Ndipo Daudi akafika kwa Sauli na kuanza kazi yake. Sauli alimpenda sana Daudi, na akawa mbeba silaha wake.
22 Entonces Saúl envió a Isaí diciendo: Que David se quede conmigo, porque ha hallado gracia en mis ojos.
Sauli akawatuma wajumbe kwa Yese, akisema, “Mruhusu Daudi awe mbele yangu, maana amepata kibali machoni pangu.”
23 Y cada vez que el espíritu maligno de Dios venía a Saúl, David tomaba su instrumento y hacía música: así le llegó una nueva vida a Saúl, y él mejoró, y el espíritu maligno se fue de él.
Wakati wowote roho ya usumbufu kutoka kwa Mungu ikiwapo juu ya Sauli, Daudi alichukuwa kinubi na kukipiga. Hivyo Sauli angeburudishwa na kupona, na huyo roho wa usumbufu angemtoka.

< 1 Samuel 16 >