< 1 Samuel 14 >

1 Un día Jonatán, hijo de Saúl, dijo al joven que estaba con él, cuidando de sus armas: Ven, vamos a la guarnición filistea que está al otro lado. Pero no le dijo nada a su padre.
Siku moja, Yonathani mwana wa Sauli alimwambia mbeba silaha wake aliye mdogo, “Njoo, hebu twende hadi upande mwingine kwenye ngome ya Wafilisti.” Lakini hakumjulisha baba yake.
2 Y Saúl todavía esperaba en la parte más alejada de Geba, debajo de un granado en Migrón: había unos seiscientos hombres con él;
Sauli alikuwa akikaa nje ya mji wa Gibea chini ya mti wa mkomamanga ulio katika Migroni. Takribani watu mia sita walikwa pamoja naye,
3 Y Ahías, hijo de Ahitob, hermano de Icabod, hijo de Finees, hijo de Elí, sacerdote del Señor en Silo, que tenía el efod. Y la gente no tenía idea de que Jonatan se había ido.
akiwemo Ahiya mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi) mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa BWANA huko Shilo, aliyevaa naivera. Watu hao hawakujua kwamba Yonathani ameondoka.
4 Ahora, entre los estrechos caminos sobre las montañas por las que Jonatán se dirigía hacia las fuerzas de los filisteos, había una roca afilada que sobresalía en un lado y una roca afilada en el otro lado, una se llamaba Boses y el otro Sene.
Katikati ya vichochoro, ambavyo Yonathani alinuia kuvipita hadi ngome ya Wafilisti, kulikuwa na mwamba wenye mteremko mkali upande mmoja, na mteremko mkali upande mwingine. Jabali moja liliitwa Bosesi, na jingine liliitwa Sene.
5 Una roca subió al norte frente a Micmas y la otra al sur frente a Guibeá.
Lile jabali lenye mteremko mkali zaidi liliinuka upande wa kaskazini mbele ya Mikmashi, na jingine upande wa kusini mbele ya Geba.
6 Y Jonatán dijo a su joven siervo que tenía sus armas: Ven, vamos a los ejércitos de estos hombres que no tienen circuncisión: puede ser que el Señor nos ayude, porque no hay límite a su poder; el Señor puede dar la salvación por un gran ejército o por una pequeña banda.
Yonathani akamwambia kijana mbeba silaha, “Njoo, na tuvuke hadi ngome ya hawa wasiotahiriwa. Pengine BWANA atatenda kwa niaba yetu, kwa maana hakuna kitu kiwezacho kumzuia BWANA asiokoe kwa wengi au kwa watu wachache.”
7 Y su criado le dijo: Haz lo que esté en tu mente; mira, estoy contigo en cada impulso de tu corazón.
Mbeba silaha wake akajibu, “Fanya kila kitu kilicho ndani ya moyo wako. Songa mbele, tazama, niko pamoja nawe, nitatii maagizo yako yote.”
8 Entonces Jonatán dijo: Ahora pasaremos a estos hombres y dejaremos que nos vean.
Ndipo Yonathani akasema, “Tutavuka twende kwa watu hao, na tutajionesha wenyewe kwao.
9 Si nos dicen: Quédate quieto donde estás hasta que lleguemos a ustedes; entonces mantendremos nuestros lugares y no subiremos a ellos.
Kama watatuambia, 'Subirini hapo hadi tutakapokuja kwenu' - basi tutabaki katika sehemu yetu na hatutavuka kwenda kwao.
10 Pero si ellos dicen: Vengan acá; luego subiremos, porque el Señor los ha entregado en nuestras manos, y esta será la señal para nosotros.
Lakini kama watajibu, 'Njoni kwetu,' ndipo tutavuka; kwa sababu BWANA amewaweka mkononi mwetu. Hii ndiyo itakuwa ishara yetu.”
11 Y dejaron que los filisteos los vieran a los dos; y los filisteos dijeron: ¡Miren! Los hebreos están saliendo de los agujeros donde se han cubierto.
Kwa hiyo wote wawili wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Angalia, Webrania wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha.”
12 Y los hombres armados de la fuerza respondieron a Jonatán y su siervo, diciendo: Vengan a nosotros y le dejaremos ver algo. Entonces Jonatán dijo a su siervo: Sube conmigo, porque el Señor los ha entregado en manos de Israel.
Ndipo watu wa ile ngome wakamwita Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njoni huku kwetu, tutawaonesha jambo fulani.” Na Yonathani akamwambia mbeba silaha wake; “Nifuate nyuma yangu, kwa sababu BWANA amewaweka katika mkono wa Israeli.”
13 Subió Jonatán con sus manos y sus pies, y su siervo subió tras él; y los filisteos caían ante Jonatán, y su siervo los mataba después de él.
Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake, na mbeba silaha akimfuata nyuma yake. Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani, na mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake.
14 En su primer ataque, Jonatán y su criado mataron a la espada a unos veinte hombres, todos en el espacio de medio acre de tierra.
Hilo shambulio la kwanza walilofanya Yonathani na mbeba silaha wake, waliua watu wapatao ishirini katika urefu wa nusu handaki kwenye eka moja ya ardhi.
15 Y había gran temor en los campamentos, y por el campo y entre todos los hombres de la fuerza armada, y los que merodeaban temblaban de miedo; incluso la tierra tembló con un gran temblor y hubo un temor por Dios.
Kukawa na hofu kubwa katika kambi, uwandani, na katika watu. Hata ngome ya jeshi na watekaji nyara nao wakawa na hofu kubwa
16 Y los vigilantes de Saúl, mirando desde Geba en la tierra de Benjamín, vieron a todo el ejército fluir y correr aquí y allá.
Ndipo walinzi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona kundi la askari wa Wafilisti likitawanyika, wakienda kule na huku.
17 Entonces Saúl dijo a la gente que estaba con él: Pasen revista y veamos quién se ha ido de nosotros. Y cuando fueron contados, se vio que Jonatán y su escudero no estaban allí.
Kisha Sauli akawaambia watu aliokuwa nao, “Mjihesabu ili muone nani hayupo hapa.”Walipokuwa wamehesabu, wakagundua kuwa Yonathani na mbebaji wa silaha zake hawapo.
18 Y Saúl dijo a Ahías: Que venga aquí el cofre del pacto. Porque él cofre del pacto estaba con Israel en ese momento.
Sauli akamwambia Ahiya, “Lete hapa naivera ya Mungu”- kwa maana siku hiyo Ahiya alivaa naivera akiwa pamoja na askari wa Israeli.
19 Mientras Saúl hablaba con el sacerdote, el ruido en los campamentos de los filisteos se hizo cada vez más fuerte; Y Saúl dijo al sacerdote: detén tu mano.
Wakati Sauli akiongea na kuhani, kelele na ghasia kubwa iliendelea na kuongezeka katika kambi ya Wafilisti. dipo sauli akamwambia kuhani, “Acha kazi unayofanya.”
20 Entonces Saúl y todas las personas que estaban con él se reunieron y avanzaron a la lucha: y la espada de cada uno se volvió contra el hombre que estaba a su lado, y se oyó un gran ruido.
Sauli na watu wote aliokuwa nao wakajipanga na kwenda kwenye mapigano. Upanga wa kila Mfilisti ulikwa juu ya Mfilisti mwenzake, na kulikuwa na ghasia kubwa.
21 Entonces los hebreos que habían estado con los filisteos por algún tiempo, y habían subido con ellos a sus campamentos, se dieron vuelta y se unieron a los que estaban con Saúl y Jonatán.
Basi Waebrania ambao mwanzoni walijiunga na Wafilisti, na kwenda kwenye kambi yao, wao pia waliungana na Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Y todos los hombres de Israel que se habían refugiado en la región montañosa de Efraín, al oír que los filisteos habían huido, los persiguieron y los atacaron.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima karibu na Efraimu waliposikia kwamba Wafilisti wamekimbia, nao pia wakawafuata Wafilisti nakuwafukuza kwenye hiyo vita.
23 Entonces él Señor salvó a Israel aquel día, y la lucha se extendió a Bet-avén.
Hivyo siku hiyo BWANA aliwaokoa Israeli, na mapigano yalivuka kupitiliza Beth aveni.
24 Y todo el pueblo de Israel estaba en gran apuro, unos veinte mil hombres, y la lucha fue general en toda la región montañosa de Efraín. Pero Saúl cometió un gran error ese día al poner bajo juramento a la gente, diciendo: “Que se maldiga al hombre que come antes de que llegue la noche y que haya castigado a los que están en mi contra”. Así que la gente no había comido.
Siku hiyo watu wa Israeli walifadhaika kwa sababu Sauli aliwaweka watu chini ya kiapo akasema, “Na alaaniwe mtu atakaye kula chakula kabla ya jioni na kabla sijalipiza kisasi kwa maadui zangu.” Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula.
25 Y había miel en el campo, y todo el pueblo vino a la miel, habiendo salido las abejas;
Ndipo watu wote wakaingia msituni na kuona asali ikiwa juu ya ardhi.
26 Pero ningún hombre se llevó la mano a la boca por temor a la maldición.
Watu walipoingia humo msituni, asali ilitiririka, lakini hakuna aliyeweka mkono wake kinywani kwa maana watu waliogopa kiapo.
27 Pero Jonatán, no sabiendo el juramento que su padre había puesto sobre la gente, extendiendo la vara que tenía en la mano, la puso en la miel y se la puso en la boca; entonces sus ojos brillaron.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kwamba baba yake amewaagiza watu kwa kiapo. Akanyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya kwenye sega la asali. Kisha akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake, na macho yake yakaangaziwa.
28 Entonces uno de los de la gente le dijo: Tu padre juró a la gente, diciendo: Que se maldiga al hombre que come algo hoy. Y la gente era débil, necesitando comida.
Ndipo mmoja wa watu hao, akamwambia, “Baba yako aliwaagiza watu kwa mkazo na kwa kiapo, kwa kusema, 'Alaaniwe mtu atakaye kula chakula kwa siku ya leo,' ingawa watu wamedhoofika kwa ajili ya njaa.”
29 Entonces Jonatán dijo: Mi padre ha hecho que los problemas lleguen a la tierra: ahora mira qué tan brillantes se han vuelto mis ojos porque he tomado un poco de esta miel.
Baadaye Yonathani alisema, “Baba yangu amefanya matatizo katika nchi. Angalia jinsi macho yangu alivyotiwa nuru kwa sababu nilionja asali hii kidogo.
30 ¡Cuánto más si la gente hubiera tomado libremente su comida de los bienes de los que luchaban contra ellos! ¿No habría habido una destrucción mucho mayor entre los filisteos?
Je, siyo vivuri sana kama leo watu wangekula bila kizuizi nyara walizopata kutoka kwa maadui zao? Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa katikati ya Wafilisti.”
31 Ese día vencieron a los filisteos de Micmas hasta Ajalón, y la gente estaba débil por la necesidad de comida.
Siku hiyo waliwashambulia Wafilisti kutoka Mikmashi hadi Aiyaloni. Na watu walikuwa wamechoka sana.
32 Apresurándose a los bienes tomados en la lucha, la gente tomó carneros y ovejas y becerros, y los mató allí en la tierra, y comió, tomando la carne con la sangre en ella.
Hivyo watu wakazivamia nyara na kuchukua kondoo, ng'ombe na ndama na kuwachinja hapo chini. Watu walikula nyama zao pamoja na damu.
33 Entonces se dijo a Saúl: Mira, la gente está pecando contra el Señor, tomando la sangre con la carne. Y dijo a los que le dieron la noticia: Ahora, hágame rodar una gran piedra aquí.
KIsha wakamwambia Sauli, “Tazama, watu wanamtenda BWANA dhambi kwa kula pamoja na damu.” Sauli akasema, “Mmetenda isivyo haki. Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu.” Sauli akasema,
34 Entonces Saúl dijo: Llamen al pueblo y díganles: Vengan todos los hombres aquí con su toro y sus ovejas, y matenlos aquí, y tomen su comida: no pequen contra el Señor tomando la sangre con la carne. Así que toda la gente llevó sus toros esa noche y los mató allí.
“Nendeni kati watu, na muwaambie, 'Kila mtu alete ng'ombe na kondoo wake, wawachinje hapa, na kuwala. Msimtende BWANA dhambi kwa kula na damu.”' Kwa hiyo watu wote wakaleta kila mtu na ng'ombe wake usiku huo na kuwachinja mahali hapo.
35 Entonces Saúl levantó un altar al Señor: este fue el primer altar que él puso al Señor.
Sauli akamjengea BWANA madhabahu, ambayo ilikuwa ya kwanza kwake kumjengea BWANA.
36 Entonces Saúl dijo: Bajemos después de los filisteos por la noche, atacándolos hasta la mañana, hasta que no haya un hombre de ellos vivo. Y ellos dijeron: Haz lo que te parezca correcto. Entonces el sacerdote dijo: Consultemos a Dios.
Ndipo Sauli akasema, “Haya tuwafukuze Wafilisti usiku na kuwateka nyara hadi asubuhi; tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai.” Nao wakamjibu, “Fanya unaloona linakupendeza.” Lakini kuhani akasema, “Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa.”
37 Y Saúl, deseando instrucciones de Dios, dijo: ¿Voy a bajar después de los Filisteos? ¿Los entregarás en manos de Israel? Pero no le dio respuesta ese día.
Sauli alitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Je, inanipasa kuwafukuza Wafilisti? Je, utawaweka katika mkono wa Israeli?” Lakini siku hiyo BWANA hakumjibu kitu.
38 Y Saúl dijo: Acérquense, jefes del pueblo, y recibamos un mensaje de Dios y veamos en quién está este pecado hoy.
Ndipo Sauli akasema, “Njoni hapa, viongozi wote wa watu; mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo.
39 Porque, por el Señor viviente, el salvador de Israel, aunque el pecador sea Jonatán, hijo mío, la muerte ciertamente será su destino. Pero ningún hombre entre todas las personas le dio una respuesta.
Kwa maana, kama BWANA aishivyo, aliyewaokoa Israeli, hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa.” Lakini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.
40 Entonces dijo a todo Israel: Estarás de un lado, y yo estaré con Jonatán, mi hijo, del otro lado. Y la gente le dijo a Saúl: Haz lo que te parezca bien.
Basi akawaambia Waisraeli wote, “Simameni upande mmoja, na mimi na Yonathani tutasimama upande mwingine.” Kisha watu wakamwambia Sauli, “Fanya lile unaloona jema kwako.”
41 Entonces Saúl dijo al Señor, el Dios de Israel: ¿Por qué no me has dado una respuesta hoy? Si el pecado está en mí o en mi hijo Jonatán, oh Señor Dios de Israel, da Urim, y si está en tu pueblo Israel, echa suertes. Y por decisión del Señor, y Jonatán quedó marcado, y la gente quedó libre.
Kwa hiyo, Sauli akamwambia BWANA, Mungu wa Israeli, “Tuoneshe Thumimu.” Yonathani na Sauli wakatwaliwa, lakini watu walinusurika kuchaguliwa.
42 Y Saúl dijo: Toma tu decisión entre mi hijo Jonatán y yo. Y Jonatán fue tomado.
Basi Sauli akasema, “Tupa mawe ya bahati nasibu tuone kati yangu na mwanangu Yonathani.” Ndipo Yonathani akatwaliwa.
43 Entonces Saúl dijo a Jonatán: Cuéntame lo que has hecho. Y Jonatán le contó la historia y dijo: Ciertamente tomé un poco de miel con la punta de mi vara; Y ahora la muerte será mi destino.
Kisha Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie umefanya nini.” Yonathani akamwambia baba yake, “Nilionja asali kidogo kwa kutumia ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwangu. Niko hapa; Nitakufa.”
44 Y Saúl dijo: Que el castigo de Dios sea conmigo y aun añada, si no mueres, Jonatán.
Sauli akasema, “Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa.”
45 Y el pueblo dijo a Saúl: ¿Ha de venir la muerte a Jonatán, el trabajador de esta gran salvación para Israel? Que no sea así: por el Señor vivo, no se debe tocar un solo cabello de su cabeza, porque él ha estado trabajando con Dios hoy. Así que la gente libró a Jonatan de la muerte.
Basi watu wakamuuliza Sauli, “Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo! Kama BWANA aishivyo, hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini, kwa maana leo amefanya kazi pamoja na Mungu.” Hivyo hao watu walimuokoa Yonathani ili asife.
46 Entonces Saúl, volviendo atrás, dejó de seguir a los filisteos, y los filisteos volvieron a su lugar.
Basi Sauli akasita kuwafuatia Wafilisti, nao wakarudi katika makao yao.
47 Cuando Saúl ocupó su lugar como gobernante de Israel, hizo la guerra a los que estaban contra él por todos lados, Moab y los amonitas y Edom y los reyes de Soba y los filisteos: y dondequiera que se volvía, los vencía.
Sauli alipoanza kutawala juu ya Israeli, alipigana na adui zake wote kila upande. Alipigana dhidi ya Moabu, dhidi ya watu wa Amoni, Edomu, wafalme wa Zoba, na Wafilisti. Popote alipogeukia aliwapiga kwa adhabu adui zake.
48 Y reunió un ejército, venció a los amalecitas y salvó a Israel de mano de los saqueadores.
Alitenda kwa ushujaa mkubwa na kuwashinda Waamaleki. Aliwaokoa Israeli kutoka mikono ya watu ambao waliwateka nyara.
49 Ahora bien, los hijos de Saúl fueron Jonatán e Isui y Malquisua; y estos son los nombres de sus hijas: la mayor se llamaba Merab y la menor Mical;
Basi wana wa Sauli walikuwa ni hawa Yonathani, Ishvi, na Malkishua. Na majina ya binti zake wawili yalikuwa ni haya, Merabu mzaliwa wa kwanza, na mdogo aliitwa Mikali.
50 El nombre de la esposa de Saúl fue Ahinoam, la hija de Ahimaas; El capitán de su ejército fue Abner, el hijo de Ner, hermano del padre de Saúl.
Jina la mke wa Sauli aliitwa Ahinoamu; naye alikuwa binti Ahimaasi. Na jina la Jemedari wa jeshi lake aliitwa Abneri mwana wa Neri, baba mdogo wa Sauli.
51 Cis, el padre de Saúl, y Ner, el padre de Abner, eran hijos de Abiel.
Kishi alikuwa baba yake Sauli; na Neri alikuwa baba yake na Abneri, wote walikuwa wana wa Abieli.
52 A lo largo de la vida de Saúl hubo una guerra amarga contra los filisteos; y cada vez que Saúl veía a un hombre fuerte o a un buen luchador, lo mantenía cerca de sí mismo.
Kulikuwa na mapigano makali dhidi ya Wafilisti katika siku zote za Sauli. Naye alipomwona mtu yeyote mwenye nguvu, au mtu yeyote jasiri, alimuunganisha kwake.

< 1 Samuel 14 >