< 1 Reyes 16 >
1 Entonces vino la palabra del Señor a Jehú, hijo de Hanani, que protestaba contra Baasa y decía:
Neno la BWANA lilimjia Yehu mwana wa Hanani kinyume cha Baasha, likisema,
2 Porque te saqué del polvo y te hice gobernar sobre mi pueblo Israel; y has seguido los caminos de Jeroboam, e hiciste mal a mi pueblo Israel, moviéndome a la ira por sus pecados;
Ingawa Nilikuinua kutoka kwenye mavumbi na kukufanya kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli, Lakini umetembea katika njia za Yeroboamu na umewafanya watu wangu Israeli kufanya dhambi, ili kunikasirisha dhidi ya dhambi zao.
3 Verdaderamente, veré que Baasa y toda su familia, su descendencia sea borrada; Haré que tu familia sea como la familia de Jeroboam, hijo de Nebat.
Tazama, Nitamfagia kabisa Baasha na familia yake na nitaifanya familia yako kama familia ya Yeroboamu mwana wa Nebati.
4 Cualquiera de la familia de Baasa que muera en la ciudad, se convertirá en alimento para los perros; y aquel a quien muera en campo abierto, será alimento para las aves del aire.
Mbwa watamla yeyote ambaye anatoka kwa Baasha wanaofia mjini, na ndege wa angani watamla yeyote anayaefia shambani.”
5 Los demás hechos de Baasa, y lo que hizo, y su poder, ¿no están registrados en el libro de la crónicas de los reyes de Israel?
Lakini kwa mambo mengine yanayohusiana na Baasha, aliyofanya, na uwezo wake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
6 Y Baasa durmió con sus padres y fue enterrado en Tirsa; y Ela su hijo se convirtió en rey en su lugar.
Baasha akalala na mababu zake na akazikwa Tirza, na Ela mwanae akawa mfalme mahali pake.
7 Y el Señor envió su palabra contra Baasa y su familia por boca del profeta Jehú, el hijo de Hanani, a causa de todo el mal que hizo ante los ojos del Señor, lo que lo llevó a la ira por la obra. de sus manos, porque era como la familia de Jeroboam, a quienes destruyó.
Kwa kupitia nabii Yehu mwana wa Hanani neno la BWANA likaja kinyume na Baasha na familia yake, wote kwa sababu ya maovu yote aliyofanya machoni pa BWANA, akamghadhabisha kwa kazi ya mikono yake, kama familia ya Yeroboamu, na kwa sababu alikuwa ameiua familia yote ya Yeroboamu.
8 En el año veintiséis en que Asa fue rey de Judá, Ela, el hijo de Baasa, se convirtió en rey de Israel en Tirsa, y él fue rey durante dos años.
Katika mwaka wa kumi na sita wa Asa mfalme wa Yuda, Ela mwana wa Baasha akaanza kutawala juu ya Israeli kule Tirza; akatawala kwa miaka miwili.
9 Y su siervo Zimri, capitán de la mitad de sus carros de guerra, hizo planes secretos contra él: ahora estaba en Tirsa, bebiendo mucho en la casa de Arza, mayordomo de la casa del rey en Tirsa.
Mtumishi wake Zimri, mkuu wa nusu ya magari yake akatengeneza hila dhidi yake. Wakati huo Ela alikuwa Tirza, akinywa na kulewa kwenye nyumba ya Arza, ambaye alikuwa mkuu wa watumishi wa nyumbani huko Tirza.
10 Entonces Zimri entró, lo atacó y lo mató, en el año veintisiete en que Asa era rey de Judá, y se hizo rey en su lugar.
Zimri akaiingia ndani, akamshambulia na kumwua, katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, naye akawa mfalme mahali pake.
11 Inmediatamente después, cuando se convirtió en rey y ocupó su lugar en el asiento del reino, mató a toda la familia de Baasa: ni un hijo varón de sus relaciones ni sus amigos se quedaron con su vida.
Zimri alipoaanza kutawala, mara tu baada ya kukaa kwenye kiti cha enzi, akawaua wanafamilia wote wa Baasha. Hakumwacha mtoto hata mmoja wa kiume, hakuna hata wa ndugu yake wala wa rafiki zake.
12 Entonces Zimri mató a toda la familia de Baasa, de modo que la palabra que el Señor dijo contra él por boca del profeta Jehú;
Kwa hiyo Zimri aliingamiza familia yote ya Baasha, kama alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA, ambalo lilinenwa kinyume na Baasha na nabii Yehu,
13 Por todos los pecados de Baasa y los pecados de Ela, su hijo, que hicieron e hicieron que Israel hiciera, moviendo al Señor, el Dios de Israel, a la ira por sus actos insensatos.
kwa dhambi zote za Baasha na za Ela mwanae ambazo walizifanya, ambazo kwazo waliisababisha Israeli kufanya dhambi, kiasi c ha kumghadhabisha BWANA, Mungu wa Israeli, kuzikasilikia sanamu zao.
14 Los demás hechos de Ela y todo lo que hizo, ¿no están registrados en el libro de las crónicas de los reyes de Israel?
Kwa mambo mengine yanayohusiana na Ela, yote ambayo alifanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
15 En el año vigésimo séptimo de Asa, rey de Judá, Zimri fue rey durante siete días en Tirsa. Ahora la gente estaba atacando a Gibbeton en la tierra de los filisteos.
Katika mwaka wa ishirini na saba wa Asa mfalme wa Yuda, Zimri alitawala kwa siku saba tu kule Tirza. Jeshi likafanya kambi kule Gibethoni, ambao ni mji wa Wafilisti.
16 Y a la gente de las tiendas de campaña les llegó la noticia de que Zimri había hecho un plan secreto y había dado muerte al rey: así que todo Israel hizo a Omri, el capitán del ejército, rey ese día en las tiendas.
Lile jeshi lililokuwa limeweka kambi kule lilisikika lilksema, “Zimri amepanga njama na amemwua mfalme.” Kwa hiyo siku hiyo hapo kambini, Israeli yote ikamtangaza Omri, mkuu wa jeshi, kuwa mfalme wa Israeli.
17 Luego Omri subió de Gibbeton, con todo el ejército de Israel, y atacaron a Tirsa.
Omri akapanda kutoka Gibethoni na Israeli yote pamoja naye, nao wakauhusuru Tirza.
18 Y cuando Zimri vio que habían tomado la ciudad, entró en la habitación interior de la casa del rey y, quemando la casa sobre su cabeza, llegó a su fin.
Kwa hiyoZimri alipoona kuwa mji umetekwa, akaingia kwenye ngome na akaivamia ikulu ya mfalme na kulichoma moto jengo lote pamoja na yeye; kwa hiyo akafa kwa moto.
19 Por causa de su pecado al hacer lo malo ante los ojos del Señor, al ir por el camino de Jeroboam y por el pecado que hizo hacer a Israel.
Hii ilikuwa ni kwa sababu ya dhambi alizofanya kwa kufanya maovu mbele ya macho ya BWANA, kwa kutembea katika njia ya Yeroboamu na katika dhambi ambazo alifanya, kiasi cha kuifanya Israeli wafanye dhambi.
20 Ahora, el resto de los actos de Zimri y la conspiración contra él rey Ela, ¿no están registrados en el libro de las crónicas de los reyes de Israel?
Pia kwa mambo mengiine yanayomhusu Zimri, na fitina yake aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
21 Entonces hubo una división entre el pueblo de Israel; La mitad de la gente estaba por hacer a Tibni, hijo de Ginat, rey, y la otra mitad estaba apoyando a Omri.
Sasa watu wa Israeli walikuwa wamegawanyika katika makundi mawili. Nusu ya watu walimfuata Tibni mwana wa Ginathi, wakamfanya kuwa mfalme, na Nusu walimfufata Omri.
22 Pero los partidarios de Omri vencieron a los que estaban del lado de Tibni, el hijo de Ginat; y la muerte llegó a Tibni y a su hermano Joram en ese momento: y Omri se convirtió en rey en lugar de Tibni.
Lakini watu waliomfuata Omri walikuwa na nguvu kuliko wale waliomfuata Tibni mwana wa Ginathi. Kwa hiyo Tibni akafa, na Omri akawa mfalme.
23 En el año treinta y uno de Asa, rey de Judá, Omri se convirtió en rey de Israel, y él fue rey durante doce años; Durante seis años estuvo gobernando en Tirsa.
Omri alianza kutawala juu ya Israeli katika mwaka wa thelathini na moja wa Asa mfalme wa Yuda, naye akatawala miaka kumi na miwili. Alitawala akiwa Tirza kwa miaka sita.
24 Obtuvo la colina Samaria de Semer por el precio de dos talentos de plata, e hizo una ciudad allí, construyéndose en la colina y llamándola Samaria, por Semer, el dueño de la colina.
Akakinunua kilima cha Samaria kutoka kwa Shemeri kwa kilo 68 za fedha. Akajenga mji juu ya mlima na ule mji akauita Samaria, kwa sababu ya jina la Shemeri, mmiliki wa awali wa kile kilima.
25 Y Omri hizo lo malo ante los ojos del Señor, aún peor que todos los que le precedieron,
Omri akafanya maovu mbele ya BWANA na akafanya yaliyo maovu zaidi kuliko wale waliokuwa kabla yake.
26 Copiando todos los caminos malos de Jeroboam, el hijo de Nebat, y todos los pecados que hizo e hizo que Israel hiciera, moviendo al Señor, el Dios de Israel, a la ira por sus caminos insensatos.
Kwa kuwa alitembea katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati na katika dhambi zake ambazo kwa hizo aliwaongoza Waisraeli kufanya dhambi, ili kumkasirisha BWANA, Mungu wa Israeli, ili kuwa na hasira juu ya sanamu zao za ubatili.
27 El resto de los actos que hizo Omri y su gran poder, ¿no están registrados en el libro de las crónicas de los reyes de Israel?
Kwa mambo mengine yanayomhusu Omri ambayo alfanya, na nguvu zake alizoonyesha, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
28 Cuando murió Omri fue enterrado en Samaria; y su hijo Acab se hizo rey en su lugar.
Kwa hiyo Omri akalala na mababu zake na akazikwa Samaria na Ahabu mwanae akawa mfalme mahali pake.
29 En el año treinta y ocho en que Asa era rey de Judá, Acab, hijo de Omri, se convirtió en rey de Israel. Y Acab fue rey en Samaria por veintidós años.
Katika mwaka wa thelathiini na nane wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akaanza kutawala juu ya Israeli. Ahabu mwana wa Omri akatawala Israeli kule Samaria kwa miaka ishirini na mbili.
30 Y Acab, hijo de Omri, hizo lo malo ante los ojos del Señor, aún peor que todos los que le precedieron.
Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo maovu mbele ya BWANA, zaidi ya wote waliokuwa kabla yake.
31 Y como si la copia de los malos caminos de Jeroboam, el hijo de Nebat, fuera una pequeña cosa para él, tomó como esposa a Jezabel, hija de Etbaal, rey de Sidón, y se convirtió en un sirviente y adorador de Baal.
Ikawa kidogo tu Ahabu ayaendee makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, kwa hiyo akamwoa Yezebeli binti wa Ethibaali, mfalme wa Wasidoni; akaenda akamwabudu baali na akamsujudia.
32 Y construyó un templo y un altar para Baal en Samaria.
Akamjengea madhabahu Baali, ambayo alikuwa ameijenga kule Samaria.
33 Acab hizo una imagen de Asera e hizo más que todos los reyes de Israel que estaban delante de él para hacer enojar al Señor, el Dios de Israel.
Ahabu akatengeneza Ashera. Ahabu akafanya maovu zaidi kumghadhabisha BWANA, Mungu wa Isareli, akamkasirisha kuliko wafalme wote wa Israeli waliokuwa kabla yake.
34 En sus días reedificó Hiel a Jericó; puso los cimientos a costa de Abiram, su hijo mayor, y puso sus puertas en el lugar a costa de su hijo menor, Segub; tal como el Señor había dicho por Josué, el hijo de Nun.
Katika siku zake Hieli Mbetheli aliijenga tena Yeriko. Akaijenga misingi ya mji kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa kwanza, naye akayajenga malango ya mji kwa kufiwa na mwanae mdogo Segebu, na walifanya hivi kwa sababu walitii neno la BWANA, ambalo alikuwa amelinena kwa kinywa cha Joshua mwana wa Nuni.