< 1 Corintios 10 >
1 Porque es mi deseo, hermanos míos, que guarden en mente cómo todos nuestros padres estaban debajo de la nube, y todos atravesaron el mar;
Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
2 Y todos ellos tuvieron el bautismo de Moisés en la nube y en el mar;
Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
3 Y todos tomaron la misma comida santa;
Wote walikula chakula kile kile cha roho,
4 Y la misma bebida santa; porque todos tomaron de las aguas de la roca santa que los seguía; y la roca era Cristo.
na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
5 Pero con la mayoría de ellos, Dios no se agradó, porque llegaron a su fin en el desierto.
Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
6 Ahora bien, estas cosas nos sirvieron de ejemplo, para que nuestros corazones no vayan tras las maldades, como lo hicieron.
Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
7 Entonces no vayan tras dioses falsos, como algunos de ellos lo hicieron; como se dice en las Sagradas Escrituras, después de descansar y comer, la gente se levantó a divertirse.
Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
8 No forniquemos, como algunos de ellos hicieron, de los cuales veintitrés mil terminaron en un día.
Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
9 Y no sometamos al Señor a prueba, como algunos de ellos lo hicieron, y vinieron a la muerte por medio de serpientes.
Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
10 Y no murmuren en contra del Señor, como algunos de ellos hicieron, y perecieron por él destructor.
Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
11 Ahora estas cosas fueron hechas como un ejemplo; y fueron escritos para nuestra amonestación, sobre quienes han llegado los últimos días. (aiōn )
Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn )
12 Entonces, que el que parece estar firme, mire que no caíga.
Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
13 Ustedes no han pasado por ninguna prueba, que no sea humanamente soportable. sino como lo que es común al hombre: y Dios es fiel, que no dejará que te caiga ninguna prueba a la que no puedas someterte; sino que dará juntamente con la tentación la salida, para que puedan soportar.
Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
14 Por esta causa, mis queridos hermanos, no den culto a dioses falsos.
Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
15 Lo que estoy hablando como a hombres sabios, juzguen ustedes mismos,
Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
16 La copa de bendición que bendecimos, ¿no nos da parte en la sangre de Cristo? y ¿no es el pan quebrado una parte del cuerpo de Cristo?
Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
17 Porque, siendo muchas personas, somos un solo pan, somos un solo cuerpo, porque todos participamos en un solo pan.
Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
18 Vean a Israel según la carne: ¿no toman parte en el altar los que toman como alimento las ofrendas del altar?
Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
19 ¿Digo, entonces, que lo que se ofrece a las imágenes es algo, o que la imagen es algo?
Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
20 Lo que digo es que las cosas ofrecidas por los gentiles se ofrecen a los demonios y no a Dios; y no es mi deseo que se hagan partícipes con los demonios.
La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
21 No es posible, al mismo tiempo, tomar la copa del Señor y la copa de los demonios; no pueden participar en la mesa del Señor y en la mesa de los demonios.
Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
22 ¿O podemos ser causa de envidia para el Señor? ¿Somos más fuertes que él?
Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
23 Somos libres de hacer todas las cosas, pero no todo conviene. Somos libres de hacer todas las cosas, pero no todo edifica.
“Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
24 No Dejen que un hombre preste atención solo a lo que es bueno para sí mismo, sino también al bien de su prójimo.
Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
25 De Todo lo que se vende en la carnicería, come, tómenla como alimento sin cuestionar si está bien o mal;
Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
26 porque la tierra es del Señor y su plenitud.
Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
27 Si un gentil hace un banquete para ti, y te agrada ir como invitado, toma todo lo que se te presenta, sin cuestionar si está bien o mal.
Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
28 Pero si alguien te dice: Este alimento ha sido usado como ofrenda, no lo tomes, a causa de él que lo dijo, y por motivos de conciencia; porque del Señor es la tierra y su plenitud.
Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
29 La conciencia, digo, no la tuya, sino la del otro hombre. Pues porque se ha de juzgar mi libertad por la conciencia de otro?
Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
30 Pero si doy gracias a Dios por la comida que tomo, porque me han de criticar por comerlo?
Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
31 Entonces, si se trata de comida o bebida, o cualquier otra cosa, hagas lo que hagas, hazlo todo para la gloria de Dios.
Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
32 No Sean piedra de tropiezo a los judíos, ni a los gentiles, ni a la iglesia de Dios.
Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
33 Así como yo procuro agradar a todos los hombres en todas las cosas, sin buscar ganancias para mí, sino para el bien de los demás, para que puedan obtener la salvación.
kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.