< 1 Crónicas 8 >
1 Benjamín fue el padre de Bela, su hijo mayor, Ashbel el segundo; y Ahara el tercero;
Benyamini akamzaa: Bela mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli mwanawe wa pili, Ahara mwanawe wa tatu,
2 Noha el cuarto; y Rapha el quinto;
Noha mwanawe wa nne na Rafa mwanawe wa tano.
3 Y Bela tuvo hijos, Adar, Gera, Abiud,
Wana wa Bela walikuwa: Adari, Gera, Abihudi,
4 Y Abisua y Naaman y Ahoa.
Abishua, Naamani, Ahoa,
5 Y Gera y Sefufan e Hiram.
Gera, Shefufani na Huramu.
6 Y estos son los hijos de Aod, jefes de familia de los que viven en Geba:
Hawa ndio wazao wa Ehudi, waliokuwa viongozi wa jamaa za wale walioishi huko Geba na ambao walihamishiwa Manahathi:
7 Y Naamán, Ahías, Gera; fue el padre de Uza y Ahihud.
Naamani, Ahiya na Gera. Gera alikuwa baba yao Uza na Ahihudi na ndiye aliwaongoza kwenda uhamishoni.
8 Y Saharaim se convirtió en el padre de los niños en el país de los moabitas, después de divorciar a Husim y Beera de sus esposas;
Shaharaimu aliwazaa wana katika nchi ya Moabu baada ya kuwapa talaka wake zake wawili yaani, Hushimu na Baara.
9 Y por su esposa Hodes, se convirtió en el padre de Jobab, Zibia, Mesa y Malcam.
Kwa mkewe Hodeshi, akawazaa wana saba: Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu,
10 Y Jeuz y Saquias y Mirma. Estos fueron sus hijos, jefes de familia.
Yeuzi, Sakia na Mirma. Hawa ndio waliokuwa wanawe, viongozi wa jamaa zao.
11 Y Husim fue el padre de Abitob y Elpaal.
Hushimu alimzalia: Abitubu na Elpaali.
12 Y los hijos de Elpaal: Eber, Misam y Semed él fue el constructor de Ono y Lod y sus aldeas;
Wana wa Elpaali walikuwa: Eberi, Mishamu, Shemedi (aliyeijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji vilivyoizunguka),
13 Y Bería y Sema, que eran jefes de las familias de los que vivían en Ajalón, que hicieron huir a las personas que viven en Gat;
na Beria na Shema, waliokuwa viongozi wa zile jamaa zilizokuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na ambao waliwafukuza wenyeji wa Gathi.
14 Y sus hermanos Sasac y Jeroham.
Wana wa Beria walikuwa Ahio, Shashaki, Yeremothi,
15 Y Zebadias, Arad, y Ader.
Zebadia, Aradi, Ederi,
16 Y Micael, Ispá, Joha, los hijos de Bería;
Mikaeli, Ishpa, na Yoha.
17 Y Zebadias y Mesulam, Hizqui, Heber.
Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi,
18 E Ismerai, Jezlias y Jobab, los hijos de Elpaal;
Ishmerai, Izlia na Yobabu ndio waliokuwa wana wa Elpaali.
19 Y Jaquim, Zicri, Zabdi.
Yakimu, Zikri, Zabdi,
20 Y Elienai, Ziletai, Eliel.
Elienai, Silethai, Elieli,
21 Y Adaías, Beraías y Simrat, hijos de Simei;
Adaya, Beraya na Shimrathi walikuwa wana wa Shimei.
22 E Islam, Heber y Eliel.
Wana wa Shashaki walikuwa Ishpani, Eberi, Elieli,
23 Y Abdon, Zicri y Hanan.
Abdoni, Zikri, Hanani,
24 Y Hananías, Elam y Anatotias.
Hanania, Elamu, Anthothiya,
25 Ifdaias y Peniel, los hijos de Sasac;
Ifdeya na Penueli.
26 Y Samserai, Seharia, y Atalias.
Shamsherai, Sheharia, Athalia,
27 Y Jaresias, Elías y Zicri, los hijos de Jeroham.
Yaareshia, Eliya na Zikri walikuwa wana wa Yerohamu.
28 Estos eran jefes de familia en sus generaciones: estos vivían en jerusalén.
Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao wakuu, kama ilivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
29 Y en Gabaón vivía el padre de Gabaón, Jehiel, cuya esposa se llamaba Maaca;
Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka.
30 Y su hijo mayor, Abdón, Zur, Cis, Baal, Ner, Nadab.
Mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
31 Y Gedor, Ahio, Zequer, y Miclot,
Gedori, Ahio, Zekeri,
32 Y Miclot fue el padre de Simea. Y vivían con sus hermanos en Jerusalén.
na Miklothi ambaye alikuwa baba yake Shimea. Hawa pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
33 Y Ner fue el padre de Cis, y Cis fue el padre de Saúl, y Saúl fue el padre de Jonatán, Malquisua, Abinadab y Es Baal.
Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli, Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
34 Y el hijo de Jonatán fue Merib-baal; y Merib-baal fue el padre de Micaia.
Yonathani akamzaa: Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
35 Y los hijos de Micaia: Pitón, Melec, Tarea y Acaz.
Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi.
36 Y Acaz fue el padre de Joada; y Joada fue el padre de Alemet, Azmavet y Zimri; y Zimri fue el padre de Mosa;
Ahazi akamzaa Yehoada. Naye Yehoada akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
37 Y Mosa fue el padre de Bina: Rafa fue su hijo, Elasa su hijo, Azel su hijo;
Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
38 Y Azel tuvo seis hijos, cuyos nombres son: Azricam, su hijo mayor, Bocru, Ismael y Searias y Obadiah y Hanan. Todos estos fueron los hijos de Azel.
Aseli alikuwa na wana sita; haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Aseli.
39 Y los hijos de Esec su hermano: Ulam su hijo mayor, Jehus el segundo; y Elifelet el tercero;
Wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti.
40 Y los hijos de Ulam eran hombres de guerra, expertos en el manejo de arcos, y tenían gran número de hijos y nietos, ciento cincuenta. Todos estos fueron los hijos de Benjamín.
Wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kutumia upinde. Alikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla yao 150. Hawa wote ndio walikuwa wazao wa Benyamini.