< 1 Crónicas 26 >

1 Para las divisiones de los guardianes de las puertas: de los Coreitas, Meselemías, el hijo de Coré, de los hijos de Ebiasaf.
Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Y Meselemias: tuvo hijos: Zacarías, el mayor; Jediael el segundo; Zebadías el tercero; Jatniel el cuarto;
Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 Elam, el quinto; Johanán, el sexto; Elioenai, el séptimo.
Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4 Y Obed-edom tuvo hijos: Semaías; el mayor; Jozabad, el segundo; Joa, el tercero; Sacar, el cuarto; Natanael, el quinto;
Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 Amiel, sexto; Isacar, séptimo; Peulatai octavo; porque la bendición de Dios estaba sobre él.
Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 Y su hijo Semaías tuvo hijos, gobernantes de la familia de su padre, porque eran hombres fuertes y valientes.
Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Los hijos de Semaías: Otni, Rafael Obed, Elzabad, cuyos hermanos eran grandes hombres de guerra, Eliú y Samaquias.
Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 Todos estos eran hijos de Obed-edom: ellos y sus hijos y sus hermanos, hombres valientes y fuertes para la obra; Sesenta y dos hijos de Obed-edom.
Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Meselemias tuvo hijos y hermanos, dieciocho hombres valientes.
Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 Y Hosa, hijo de los hijos de Merari: Simri el jefe (porque aunque no era el mayor, su padre lo hizo jefe);
Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Hilcías, el segundo; Tebalías, el tercero; Zacarías, el cuarto; Hosa tenía trece hijos y hermanos.
Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
12 Estas fueron las divisiones de los encargados de las puertas, hombres de autoridad, que tenían posiciones responsables como sus hermanos para servir en él templo del Señor.
Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 Y las familias fueron tomadas por la decisión del Señor por cada puerta; La pequeña familia tenía la misma oportunidad que la grande.
Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 Y el cuidado de la puerta en el este salió para Selemias. Entonces salió el nombre de su hijo Zacarías, un hombre sabio en la consejería, y se le dio la puerta del norte.
Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 A Obed-edom, en el sur; y a sus hijos, el almacén.
Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 A Supim y Hosa, la puerta del oeste, junto a la puerta de Salequet, en la acera que sube, guardia contra guardia.
Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
17 Al este había seis levitas al día, y al norte y al sur cuatro al día, y al almacén dos y dos.
Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 Por él atrio, en el oeste, cuatro en el pasillo y dos en el atrio.
Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Estas fueron las divisiones de los guardianes de las puertas, de los hijos de los Core y de los hijos de Merari.
Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 Y los levitas, sus hermanos, eran responsables de los tesoros del templo de Dios y de los tesoros de las las cosas santificadas.
Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 Los hijos de Laadan: hijos de Gersón de la familia de Laadan, jefes de familia de Laadan y Jehiel.
Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 Los hijos de Jehiel: Zetam y Joel, su hermano, tenían el cuidado de los tesoros del templo del Señor.
wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
23 De los descendientes de Amram, Izahar, Hebron, y Uziel,
Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
24 Y Sebuel, descendiente de Gersón, y de Moisés, era el controlador de los tesoros.
Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 Y sus hermanos: de Eliezer, Rehabías, su hijo; y Jesahias, su hijo, y Joram su hijo, y Zicri su hijo, y Selomit su hijo.
Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Selomit y sus hermanos eran responsables de todas las cosas sagradas que David el rey y los jefes de familia, los capitanes de miles y cientos y los capitanes del ejército habían dado al Señor.
Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 De los bienes tomados en la guerra, dieron, como una ofrenda sagrada, materiales para la construcción de la casa del Señor.
Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
28 Y todo lo que Samuel el profeta y Saúl, hijo de Cis, y Abner, hijo de Ner, y Joab, hijo de Sarvia, Todo lo santificado; Lo que sea que alguien haya dado, estaba bajo el cuidado de Selomit y sus hermanos.
Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 De los Izhar, Quenanías y sus hijos tuvieron que hacer todos los asuntos públicos de Israel, en relación con los jueces y los hombres en autoridad.
Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 De los Hebrón, Hasabias y sus hermanos, setecientos cien hombres capaces, eran supervisores de Israel al otro lado del Jordán, al oeste, siendo responsables de toda la obra del templo del Señor y de la obra realizada por los siervos del rey.
Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
31 De los de Hebron, Jerías era el jefe de todos los hebronitas, en sus generaciones por familias. En el cuadragésimo año del gobierno de David se hizo una búsqueda, y se vieron hombres capaces entre ellos en Jazer de Galaad.
Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 Y sus hermanos eran dos mil setecientos hombres capaces, jefes de familia, a quienes el rey David hizo supervisores sobre los de Rubén y los de Gad y la media tribu de Manasés, en todo lo relacionado con Dios, y para todos los asuntos del rey.
Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.

< 1 Crónicas 26 >