< Proverbios 9 >

1 La sabiduría edificó su casa, labró sus siete columnas;
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 mató su víctima, templó su vino, y puso su mesa.
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 Envió sus criadas; sobre lo más alto de la ciudad clamó:
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 cualquier simple, venga acá. A los faltos de entendimiento ( o de corazón ) dijo:
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 Venid, comed mi pan, y bebed del vino que yo he templado.
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Dejad las simplezas, y vivid; y andad por el camino de la inteligencia.
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 El que castiga al burlador, afrenta se acarrea; el que reprende al impío, se atrae mancha.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 No castigues al burlador, para que no te aborrezca; castiga al sabio, y te amará.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Da al sabio, y será más sabio; enseña al justo, y acrecerá su saber.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 El temor del SEÑOR es el principio de la sabiduría; y la ciencia de lo santo es inteligencia.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 Porque por mí se aumentarán tus días, y años de vida se te añadirán.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 Si fueres sabio, para ti lo serás; mas si fueres burlador, pagarás tú solo.
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 La mujer loca, alborotadora, simple e ignorante;
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 se sienta en una silla a la puerta de su casa, en lo alto de la ciudad,
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 para llamar a los que pasan por el camino; a los que enderecen sus caminos:
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 Cualquier simple, venga acá. A los faltos de entendimiento dijo:
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 Las aguas hurtadas son dulces, y el pan comido en oculto es suave.
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 Y no saben que allí están los muertos; que sus convidados están en los profundos de la sepultura. (Sheol h7585)
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbios 9 >